Njoo, Unifuate
Machi 16–22. “Mungu Aliyakusudia Kuwa Mema”: Mwanzo 42–50


“Machi 16–22. ‘Mungu Aliyakusudia Kuwa Mema’: Mwanzo 42–50,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)

“Machi 16–22. ‘Mungu Aliyakusudia Kuwa Mema’,” Njoo, Unifuate: 2026

Yusufu akiwasamehe kaka zake

Msamaha, na Megan Rieker

Mwanzo 16–22: “Mungu Aliyakusudia Kuwa Mema”

Mwanzo 42–50

Ilikuwa takribani miaka 22 tangu kaka zake Yusufu wamuuze utumwani. Joseph aliteseka majaribu mengi, ikijumuisha shutuma za uongo na kifungo. Wakati alipowaona kaka zake tena, Yusufu alikuwa gavana wa Misri yote, wa pili tu kutoka kwa Farao. Angeweza kwa urahisi kabisa kulipa kisasi kwa kaka zake, na ukizingatia kile wao walichomtendea Yusufu, hilo lingeeleweka. Na bado Yusufu aliwasamehe wao. Siyo hilo tu, lakini yeye aliwasaidia kuona kusudi takatifu katika mateso yake. “Mungu aliyakusudia kuwa mema” (Mwanzo 50:20), yeye aliwaambia, kwa sababu hilo lilimweka yeye katika nafasi ya kuokoa “kaya yote ya baba yake” (Mwanzo 47:12) kutokana na baa la njaa.

Katika njia nyingi, Yusufu alikuwa kama Yesu Kristo. Ingawa dhambi zetu zilimsababishia Yesu mateso makuu, Yeyeanatupatia msamaha, akitukomboa sisi sote kutokana na maangamizi makubwa kuliko njaa. Iwe sisi tunahitaji kupokea msamaha au kutoa—mahali fulani sisi sote tunahitaji kufanya vyote—mfano wa Yusufu unatuelekeza sisi kwa Mwokozi, aliye chanzo cha kweli cha uponyaji na usuluhishi.

ikoni ya kujifunza

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Mwanzo 45:5–7; 47:12

“Mungu alinipeleka mbele yenu ili niwaokoe ninyi.”

Je, umegundua mifanano yoyote kati ya maisha ya Yusufu na misheni ya ya Yesu Kristo ya kulipia dhambi? Ili kuona baadhi ya mifanano hii, jaribu kulinganisha:

  • Mwanzo 37:3 na Mathayo 3:17.

  • Mwanzo 37:26–28 pamoja na Mathayo 26:14–16.

  • Mwanzo 45:5–7 na Luka 4:18.

  • Mwanzo 47:12 pamoja na Yohana 6:35.

Ni misukumo gani unaipata kuhusu Mwokozi unaposoma vifungu hivi?

Mwanzo 45; 50:15–21

ikoni ya seminari
Msamaha huleta uponyaji.

Kusoma kuhusu Yusufu kuwasamehe kaka zake kwa mambo ya mabayawaliyofanya inaweza kukushawishi wewe kufikiria kuhusu mtu unayehangaika kumsamehe. Maswali yafuatayo yanaweza kusaidia unapojitahidi kutumia kanuni hii:

  • Kwa nini pengine ingekuwa vigumu kwa Yusufu kuwasamehe kaka zake? (kurejelea kile walichomfanyia, ona Mwanzo 37). Ni uzoefu au mitazamo gani inawezekana ilimpa Yusufu nguvu ya kuwasamehe? (Ona, kwa mfano, Mwanzo 45:1–15 au 50:15–21)

  • Ni baraka gani zilikuja kutokana na msamaha wa Yusufu kwa kaka zake? Kwa mfano, linganisha mahusiano katika familia ya Yakobo mwanzoni mwa hadithi (ona, kwa mfano, Mwanzo 37:3–11) na mahusiano hapo mwishoni (ona Mwanzo 45:9–15; 50:15–21). Ni kwa jinsi gani mambo yangeweza kuwa tofauti kama Yusufu asingekuwa radhi kusamehe?

