“Njia Rahisi za Kuwa Zaidi Kama Kristo katika Utumishi Wetu,” Liahona, Julai 2025.
Njia Rahisi za Kuwa Zaidi Kama Kristo katika Utumishi Wetu
Fursa zimetuzunguka kote za kutumikia kama ambavyo Mwokozi angetumikia.
Kielelezo na Jen Tolman
Kazi ya utumishi, iliyotumwa kutoka mbinguni kama ilivyo, sio ngumu. Kutoa uangalifu zaidi na kujali huja chini kwa mazoea machache ya msingi ambayo, yanapofikiriwa kwa makini, husaidia “kuinua macho yetu ya kiroho kuelekea kuishi sheria ya upendo ulimwenguni kote.”
Tunashauriwa “kuwalinda watu [wetu], na … kuwalisha kwa vitu vilivyohusu utakatifu” (Mosia 23:18). Baadhi ya njia muhimu za utumishi zinajumuisha:
-
Kuwafikia wao. Hivi ndivyo fursa za kutumikia zinavyofunguliwa.
-
Waache wao wajue unajali kwa kujifunza kuwahusu wao na kukuza huruma.
-
Sali kwa ajili ya fursa za kutumikia na kutafuta mwongozo wa kiungu ili kujua mahitaji yao.
-
Kuwa karibu nao na kuwa wenye kuwasiliana mara kwa mara ili uweze kujiandaa kuwahudumia.
Fursa ziko pande zote za kutumikia kama ambavyo Mwokozi angefanya. Hapa kuna mifano minne inayo angazia utumishi kama wa Kristo.
Pata Kuwajua Wengine
Na Francisco Lázaro Campos de Sousa, Brazil
Wakati wa mkutano wa urais wa akidi ya wazee, nilihisi hamu ya kukutana na mshiriki wa akidi ambaye hakuwa mshiriki hai, mtu ambaye sijawahi kukutana naye. Siku moja baada ya kununua vitu nilihisi msukumo wa kwenda nyumbani kwake. Nilisita, lakini hisia za kukutana naye zilizidi kuongezeka. Nilijitambulisha mwenyewe na kusema mambo yaliyokuja akilini mwangu. Nilimwambia kwamba Bwana alimhitaji, na yeye alimhitaji Bwana.
Alishiriki maumivu yake ya upweke na magumu mengine. “Utapata marafiki katika akidi ambao watasaidia na kukidhi,” nilimwambia. Kwa urahisi alikubali mwaliko wangu na kuhudhuria mikutano ya Sabato.
Sikumjua mwanzoni, lakini Bwana alimjua na kuhisi moyo wake. Imani yangu ilithibitishwa tena. Tunapowatumikia watoto wa Baba yetu na kuomba ili kujua shida zao, Bwana hutuongoza kwao. Tunashiriki katika uzoefu wa furaha wa “inyooshe mikono iliyolegea, na yaimarishe magoti yaliyo dhaifu” (Mafundisho na Maagano 81:5).
Wafikie Wengine
Na Ana Rodriguez Ramirez, Uhispania
Siku moja katika misheni yangu, mimi na mwenzangu tulishawishiwa kumtembelea dada katika kata. Tulikata mioyo ya karatasi na kuandika jumbe za upendo juu yake ili kumkumbusha juu ya thamani yake.
Tulifika nyumbani kwake, tukifikiri asingekuwa nyumbani. Tulipokuwa tunaweka mioyo ile ya karatasi, gari lake lilifika nyumba. Mimi na mwenzangu tulijaribu kujificha ili kuendelea na mshangao wa kirafiki, lakini bila mafanikio. Alituona.
Dada huyo alitoka nje ya gari lake akiwa na machozi usoni mwake. Alitukumbatia na kusema, “Ninyi wawili ni malaika zangu. Daima mko pale ninapowahitaji zaidi. Asanteni.”
Alitualika ndani na kutuambia juu ya siku ndefu aliyokuwa akikabiliana na hali mbaya ya kifamilia. Tulimsikiliza tu. Tulishiriki jinsi Mungu anavyompenda na kwamba Yeye hajasahau kuhusu kile alichokuwa akipitia. Tunasoma maandiko pamoja naye, na nyumba yake ilijawa na Roho Mtakatifu wakati tulipoondoka.
Wanafunzi wa Yesu Kristo “wako tayari … kuwafariji wale ambao wanahitaji kufarijiwa” (Mosia 18:9). Anatutumainia sisi kuwa sehemu ya kazi Yake kuu—utumishi wa juu na mtakatifu zaidi. Tunapochukua muda kuwajua watu na kuwasikiliza, tunakuwa na uwezo zaidi wa kuwa malaika wa Mungu walio duniani.
