Hadithi za Maandiko
Sura ya 2: Mariamu na Malaika


Sura ya 2

Mariamu na Malaika

Mariamu na Yusufu

Mariamu na Yusufu waliishi Nazareti. Walikuwa watu wema sana. Walipendana na walikuwa waoane.

Luka 1:26–27

malaika akizungumza na Mariamu

Siku moja malaika Gabrieli alimjia Mariamu. Alimwambia Mariamu kwamba Mungu angembariki.

Luka 1:26, 28–30

malaika akizungumza na Mariamu

Gabrieli alimwambia Mariamu kwamba angekuwa mama wa Mwana wa Mungu. Jina lake lingekuwa Yesu, na angekuwa Mfalme wa watu wote wenye haki.

Luka 1:31–33

malaika akizungumza na Mariamu

Mariamu alisema kwamba angemtii Baba wa Mbinguni na kuwa mama wa Yesu.

Luka 1:34–35, 38; 1 Nefi 11:18–21