Njoo, Unifuate
Machi 23–29. “Nimekumbuka Agano Langu”: Kutoka 1–6


“Machi 23–29. ‘Nimekumbuka Agano Langu’: Kutoka 1–6,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)

“Machi 23–29. ‘Nimekumbuka Agano Langu’,” Njoo, Unifuate: 2026

Musa na kichaka kinachoteketea

Musa na Kichaka Kinachoteketea,na Harry Anderson

Kutoka 23–29: “Nimekumbuka Agano Langu”

Kutoka 1–6

Mwaliko wa kuishi Misri uliokoa familia ya Yakobo. Lakini baada ya mamia ya miaka, wazao wao walifanywa watumwa na kufanyiwa ukatili na farao mpya ambaye “hakumjua Yusufu” (Kutoka 1:8). Ingekuwa kawaida kwa Waisraeli kujiuliza kwa nini Mungu ameruhusu hili litokee kwao, watu Wake wa agano. Je, alilikumbuka agano alilofanya nao? Bado wao walikuwa watu Wake? Je, aliweza kuona ni kiasi gani walikuwa wakiteseka?

Yawezekana kuna wakati umejisikia kujiuliza maswali kama haya. Yawezekana ukajiuliza, “Je, Mungu anajua hiki ninachopitia? Je, anaweza kusikia kilio changu kwa ajili ya msaada?” Ukombozi wa Israeli kutoka Misri unajibu maswali ya aina hiyo kwa uwazi: Mungu hasahau watu Wake. Yeye anakumbuka maagano Yake na sisi na atayatimiza katika wakati Wake mwenyewe na katika njia Yake. “Nitawakomboeni kwa mkono ulionyooshwa,” Yeye anatamka. “Mimi ni Bwana Mungu wenu, ambaye niwatoa ninyi kutoka chini ya mizigo [yenu]” (Kutoka 6:6–7).

Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Kutoka, ona “Kutoka, kitabu cha” katika Kamusi ya Biblia.

ikoni ya kujifunza

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Kutoka 1–2

Mungu anaweza kufanya kazi kupitia mimi ili kutimiza makusudi Yake.

Je, ni kitu gani kinakuvutia kuhusu wanawake walioelezewa katika Kutoka 1–2? Ni kwa jinsi gani walisaidia kutimiza mpango wa Mungu kwa watu Wake? Juhudi zao zinakufundisha nini kuhusu huduma katika kazi ya Mungu?

Kutoka 1–3

Yesu Kristo ni Mkombozi wangu.

Kabla hujaanza kusoma Kutoka, unaweza kufikiria kuhusu ugumu wa maisha unaopitia—ni kitu gani unatumaini Bwana atakukomboe kwenye hiyo. Ni maneno na virai gani katika Kutoka 1–3 vinaonekana sawa na utumwa wa kiroho au vitu vingine tunavyokabiliana navyo leo? Tazama pia jinsi wana wa Israeli walivyotafuta ukombozi na jinsi Bwana alivyojibu (ona, kwa mfano, Kutoka 2:23–25; 3:7–8). Ni kwa jinsi gani Bwana “ameshuka chini ili kukukomboa” wewe?

Kote katika kitabu cha Kutoka, unaweza pia kuona baadhi ya mifanano kati ya Musa na Yesu Kristo (ona Kumbukumbu la Kumbukumbu la Torati 18:18–19; 1 Nefi 22:20–21). Kwa mfano, ni mifanano gani unayoiona kati ya Kutoka 1:22; 2:1–10 na Mathayo 2:13–16? Au kati ya Kutoka 24:18 na Mathayo 4:1–2? Unahisi ni nini Bwana anakutaka wewe kufahamu kumhusu Yeye Mwenyewe na Nguvu Zake.

Tafuta Ishara ambazo hushuhudia juu ya Yesu Kristo. “Unaweza … kupata maisha sambamba na Mwokozi katika maisha ya manabii na watu wengine wake kwa waume walio waaminifu katika maandiko. [Kufanya hivyo] hufunua kweli kuhusu Mwokozi katika sehemu ambazo vinginevyo ungeweza kuzipuuza” (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,7; ona pia Hosea 12:10).

wanawake wakivuta kikapu kukitoa mtoni

Imani katika Ukingo wa Maji, na Anne Marie Oborn

Kutoka 3:1–6

ikoni ya seminari
Ninaweza kuonesha staha kwa vitu na sehemu takatifu.

