Katika Kipindi Kisicho cha Miaka Mingi
Dondoo
Kitabu cha Mormoni kimsingi si kumbukumbu ya kihistoria ambayo inaangazia yaliyopita. Badala yake, kitabu hiki cha maandiko kinaangalia siku zijazo na kina kanuni muhimu, maonyo, na masomo yaliyokusudiwa kwa ajili ya hali na changamoto za siku zetu. Kwa hivyo, Kitabu cha Mormoni ni kitabu kuhusu mustakabali wetu wa baadaye na nyakati ambazo kwa sasa tumo na ambazo tutakuwamo. …
Sauti za kale kutoka mavumbini zinatusihi leo tujifunze somo hili la milele: ustawi, mali, na raha hutengeneza mchanganyiko wenye nguvu ambao unaweza kusababisha hata wenye haki kunywa sumu ya kiroho ya kiburi. …
… Lazima tujilinde siku zote dhidi ya hisia-shawishi za kiburi na za kujipendelea kupitiliza, kujitathimini kwetu kusiko sawa juu ya uwezo wetu na kujiona wenyewe, na kujijali wenyewe badala ya kuwatumikia wengine.
Naomba nipendekeze kwamba kama wewe au mimi tunaamini tuna nguvu vya kutosha na ni waumini hodari kuepuka dharau ya kiburi, basi labda tayari tunasumbuliwa na ugonjwa huu hatari wa kiroho. …
Ikiwa, hata hivyo, wewe au mimi tunaamini tunaweza kuathiriwa na kiburi, basi tutafanya kila wakati mambo madogo na rahisi ambayo yatatulinda na kutusaidia tuwe “kama mtoto, mtiifu, mpole, mnyenyekevu, mvumilivu, aliyejaa upendo, aliye tayari kutii vitu vyote ambavyo Bwana anaona vinafaa kutuletea [sisi]” [Mosia 3:19].
… Tunapojifunza na kutafakari [Kitabu cha Mormoni], tutabarikiwa kwa macho ya kuona, masikio ya kusikia, uwezo wa kupambanua na mioyo ya kuelewa masomo tunayopaswa kujifunza ili “kujihadhari na kiburi, kwamba [tusiingie] katika majaribu.” [Mafundisho na Maagano 23:1].