Fumbo la Kwanza
Kondoo Aliyepotea
Mchungaji mwema alikuwa na kondoo 100. Mmoja wao alikuwa amepotea.
Luka 15:4
Mchungaji aliwaacha wale kondoo 99 kumtafuta yule mmoja aliyepotea. Alipompata, alikuwa na furaha sana.
Luka 15:4–5
Mchungaji alimbeba kondoo kumleta nyumbani. Aliwaita rafiki zake wote na majirani waje na kufurahia pamoja naye. Alikuwa amempata kondoo aliyepotea.
Luka 15:5–6
Yesu Kristo aliwaambia Mafarisayo kile ambacho fumbo lilimaanisha. Alisema kwamba wale wanaotenda dhambi ni kama kondoo aliyepotea.
Luka 15:7
Kama vile mchungaji alivyotaka kumuokoa kondoo aliyepotea, Yesu anataka kuwaokoa wale wanaotenda dhambi.
Marko 2:17
Yesu alisema kwamba hiyo ndiyo sababu alikuwa akizungumza na wenye dhambi.
Mathayo 18:11 (ona rejeo chini ya ukurasa 11c); Marko 2:17
Na kama vile mchungaji alivyokuwa na furaha alipompata kondoo aliyepotea, Yesu hufurahia pale tunapotubu.
Luka 15:6–7