“Mawazo ya Kuweka Akilini: Nyumba ya Israeli,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)
“Nyumba ya Israeli,” Njoo, Unifuate: 2026
Mawazo ya Kuweka Akilini
Nyumba ya Israeli
Mahali fulani nyikani mashariki mwa Kanaani, Yakobo akiwa mwenye wasiwasi alisubiria kukutana na kaka pacha wake, Esau. Mara ya mwisho Yakobo kumuona Esau, ilikuwa takribani miaka 20 iliyopita, Esau alipotaka kumuua. Yakobo alitumia usiku mzima akipigana mieleka, akitafuta baraka kutoka kwa Mungu. Kama matokeo ya imani ya Yakobo, ung’ang’anizi na ushupavu wake, Mungu alijibu maombi yake. Usiku ule jina la Yakobo lilibadilishwa kuwa Israeli, jina ambalo linamaanisha, miongoni mwa mambo mengine, “alishindana na Mungu” (Mwanzo 32:28, tanbihib).
Karibu na mto Yaboki, Yakobo alipokea jina la Israeli.
Hii ni mara ya kwanza jina Israeli linaonekana katika Biblia, na ni jina ambalo huvumilia kitabu chote hadi mwisho wa historia.yote. Jina ambalo punde likaja kuitwa kwa zaidi ya mtu mmoja. Israeli alikuwa na wana 12, na wazao wao kwa ujumla walijulikana kama “nyumba ya Israeli,” “makabila ya Israeli,” “watoto wa Israeli,” au “Waisraeli.”
Kote katika historia, watoto wa Israeli waliweka umuhimu mkubwa kwa vizazi vyao kutoka mojawapo ya makabila kumi na mawili ya Israeli. Nasaba yao ilikuwa sehemu muhimu ya utambulisho wao wa agano. Mtume Paulo alitangaza kwamba yeye alikuwa “wa kabila ya Benyamini” (Warumi 11:1). Sababu moja ambayo Lehi aliwatuma wanawe Yerusalemu kuchukua mabamba ya shaba, ilikuwa kwamba mabamba hayo yalikuwa na “historia ya nasaba ya mababu zake” (1 Nefi 5:14; Lehi aligundua kwamba yeye alikuwa wa uzao wa Yusufu, na uelewa wa uzao wake juu ya muungano wao kwenye nyumba ya Israeli ulithibitika kuwa wa muhimu kwao katika miaka iliyofuata.
Katika Kanisa leo, unaweza ukasikia kuhusu Israeli katika maongezi kama “kukusanywa kwa Israeli.” Tunaimba kuhusu “Mkombozi wa Israel,” “Tumaini la Israel,” na “Wazee wa Israeli.” Katika masuala haya, hatuongelei au kuimba tu kuhusu ufalme wa kale wa Israeli au taifa la sasa liitwalo Israeli. Bali, tunatumia kwa watu ambao wamekuwa wamekusanywa kutoka mataifa ya ulimwengu kuja katika Kanisa la Yesu Kristo. Tunatumia kwa watu ambao wameshindana na Mungu, ambao kwa dhati wanatafuta baraka Zake, na ambao, kupitia ubatizo, wamekuwa watu Wake wa agano. Katika maneno ya Rais Russell M. Nelson, kuwa wa Israeli inamaanisha “kuacha Mungu ashinde katika maisha yetu, … kuacha Mungu awe ushawishi wenye nguvu zaidi katika maisha yetu.”
Baraka zako za patriaki zinatamka muunganiko wako na moja ya makabila ya nyumba ya Israeli. Hiyo ni zaidi ya kipande cha kufurahisha cha historia ya familia. Pia inahusiana na wakati wako wa sasa na siku zijazo. Kuwa sehemu ya nyumba ya Israeli inamaanisha una uhusiano wa kiagano na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Inamaanisha kwamba wewe, kama Ibrahimu, unakusudiwa “kuwa baraka” kwa watoto wa Mungu (Mwanzo 12:2; Ibrahimu 2:9–11). Ina maana, katika maneno ya Petro, kwamba “ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu; mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu” (1 Peter 2:9). Inamaanisha kwamba wewe “mwache Mungu ashinde”—kwamba wewe ni mmoja ambaye “umeacha Mungu shinde” unapoheshimu maagano yako na Yeye.
Mti wa Familia ya Yakobo (Israeli), na Brent Evans