Kikao cha Jumamosi Mchana
Kufunganisha Mapenzi Yetu na Yake
Dondoo
Rafiki zangu wapendwa, tunapochagua kuacha Mungu awe ushawishi wenye nguvu zaidi katika maisha yetu juu ya shughuli za utafutaji wa kuridhisha nafsi zetu, tunaweza kupiga hatua katika ufuasi wetu na kuongeza uwezo wetu wa kuunganisha akili na moyo wetu kwa Mwokozi. Kwa upande mwingine, tusiporuhusu njia ya Mungu ishinde katika maisha yetu, tunaachwa peke yetu, na bila mwongozo wa kiungu wa Bwana, tunaweza kuhalalisha karibu chochote tunachofanya au tusichofanya. Tunaweza pia kujitengenezea visingizio kwa kufanya mambo kwa njia yetu wenyewe, tukisema kwa kuhalalisha, “Ninafanya tu mambo kwa njia yangu.” …
… Wakati hali binafsi kama vile vinasaba, jiografia, na changamoto za kimwili na kiakili huathiri safari yetu, katika mambo ambayo kwa kweli ni muhimu, kuna nafasi ya ndani ambapo tuko huru kuchagua kama tutaamua kufuata mpangilio ambao Bwana ameuandaa kwa ajili ya maisha yetu ama la. …
Kama wafuasi wa Kristo, tunatamani kutembea njia aliyoiwekea alama kwa ajili yetu wakati wa huduma Yake duniani. Hatutamani tu kufanya mapenzi Yake na yote yatakayompendeza Yeye bali pia tunatafuta kuiga Mfano Wake. …
Ninashuhudia kwenu kwamba kufuata mapenzi ya Bwana katika maisha yetu kutatuwezesha kupata lulu ya thamani kuu ulimwenguni—ufalme wa mbinguni. Ninaomba kwamba kila mmoja wetu, katika wakati wetu na zamu yetu, tutaweza kutangaza, kwa ujasiri wa agano, kwa Baba yetu wa Mbinguni na Mwokozi Yesu Kristo kwamba “kile kinachofanya kazi Kwako, kinafanya kazi kwangu.”