Kikao cha Jumamosi Asubuhi
Ishi Kulingana na Fursa Zako
Dondoo
Ibada za ukuhani na ahadi za maagano humruhusu Mungu kututakasa na kisha kutenda maajabu katika maisha yetu. Lakini hii inatokeaje?
Kwanza, ili ibada idhihirishe nguvu za Mungu katika maisha yetu, lazima ifanyike kwa mamlaka kutoka kwa Mwana wa Mungu. …
Pili, hatufanyi tu ahadi za agano—lazima tuzishike. …
Wakati Nabii Joseph alipokuwa akifundishwa kuhusu funguo, ofisi, ibada, na jinsi ya kusaidia katika huduma ya ukuhani, Bwana Mwenyewe, kupitia nabii Wake, alitoa ufunuo kwa Emma. …
Ikiwa tutasoma sehemu ya 25 kwa makini, tunagundua upigaji hatua muhimu ukifanyika. Emma angeenda kutoka kuwa binti katika ufalme hadi kuwa “mwanamke mteule” hadi malkia. Ibada za Ukuhani wa Haruni na Melkizedeki, zikiunganishwa na ushikaji wa Emma wa maagano, zingeongeza wenzi wake wa Roho na malaika, zikimwezesha kusafiri katika maisha yake kwa mwongozo mtakatifu. …
… Hiki ni kitu ambacho ninataka kila msichana katika ufalme aelewe.
“Ishi kulingana na fursa zako.”
Jifunze jinsi ibada za ukuhani na ahadi za maagano zitakavyoruhusu nguvu za Mungu kutiririka katika maisha yako kwa ufanisi mkubwa, zikifanya kazi ndani yako na kupitia wewe, zikikuwezesha na kukutayarisha ufikie lengo na uwezekano wako wote. …
Sisi sote tunaweza kufikia kipawa cha nguvu za Mungu.
Kila wakati tunapopokea sakramenti.
Kila wakati tunapovuka kizingiti cha hekalu.
Hii ndiyo fokasi ya Sabato yangu. Hii ndiyo sababu ninathamini kibali changu cha hekaluni.
“Katika maagano na ibada za Hekaluni, nguvu za uchamungu hujidhihirisha” (Mafundisho na Maagano 84:20).