Je, unaweza kufikiria wakati kitu kilipokujaza kwa mshangao na kustaajabu? Je! ni kwa namna gani wewe ulijibu? Ni kwa jinsi gani ungeelezea hisia ulizohisi?

Ukiwa na hilo akilini, soma Kutoka 3:1–6. Ni kitu gani kinakuvutia wewe kuhusu uzoefu wa Musa wenye mwongozo wa kiungu? Musa alifanya nini ili kuonyesha staha kwa Mungu? Ni uhusiano gani unaouona kati ya matendo yake na staha kwa vitu vitakatifu?

Kusoma mistari hii kunaweza kukushawishi ufikirie kuhusu vitu vitakatifu na sehemu takatifu katika maisha yako. Kwa nini ni vitakatifu kwako? Ni kwa jinsi gani unavichukulia tofauti na vitu ambavyo ni vya kawaida? Ili kuongoza kutafakari kwako, ungeweza kurejelea sehemu yenye kichwa cha habari “Kukumbuka Ahadi” katika ujumbe wa Mzee David A. Bednar “Ahadi Kubwa Mno na za Thamani” (Liahona, Nov. 2017, 91–93). Unaweza pia kuimba au kusikiliza wimbo unaovutia sana, kama “I Stand All Amazed” (Nyimbo za Dini, na. 193) na kutafakari ni nini kuhusu injili ambacho kinakushangaza.

Bila shaka, hata wakati tumekuwa na uzoefu mzuri wa kiroho, kuna hatari ya kuwa wa kawaida sana kuhusu vitu vitakatifu. Ni kwa jinsi gani unaepuka hili? Hapa kuna jumbe mbili zinazozungumzia suala hili; chagua moja, na utafute kauli ambazo zinakusaidia: Ulisses Soares, “Kwa Mshangao wa Kristo na Injili Yake” (Liahona, Mei 2022, 115–17); Gérald Caussé, “Bado Ni Ajabu Kwako?” (Liahona, Mei 2015, 98–100).

Ona pia Mafundisho na Maagano 6:10–12, 63:64.

Kutoka 3–4

Mungu anatoa uwezo kwa watu anaowaita kutenda kazi Yake.

Leo tunamjua Musa kama nabii mkuu na kiongozi. Lakini Musa mwenyewe hakujiona hivyo wakati Bwana mara ya kwanza alipomwita. Unaposoma Kutoka 3–4, orodhesha wasiwasi wa Musa na jinsi Bwana alivyomjibu kwa kila moja. Je, unapata nini katika milango hii ambacho kinaweza kukupa mwongozo wa kiungu wakati unapojiona kuwa una mapungufu? Ni lini umeona Mungu akikuwezesha wewe au wengine kufanya kazi Yake?

Ona pia “Kanisa Linatupatia Fursa za Kusaidia katika Kazi ya Mungu” katika “Muundo wa Kanisa” katika Mada na Maswali, Maktaba ya Injili.

Kutoka 5-6

Madhumuni ya Bwana yatatimizwa katika wakati Wake mwenyewe.

Inaweza kukatisha tamaa wakati juhudi zetu za dhati za kufanya mema inapokuwa hazionekani kufanya kazi—tunapojaribu kufanya mapenzi ya Bwana lakini hatuoni matokeo tuliyotarajia. Kujifunza kuhusu uzoefu kama huo aliokuwa nao Musa, soma Kutoka 5:4–9, 20–23. Bwana alimsaidiaje Musa kushinda hisia zake za kukata tamaa? (Ona Kutoka 6:1–13). Je, ni kwa jinsi gani Bwana amekusaidia wewe kuvumilia katika kufanya mapenzi Yake?

Ona pia Jeffrey R. Holland, “Kumngoja Bwana,” Liahona, Nov. 2020, 115-17.

