Sura ya 2
Mariamu na Malaika
Mariamu na Yusufu waliishi Nazareti. Walikuwa watu wema sana. Walipendana na walikuwa waoane.
Luka 1:26–27
Siku moja malaika Gabrieli alimjia Mariamu. Alimwambia Mariamu kwamba Mungu angembariki.
Luka 1:26, 28–30
Gabrieli alimwambia Mariamu kwamba angekuwa mama wa Mwana wa Mungu. Jina lake lingekuwa Yesu, na angekuwa Mfalme wa watu wote wenye haki.
Luka 1:31–33
Mariamu alisema kwamba angemtii Baba wa Mbinguni na kuwa mama wa Yesu.
Luka 1:34–35, 38; 1 Nefi 11:18–21