Hadithi za Maandiko
Sura ya 45: Senti za Mjane


Sura ya 45

Senti za Mjane

mtu akiweka pesa ndani ya sanduku

Yesu alienda hekaluni huko Yerusalemu. Alitazama watu wakitoa pesa kwa ajili ya kanisa. Watu wengi matajiri walitoa pesa nyingi.

Marko 12:41

mwanamke akiweka sarafu ndani ya sanduku

Mjane maskini alitoa vipande viwili vya pesa vilivyoitwa senti. Haikuwa pesa nyingi sana, lakini ilikuwa pesa yote ambayo alikuwa nayo.

Marko 12:42, 44

Yesu akizungumza

Yesu alimwona mjane na akawaambia wanafunzi nini alichokuwa amefanya.

Marko 12:43

mtu akihesabu pesa

Alisema watu matajiri walikuwa wametoa kiasi kikubwa zaidi cha pesa kuliko kile mjane alichokuwa ametoa, lakini walikuwa na zaidi za kutoa.

Marko 12:43–44

mwanamke akiondoka hekaluni

Mjane hakuwa na pesa nyigine zaidi. Alitoa zote alizokuwa nazo. Alitoa zaidi kwa Mungu kuliko watu wote matajiri.

Marko 12:44