Hadithi za Maandiko
Sura ya 32: Petro Anashuhudia juu ya Kristo


Sura ya 32

Petro Anashuhudia juu ya Kristo

Yesu akiwafundisha wanafunzi

Yesu aliwauliza wanafunzi Wake watu walidhani Yeye ni nani.

Mathayo 16:13; Marko 8:27; Luka 9:18

wanafunzi wakizungumza na Yesu

Wanafunzi walijibu kwamba baadhi ya watu walidhani Yesu alikuwa Yohana Mbatizaji. Wengine walidhani alikuwa nabii wa Agano la Kale aliyekuwa amefufuka.

Mathayo 16:14; Marko 8:28; Luka 9:19

Petro akizungumza

Yesu aliwauliza wanafunzi Wake walidhani Yeye alikuwa ni nani. Petro alisema, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”

Mathayo 16:15–16; Marko 8:29; Luka 9:20

Yesu akizungumza na wanafunzi

Yesu alieleza kwamba ushuhuda wa Petro haukuja kutoka kwa mafundisho ya watu. Ushuhuda wake ulikuwa umekuja kwa ufunuo kutoka kwa Mungu.

Mathayo 16:17

Yesu akizungumza na Petro

Yesu alimwahidi Petro kwamba angempa ukuhani na mamlaka ya kuongoza Kanisa Lake. Kisha Petro na wanafunzi wangekuwa na mamlaka ya kuanzisha Kanisa la Yesu duniani.

Mathayo 16:18–19

Yesu amesimama kando ya Petro

Yesu aliwaambia wanafunzi Wake wasimwabie yeyote kwanza kwamba Yeye alikuwa ndiye Kristo. Kwanza alihitaji kuteseka, kuuwawa, na kufufuka siku ya tatu.

Mathayo 16:20; Marko 8:30–31; Luka 9:21–22