2024
Rahisi Ni Mafundisho ya Yesu Kristo
Novemba 2024


Kikao cha Jumapili Asubuhi

Rahisi Ni Mafundisho ya Yesu Kristo

Dondoo

bango

Pakua PDF

Neno la Mungu ni mafundisho yanayofundishwa na Yesu Kristo na manabii Wake. …

… Fundisho hili ni kwamba imani katika Bwana Yesu Kristo, toba, ubatizo, kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu na kuvumilia hadi mwisho huwabariki watoto wote wa Mungu.

Tunapofundisha kanuni hizi kwa wale tunaowapenda, Roho Mtakatifu atatusaidia tuujue ukweli. Kwa sababu tunahitaji maongozi ya Roho Mtakatifu, ni lazima tuepuke udadisi au tafsiri binafsi ambavyo vinapitiliza mafundisho ya kweli.

… Njia moja ya hakika zaidi ya kuzuia hata kukaribia tu mafundisho ya kupotosha ni kuchagua kurahisisha kufundisha kwetu. …

Kufundisha kwa urahisi huturuhusu kushiriki mafundisho ya kuokoa mapema, wakati watoto wakibaki bila kuguswa na vishawishi vya mdanganyifu ambavyo vitawakabili baadaye, muda mrefu kabla ya kweli wanazohitaji kujifunza kuzimishwa na kelele za mitandao ya kijamii, makundi rika na mapambano yao binafsi. …

Tunapofanya tuwezavyo kuwafundisha wale tunaowapenda kuhusu mafundisho ya Yesu Kristo, wengine wanaweza bado wasiitikie. Mashaka yanaweza kuingia akilini mwako. … Usikubali mashaka hayo. Mgeukie Mungu akusaidie. …

… Utakuwa mwenye bidii na mvumilivu. Na kisha unaweza kujua kwamba umefanya yote unayoweza ili kuwasaidia wale unaowapenda na wale unaowaombea wavuke jaribio la Shetani la kuwapotosha.