Njoo, Unifuate
Mei 18–24. “Uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa”: Yoshua 1–8; 23–24


“Mei 18–24. ‘Uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa: Yoshua 1–8; 23–24:” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)

“Mei 18–24. ‘Uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa’” Njoo, Unifuate: Agano la Kale 2026

Musa akimbariki Yoshua

Musa Akimtawaza Yoshua, na Darrell Thomas (utondoti)

Mei 18–24: “Uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa”

Yoshua 1–8; 23–24

Ilikuwa imechukua vizazi vingi, lakini ahadi ya Bwana ilikuwa karibu kutimizwa: wana wa Israeli walikuwa hatimaye wanakwenda kurithi nchi ya ahadi. Ila katika njia yao ulisimama Mto Yordani, kuta za Yeriko, na watu wenye nguvu waliomkataa Bwana (ona 1 Nefi 17:35). Na wangelazimika kukabiliana na hayo yote bila kiongozi wao mpendwa Musa. Hali ingewafanya baadhi ya Waisraeli kujihisi dhaifu na waoga, ila Bwana alisema, “Uwe hodari na wenye moyo wa ushujaa.” Ni sababu gani waliyokuwa nayo ya kuwa wajasiri? Haikuwa kwa sababu ya nguvu zao wenyewe—au hata za Musa au Yoshua—ila kwa sababu “Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako” (Yoshua 1:9). Tunapokuwa na mito yetu ya kuvuka na kuta za kubomoa, vitu vya ajabu vinaweza kutokea katika maisha yetu, kwa sababu ni “Bwana [ambaye] atatenda mambo ya ajabu miongoni [mwetu]” (Yoshua 3:5).

Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Yoshua, ona “Yoshua, kitabu cha” katika Kamusi ya Biblia.

ikoni ya kujifunza

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Yoshua 1:1–9

Mungu atakuwa pamoja nami ninapojitahidi kuwa mwaminifu Kwake.

Fikiria jinsi ambavyo ingalikuwa kwa Yoshua kuitwa kuwa mbadala wa Musa. Angalia nini Bwana alichosema katika Yoshua 1:1–9 ili kumpa moyo. Fikiria kuhusu changamoto ngumu unazokabiliana nazo; kuna nini katika mistari hii kinachokupatia ujasiri?

Jina Yoshua (Yehoshua au Yeshua kwa Kiebrania) humaanisha “Yehova anaokoa.” Na jina Yesu linatoka katika neno Yeshua. Kwa hiyo unaposoma kuhusu Yoshua, fikiria wajibu wake katika kuwaongoza wana wa Israeli kuvuka Mto Yordani na kuingia nchi ya ahadi. Ni kwa jinsi gani misheni yake ilikuwa sawa na kile Kristo anachofanya kwa ajili yetu?

Yoshua 1:8

ikoni ya seminari
Neno la Mungu linaweza kuifanya njia yetu iwe yenye mafanikio.

Alivyomtia moyo Yoshua, Bwana alitoa ushauri katika Yoshua 1:8 kuhusu maandiko, au “neno la sheria.” Ukizingatia majukumu mazito ya Yoshua, kwa nini ushauri huu ungeweza kuwa hususani wenye msaada?

Wakati Bwana anapotualika tusome maandiko, mara nyingi Yeye hutumia maneno ambayo huenda zaidi ya kusoma tu. Yeye pia anaahidi baraka kubwa. Jedwali hapa chini linaweza kukusaidia kugundua mialiko hii na baraka zilizoahidiwa:

Mwaliko

Baraka Zilizoahidiwa

Yoshua 1:8

Mwaliko

Tafakari mchana na usiku

Baraka Zilizoahidiwa

1 Nefi 15:23–24

Mwaliko

Baraka Zilizoahidiwa

2 Nefi 32:3

Mwaliko

Baraka Zilizoahidiwa

Mosia 1:7

Mwaliko

Baraka Zilizoahidiwa

Stawi katika nchi

Helamani 3:29–30

Mwaliko

Baraka Zilizoahidiwa

Mafundisho na Maagano 84:85

Mwaliko

Baraka Zilizoahidiwa

Russell M. Nelson, “Msikilize Yeye,” Liahona, Mei 2020, aya ya mwisho kwenye ukurasa wa 89

Mwaliko

Baraka Zilizoahidiwa

Ni kwa jinsi gani Bwana ametimiza ahadi hizi katika maisha yako? Sasa unaweza kuwa wakati mzuri wa kutathmini tabia zako za kujifunza maandiko. Nini kinaendelea vizuri?” Je, unahisi kutiwa msukumo kufanya nini ili kuwa na uzoefu wa maana zaidi wa neno la Mungu?