  • Fikiria kuandika jina la mtu ambaye anaweza kuhitaji msamaha wako—kama wameomba msamaha au la. Unaweza kufanya nini ili kualika nguvu ya uponyaji ya Mwokozi katika hali hiyo? Kama kusamehe kunaonekana kuwa vigumu sana, fikiria kurejelea ushauri wa Mzee Gerrit W. Gong katika aya sita za mwisho za ujumbe wake “Furaha na Milele” (Liahona, Nov. 2022, 85). Unapata nini ambacho kinakupa tumaini kwamba unaweza kusamehe?

Ona pia Mafundisho na Maagano 64:9–11; “Forgiveness: My Burden Was Made Light” (video), Maktaba ya Injili.

8:24

Forgiveness: My Burden Was Made Light

Mwanzo 49

Yakobo aliipa familia yake baraka za kinabii.

Baraka za Yakobo kwa uzao wake zina picha dhahiri, lakini si rahisi kuelewa. Tunashukuru, injili ya urejesho inatupa msaada fulani. Unaposoma baraka za Yusufu katika Mwanzo 49:22–26, soma mistari ifuatayo pia, na uone ni umaizi gani inatoa: 1 Nefi 15:12; 2 Nefi 3:4–5; Yakobo 2:25; Mafundisho na Maagano 50:44.

Unaposoma kuhusu baraka za Yuda katika Mwanzo 49:8–12, kumbuka kwamba Yesu Kristo alikuwa wa uzao wa Yuda. Unapata nini katika mistari hii ambacho kinakukumbusha juu ya Mwokozi? (ona pia Ufunuo 5:5–6, 9; 1 Nefi 15:14–15; Mafundisho na Maagano 45:59; 133:46–50).

Kusoma baraka hizi kunaweza kukupa msukumo wa kurejelea baraka yako ya kipatriaki—au, kama huna, fikiria kupokea moja. Ni maneno na virai gani katika baraka yako vinageuza mawazo yako kwa Yesu Kristo?

Ona pia Randall K. Bennett, “Baraka Yako ya Kipatriaki—Mwongozo wenye uvuvio kutoka kwa Baba wa Mbinguni,” Liahona, Mei 2023, 42–44.

Mwanzo 50:19–21

Mungu anaweza kunisaidia kupata maana katika majaribu yangu.

Ingawa yawezekana haikuwa wazi alipokuwa akiyapitia, Yusufu hatimaye aliweza kuangalia nyuma kwenye shida zake Misri na kuona kwamba “Mungu aliyakusudia kuwa mema” (Mwanzo 50:20). Kama ungeweza kumtembelea Yusufu alipokuwa shimoni au gerezani, ni kwa jinsi gani ungeweza kumfariji? Ni kwa jinsi gani Mwanzo 50:19–21 inaweza kukusaidia katika nyakati zako za majaribu?

Ona pia Mafundisho na Maagano 122; “Msingi Imara,” Nyimbo za Dini, na. 36.

Yusufu wa Misri akiwa na ono la Joseph Smith akipokea mabamba ya dhahabu kutoka kwa malaika Moroni

Joseph Smith miongoni mwa Manabii, na Paul Mann (utondoti)

Mwanzo 50:24–25

“Mwonaji Bwana Mungu wangu atamwinua.”

Unaposoma Mwanzo 50:24–25 na Tafsiri ya Joseph Smith, Mwanzo 50:24–38 (katika kiambatisho cha Biblia), tafakari kwa nini ingekuwa muhimu kwa Yusufu kujua kuhusu Musa na Joseph Smith karne nyingi kabla. Ni kwa jinsi gani Joseph Smith alitimiza unabii wa Yusufu kumhusu yeye? (ona Mafundisho na Maagano 1:17–23; 20:7–12; 39:11; 135:3).

