Hadithi za Maandiko
Sura ya 49: Sakramenti ya Kwanza


Sura ya 49

Sakramenti ya Kwanza

familia ikila mlo pamoja

Kila mwaka Wayahudi walikuwa na karamu iliyoitwa Pasaka. Iliwasaidia Wayahudi kukumbuka kwamba Mungu alikuwa amewaokoa mababu zao katika siku za Musa.

Kutoka 12:27; Luka 22:7

Yesu na Mitume wakitembea

Yesu na Mitume Kumi na Wawili walihitaji mahali pa kula karamu ya Pasaka. Mwokozi aliwatuma Petro na Yohana kutafuta chumba na kuhakikisha kwamba kila kitu kilikuwa tayari kwa ajili ya karamu.

Luka 22:8

Mitume mlangoni

Walipata chumba na kuandaa karamu.

Luka 22:9–13

Yesu na Mitume wakila karamu ya Pasaka

Yesu na Mitume wote walienda pale. Walikula karamu ya Pasaka pamoja.

Luka 22:14

Yesu akibariki mkate

Yesu aliwapa Mitume Wake sakramenti kwa mara ya kwanza. Alichukua mkate mikononi Mwake, akaubariki, na kisha akaumega vipande vipande. Aliwaambia Mitume wale mkate.

Mathayo 26:26; Luka 22:19

Yesu akimega mkate

Yesu aliwaambia wafikirie juu ya mwili Wake wakati wakila mkate. Aliwasihi wakumbuke kwamba angekufa kwa ajili yao.

Mathayo 26:26; Luka 22:19

Yesu akimimina divai

Yesu alimimina divai katika kikombe. Alibariki divai na kuwaambia Mitume wainywe.

Mathayo 26:27

Yesu akipitisha bilauri kwa mzunguko

Yesu aliwaambia wafikirie juu ya damu Yake wakati walipokunywa divai. Aliwasihi wakumbuke kwamba angemwaga damu na kuteseka kwa ajili ya dhambi za watu wote.

Mathayo 26:28; Luka 22:20

Yesu akiwafundisha Mitume

Yesu pia aliwaambia Mitume kwamba watu waovu punde wangemwua. Mitume Kumi na Mmoja walikuwa na huzuni sana. Walimpenda Mwokozi na hawakutaka afe. Yesu alijua kwamba mmoja wa Mitume angewasaidia wale watu waovu. Jina lake lilikuwa Yuda Iskariote.

Mathayo 26:2, 14–16, 21–25