Mwakilishe Mwokozi
Na Talia Rodríguez, Uswisi
Sala ni sehemu muhimu ya utumishi kama Mwokozi. Sala inaweza kuanza upekuzi wetu ili kujua nani wa kumbariki. Inaweza kutusaidia kuja kuelewa mapenzi ya mbinguni kuhusu jinsi ya kubariki. Sala pia ni hatua muhimu katika kujifunza jinsi ya kutekeleza wajibu wetu.
Mume wangu, Mario, aliteseka na UVIKO katika siku za mwanzo za ugonjwa huu kabla ya chanjo. Askofu alimwomba mzee katika kata yetu, Moroni, kumpa baraka ya ukuhani.
Kwa sababu hakutaka kuambukizwa virusi na kuvisambaza kwa familia yake, Moroni alihitaji uthibitisho wa mbinguni kabla ya kuendelea. Alipiga magoti kusali pamoja na mke wake, akisubiri hakikisho la amani. Walipohisi amani, mke wake alimwambia, “Nenda na silaha zako, Moroni.”
Alipoingia nyumbani kwetu, tulimwona shujaa wa Bwana. Mume wangu alimwaga machozi ya furaha alipomwona kaka kwa ujasiri akija kumpa baraka aliyotamani. Ilikuwa ni uzoefu usio elezeka.
Mwokozi alikuja kupitia mtumishi Wake, kaka yetu mpendwa Moroni, ambaye aliweka mikono yake juu ya kichwa cha Mario na kumbariki kama ambavyo Kristo angefanya.
Wasaidie Kupokea Baraka za Maagano
Na Geiziane Morais Freitas Duarte, Brazili
Wakati mmoja nilimtumikia dada ambaye alikuwa ameacha kuhudhuria kanisa. Nilipomtembelea, ningeshiriki jinsi Mwokozi alivyompenda yeye na familia yake. Daima ningewaalika waje kanisani Jumapili iliyofuata. Mazoezi haya yaliendelea kwa muda mrefu, lakini kamwe hawakuja. Nilihisi kukata tamaa. Jaribu la kukata tamaa lilikuwa la nguvu sana. Lakini kila wakati mwenza wangu na mimi tulipotembelea nyumba yao, tulikuwa na taswira ya mbinguni. Daima tungewaona wao hekaluni, wakiwa wamevalia mavazi meupe. Tulijua tulipaswa kuendelea kujaribu.
Baada ya sala nyingi na matembezi, siku hatimaye ilikuja—familia ilikuja kanisani! Waliendelea kurudi kila wiki. Familia ilifanya kazi kwa bidii ili kukuza imani yao na kufika kwenye njia ya agano. Ilikuwa dhahiri kwamba injili ilikuwa imewaimarisha.
Hatimaye, nilipokea mwaliko wa kuunganishwa kwao hekaluni. Nilipokuwa nikitazama ibada hii takatifu, sikuweza kujizuia kumwaga machozi ya furaha. Ulikuwa ni muujiza.
Wakati mwingine nilitaka kukata tamaa. Lakini kila mara nilipowatembelea, niliona hekalu. Mungu alinionyesha taswira ya mpango Wake kwa ajili ya familia hii. Yeye alinitumia kama chombo Chake cha kuwasiliana nao. Ninamshukuru Yeye kwa kunionyesha ono la kweli la utumishi.
Kufuata Mpangilio wa Kristo
Shangwe na nguvu ya utumishi hupatikana tunapokuwa baraka katika maisha ya mtu fulani, tukiwahudumia kama ambavyo Mwokozi angefanya. Rais Mkuu wa Muungano wa Usaidizi Camille N. Johnson alifundisha kwamba “wakati wowote unapofanya chochote ili kuleta faraja kwa wengine—kimwili au kiroho— … unawaletea upendo wa Yesu Kristo. Ninashuhudia kwamba unapofanya hivyo, utabarikiwa kupata faraja yako mwenyewe Kwake.”
Tunakuwa zaidi kama Mwokozi katika uhudumiaji wetu tunapomgeukia Bwana kwa ajili ya msaada katika juhudi zetu. Tunafuata misukumo, kupata kuwajua wale tunao wahudumia, kuwaombea, kuwasaidia kufanya na kushika maagano, na kuendelea katika juhudi zetu.
Uhudumiaji wa Mwokozi—mmoja mmoja—ni mpangilio mzuri kwa ajili yetu wenyewe (ona 3 Nefi 11:15). Kama Mzee Juan Pablo Villar wa Sabini alivyofundisha: “Kama tutamfuata Yesu Kristo—Bwana mtumishi—na kuwatumikia wengine kama ambavyo Yeye angefanya, Yeye atatuimarisha na kutuwezesha. Kupitia utumishi wetu, tunaweza kubariki maisha ya wengine na kupata amani na shangwe kwa ajili yetu wenyewe.”