Kwa ajili ya zaidi, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .

ikoni ya 01 ya sehemu ya watoto

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Kwa sababu Jumapili hii ni Jumapili ya tano ya mwezi, walimu wa madarasa ya Watoto wanahimizwa kutumia shughuli za kujifunza katika “Kiambatisho B: Kuwaandaa Watoto kwa Ajili ya Maisha Yote juu ya njia ya Agano la Mungu.”

Kutoka 1–2

Mungu anaweza kufanya kazi kupitia mimi ili kutimiza makusudi Yake.

  • Musa alikuwa na jukumu kubwa katika kuikomboa Israeli kutoka utumwani. Lakini hasingeweza kutimiza hii kama mama yake, dada yake, binti wa Farao, na wanawake wengine waaminifu wasingemlinda na kumtunza. Wasaidie watoto wako wajifunze kuhusu wanawake hawa katika Kutoka 1:15–20; Kutoka 2:2–10 (ona pia Hesabu 26:59); na Kutoka 2:16–21. Ungeweza pia kutumia ukurasa wa shughuli ya wiki hii na “Mtoto Musa” (katika Hadithi za Agano la Kale, 61–63) kusimulia hadithi zao. Je, ni kwa jinsi gani wanawake hawa walisaidia kutimiza mpango wa Mungu? Zungumza na kila mmoja kuhusu watu wengine unaowaenzi ambao wanasaidia katika kazi ya Mungu, ikijumuisha kwa njia ndogo na rahisi. Ni kwa jinsi gani tunaweza kufuata mfano wao?

    1:36

    Baby Moses

Kutoka 3:1–5

Ninaweza kutendea sehemu takatifu kwa staha.

  • Baada ya kusoma Kutoka 3:1–5 pamoja, waombe watoto wako wafupishe mistari hii kwa maneno yao wenyewe (ona pia “Musa Nabii” katika Hadithi za Agano la Kale, 64–66). Ni kwa jinsi gani Musa alionyesha staha katika uwepo wa Bwana? Ni kwa jinsi gani Bwana anatutaka kuonesha staha? Unaweza pia kuwaomba watoto wako wakusaidie kupata (au kuchora) picha za mahali patakatifu au shughuli ambapo tunapaswa kuwa wenye staha. Tunaweza kufanya nini ili kufanya nyumba zetu kuwa sehemu takatifu

    1:26

    Moses the Prophet

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu staha, kama vile “Reverence Is Love” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,31). Unapofanya hivyo, watoto wako wangeweza kupata maneno au virai ambavyo vinaelezea kile inachomaanisha kuwa na staha. Kama tungekuwa tunamleta rafiki kanisani kwa mara ya kwanza, tungemwelezea maana ya kuwa na staha ni nini?

Musa na Haruni wanazungumza na watu

Musa na Haruni Wanazungumza na Watu, na James J. Tissot

Kutoka 3–4

Wakati Bwana anaponiomba nifanye kitu fulani, Yeye atanisaidia kufanya hivyo.

  • Tumia simulizi kwenye Kutoka 3; 4:1–17, acha watoto wako wachukue zamu kujifanya kuwa ni Musa. Inaweza kuwa ya kufurahisha kujumuisha vitu au vitu rahisi, kama vile tochi na mmea kuwakilisha kichaka kinachoteketea. Wasaidie watoto wako wagundue jinsi Musa alivyohisi kuhusu kazi ambayo Bwana alimpa (ona Kutoka 3:11; 4:1, 10). Pengine mngeweza kuelezeana ninyi kwa ninyi wakati mlipokuwa na hisia sawa na hizo. Je, ni ushauri gani tungeweza kushiriki na Musa ili kumsaidia? Soma kuhusu jinsi Bwana alivyomtia moyo Musa katika ( Kutoka 3:12; 4:2–9, 11–12 Waambie watoto jinsi Mwokozi alivyokusaidia kutimiza wito, kufuata msukumo, au kufanya kitu kingine ambacho kilikuwa kigumu kwako.

Kwa ajili ya zaidi, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki

Mama wa Musa

Mama wa Musa, na Simeon Solomon

Ukurasa wa shughuli:za Msingiss: Ninaweza kusamehe