Ona pia:“Ninapopekua Maandiko Matakatifu,” Nyimbo za Dini, na. 159.

Yoshua 2

Vyote imani na matendo ni muhimu kwa wokovu.

Wakristo wa Agano Jipya walimwona Rahabu kama mfano wa nguvu ya vyote viwili imani na matendo (ona Waebrania 11:31; Yakobo 2:25). Unaposoma Yoshua 2, fikiria wajibu wa imani ya Rahabu na matendo katika kujiokoa mwenyewe, familia yake, na wapelelezi wa Kiisraeli. Hili linakufundisha nini wewe kuhusu jinsi imani yako katika Kristo na matendo yako vinavyoweza kukushawishi wewe na wengine?

Rahabu akiangalia nje dirishani

Rahabu dirishani kwake. Kusubiri Ahadi, na Elspeth Young (utondoti)

Yoshua 3–4

Kwa imani katika Yesu Kristo, ninaweza kupata uzoefu wa “maajabu” ya Mungu.

Bwana alifanya maajabu miongoni mwa watu Wake alipowaongoza hadi kwenye nchi ya ahadi, na Yeye anaweza kufanya vivyo hivyo kwako. Haya ni baadhi ya maswali ya kukuongoza katika kujifunza kwako juu ya Yoshua 3–4:

  • Kwa nini unafikiri Waisraeli walihitaji kujitakasa wenyewe kabla ya kuvuka Mto Yordani? (ona Yoshua 3:5)

  • Kumbuka kwamba mto uligawanyika tu baada ya “nyayo za makuhani … zitakaposimama katika maji ya ukingoni” (Yoshua 3:13, 15). Je, kwa nini, hiyo ilikuwa yenye umuhimu?

  • Matukio mengine kadhaa muhimu yalitokea katika Mto Yordani—ona 2 Wafalme 2:6–15; 5:1–14; na Marko 1:9–11. Miunganiko gani unayoiona kati ya matukio haya?

  • Ni kwa jinsi gani Bwana ametenda “maajabu” maishani mwako? (Yoshua 3:5). Unawezaje kupata uzoefu—au kutambua—maajabu hayo mara kwa mara? (kwa mfano, ona Yoshua 3:17).

Yoshua 6–8

Utiifu hualika nguvu za Mungu katika maisha yangu.

Yoshia 6–8 inahusika na vita juu ya nchi ya Yeriko na Ai. Unapozisoma, sura hizi, fikiria jinsi unavyopambana na majaribu (kwa mfano, ona Yoshua 7:10–13). Unajifunza nini kuhusu jinsi Mungu anavyoweza kukusaidia na nini unahitaji kufanya ili kuzifikia nguvu Zake? Kwa mfano, ni nini kinakuvutia kuhusu maelekezo ya Bwana kwa ajili ya kuitwaa Yeriko? (ona Yoshua 6:1–5). Labda maelezo katika Yoshua 7 yatakushawishi wewe kuamua ikiwa “kuna kitu kilicholaaniwa” katika maisha yako unachohitaji kuondoa (Yoshua 7:13).

Yoshua 23–24

“Chagueni hivi leo mtakaye mtumikia.”

Mafundisho ya mwisho ya Yoshua kwa Waisraeli katika Yoshua 23–24 yanajumuisha maonyo muhimu, ushauri, na baraka zilizoahidiwa. Pengine ungeweza kutengeneza orodha ya kile unachokipata. Kwa kuzingatia kila kitu ambacho Waisraeli walikuwa wamepitia, kwa nini unafikiri Yoshua aliamua kuwaambia mambo haya wakati wa siku za mwisho za uhai wake? Unapata nini ambacho kinakutia msukumo wa “kuambatana na Bwana” (Yoshua 23:8).