Kwa ajili ya zaidi, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .

ikoni ya 01 ya sehemu ya watoto

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Mwanzo 42:21-44; 45:4–15

Ninaweza kuonyesha upendo na msamaha kwa familia yangu

  • Inaweza kuwa ya kufurahisha kwa watoto wako kuigiza hadithi ya Yusufu kuungana tena na familia yake (ona Mwanzo 42–44). Au wanaweza kutumia “Yusufu na Baa la Njaa” (katika Hadithi za Agano la Kale, 57–60) au picha katika muhtasari huu kufundishana hadithi hii. Haya ni baadhi ya maswali ambayo yangeweza kuwasaidia watoto wako wajifunze kutoka kwenye hadithi hii:

    • Yusufu alifanya nini kuonyesha upendo kwa familia yake? (ona Mwanzo 45:4–15).

    • Kwa nini unahisi Yusufu aliwasamehe kaka zake?

    • Unafikiri kaka zake Yusufu walihisi vipi walipogundua Yusufu alikuwa amewasamehe? Nani katika maisha yako anahitaji kusamehewa? Ni kwa jinsi gani unaweza kuonyesha upendo na msamaha?

    2:26

    Joseph and the Famine

Unapojiandaa kufundisha, uliza, “Watoto wangu watafanya nini ili kujifunza?” Kwa mfano, katika shughuli hii watoto wako wanaigiza au wanasimulia tena hadithi hii. Kufanya hili kutawasaidia kukumbuka yote yaliyotokea na kanuni za injili zilizomo katika hadithi.

  • Wewe au watoto wako mnaweza kutaka kushiriki uzoefu wakati walipomsamehe mtu au wakati mtu fulani alipowasamehe. Kisha mngeweza kuimba wimbo kama vile “Love One Another” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 136) au “Help Me, Dear Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 99).

Mwanzo 48:8–9

Bwana hunisaidia kupitia baraka za ukuhani.

  • Wewe na watoto wako mngeweza kuangalia picha ya Yakobo akiwabariki wanawe mwishoni mwa muhtasari huu na kujadili kile kinachotokea (ona Mwanzo 48:8–9). Kama itahitajika, elezea kwamba Yakobo baba yake Yusufu, alitaka kutoa baraka za ukuhani kwa familia yake. Pengine mngeweza kushiriki wenyewe uzoefu wowote ambao mmekuwa nao katika kupokea msaada kutoka kwa Mungu kupitia baraka ya ukuhani. Ni zipi baadhi ya sababu ambazo tunaweza kuomba baraka ya ukuhani?

msichana mdogo akipokea baraka

Mwanzo 45:5–11

Baba wa Mbinguni alimtuma Yesu Kristo kuniokoa.

  • Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto wako wamwone Mwokozi katika hadithi ya Yusufu akiokoa familia yake kutokana na baa la njaa? Fikiria kutengeneza chati yenye safu mbili zilizoandikwa Yusufu na Yesu Kristo. Saidia watoto kutafuta jozi zifuatazo za maandiko na uandike kwenye ubao vitu ambavyo Yusufu na Yesu wamefanana: Mwanzo 37:3 na Mathayo 3:17; Mwanzo 37:26–28 na Mathayo 26:14–16; Mwanzo 45:5–7 na Luka 4:18; and Mwanzo 47:12 na Yohana 6:35.

  • Waulize watoto inamaanisha nini kukomboa au kumuokoa mtu. Ikiwa yeyote kati yao amepata uzoefu wa kukombolewa au kuokolewa kutoka kwenye hatari, waalike kushiriki. Ni kwa jinsi gani Yusufu aliwaokoa kaka zake? (ona Mwanzo 42:1–3; 45:5–7). Kisha mngeweza kutazama picha ya Mwokozi pamoja na waombe watoto wako wazungumze kuhusu jinsi Yesu anavyotuokoa sisi.

Kwa ajili ya zaidi, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .

Israeli akitoa baraka ya ukuhani kwa mwanawe

Yakobo Akimbariki Yusufu (Yakobo Akibariki Wanawe), na Harry Anderson

ukurasa wa shughuli ya Msingi: Ninaweza kusamehe