Sura ya 45
Senti za Mjane
Yesu alienda hekaluni huko Yerusalemu. Alitazama watu wakitoa pesa kwa ajili ya kanisa. Watu wengi matajiri walitoa pesa nyingi.
Marko 12:41
Mjane maskini alitoa vipande viwili vya pesa vilivyoitwa senti. Haikuwa pesa nyingi sana, lakini ilikuwa pesa yote ambayo alikuwa nayo.
Marko 12:42, 44
Yesu alimwona mjane na akawaambia wanafunzi nini alichokuwa amefanya.
Marko 12:43
Alisema watu matajiri walikuwa wametoa kiasi kikubwa zaidi cha pesa kuliko kile mjane alichokuwa ametoa, lakini walikuwa na zaidi za kutoa.
Marko 12:43–44
Mjane hakuwa na pesa nyigine zaidi. Alitoa zote alizokuwa nazo. Alitoa zaidi kwa Mungu kuliko watu wote matajiri.
Marko 12:44