Ona pia Dale G. Renlund, “Chagueni Hivi Leo,” Liahona, Nov. 2018, 104–6.

ikoni ya sehemu ya watoto

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Yoshua 1–4;6

“Uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa”

  • Hapa kuna njia moja ya kuwasaidia watoto wako “kuwa hodari na moyo wa ushujaa” (Yoshua 1:6) kupitia Yesu Kristo. Waalike watafute kirai ambacho kimerudiwa katika Yoshua 1:6, 9, na 18, na kukiandika au kukikariri. Wasaidie watoto wafikirie hali ambazo wanaweza kuhitaji ujumbe huu, kama vile Yoshua alivyofanya. Mngeweza pia kurejelea pamoja baadhi ya hadithi katika Yoshua 1–46 (ona pia “Yoshua Nabii” na “Rahabu na Wapelelezi” katika Hadithi za Agano la Kale, 85–91). Ni kwa jinsi gani watu katika hadithi hizi wanaonyesha ushujaa na nguvu katika Bwana?

    2:59

    Joshua the Prophet

    1:39

    Rahab and the Spies

Yoshua 1:8

Kujifunza maandiko huniletea baraka.

  • Kusoma Yoshua 1:8 kungeweza kuwapa msukumo watoto wako wa kusoma maandiko wao wenyewe. Wasaidie watafute maneno katika mstari huu ambayo yanawafundisha jinsi gani na kwa nini tunapaswa kusoma maandiko. Wangeweza kutafuta kitu hicho hicho katika 1 Nefi 15:23–24; 2 Nefi 31:20; 32:3; Yakobo 4:6; Helamani 3:29–30. Ungeweza pia kuwasaidia kutengeneza na kutekeleza mpango wa kusoma maandiko.

Yoshua 3–4

Ni lazima nibatizwe ili kuingia ufalme wa mbinguni.

  • Unaweza kutumia hadithi ya Waisraeli kuvuka Mto Yordani kama ishara ya ubatizo—kuacha maisha yetu ya zamani nyikani na kuanza upya katika uhusiano wa agano na Mungu. Kwa hiyo mnaposoma pamoja Yoshua 3–4 (au “Yoshua Nabii” katika Hadithi za Agano la Kale, 85–89), mngeweza pia kuangalia picha ya Yesu akibatizwa na kuelezea kwamba Yesu alibatizwa katika mto ule ule Waisraeli waliovuka. Kisha mngeweza kuimba wimbo kama vile “Baptism” (Kitabu chaNyimbo za Watoto, 100–101). Shiriki na kila mmoja jinsi kubatizwa ni kama kuanza maisha mapya katika ufalme wa Yesu Kristo.

    2:59

    Joshua the Prophet

picha yenye umbo inayomwonyesha Yesu akibatizwa na mvulana akibatizwa

Yoshua 24:15.

Ninaweza kuchagua kumtumikia Yesu Kristo.

  • Ungeweza kufanya nini ili kuwasaidia watoto wako wajifunze kuchagua kumfuata Yesu Kristo, kama Yoshua alivyowaalika Waisraeli kufanya? Unaweza kuwaalika ku:

    • Kariri kirai kifupi kutoka kwa Yoshua 24:15. Jaribu kuifanya iwe ya burudani kwa ajili ya watoto wako. Idadi ya maneno wanayokariri yanaweza kutegemea umri wao.

    • Tafuta hadithi kuhusu watu waliochagua kumtumikia Yesu Kristo. Wanaweza kuangalia katika jarida la Rafiki, Kitabu cha Sanaa ya Injili, au Hadithi za Agano la Kale na vitabu vingine vya hadithi za maandiko.

    • Igiza hali ambazo wanaweza kuchagua kumfuata na kumtumikia Mwokozi.

Tumia shughuli za aina mbali mbali. “Watoto wote ni tofauti, na wanapoendelea, mahitaji yao yatabadiklika. Kutofautisha mbinu zako za kufundisha kutakusaidia kukidhi mahitaji yao mbalimbali” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,31).

Kwa ajili ya zaidi, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .

kishikanafasi

Hatua za Kwanza za Imani katika Yordani, na Trent Gudmundsen

Ukurasa wa shughuli za Msingi: Ni lazima nibatizwe ili niingie katika ufalme wa mbinguni.