“Agosti 31–Septemba 6. ‘Kila Mwenye Pumzi na Amsifu Bwana’”: Zaburi 102–103; 110; 116–119; 127–128; 135–139; 146–150,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani 2026 (2026)
“Agosti 31–Septemba 6. ‘Kila Mwenye Pumzi Na Amsifu Bwana,’” Njoo, Unifuate: Agano la Kale 2026
Kurudi kwa Staha, na Kelsy na Jesse Lightweave
Agosti 31–Septemba 6: “Kila Mwenye Pumzi na Amsifu Bwana.”
Zaburi 102–103; 110; 116–119; 127–128; 135–139; 146–150
Jina la kiutamaduni wa Kiyahudi kwa kitabu cha Zaburi ni Tehillim, neno la Kiebrania linalomaanisha “sifa.” Inahusiana na mshangao haleluya (ikimaanisha “msifu Yehova” au “msifu Bwana”). Kama ungechagua neno moja kujumuisha ujumbe mkuu wa Zaburi hizi, sifa lingekua chaguo zuri. Baadhi ya zaburi zinajumuisha mwaliko wa moja kwa moja wa “kumsifu Bwana” (ona hasa Zaburi 146–50), na zote zinaweza kutoa msukumo wa kuabudu na kusifu. Zaburi inatualika sisi kukiri nguvu za Bwana, huruma Yake, na mambo makubwa ambayo Yeye ameyafanya. Kamwe hatuwezi kumlipa Yeye katika mojawapo ya haya, ila tunaweza kumsifu Yeye. Kusifu huku kungeweza kuchukua mitindo tofauti kwa watu tofauti—kungeweza kujumuisha kuimba, kusali, au kutoa ushuhuda. Mara nyingi hukuongoza katika ahadi za kina kwa Bwana na kwenye kufuata mafundisho Yake. Vyo vyote vile, “kumsifu Bwana” inachomaanisha katika maisha yako, unaweza kupata mwongozo kufanya hivyo wakati unaposoma na kutafakari Zaburi.
Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani
Zaburi 102–3; 116
Bwana anaweza kunifariji katika mateso yangu.
Angalia jinsi Zaburi 102:1–11 inavyoelezea hisia za wasiwasi na kutengwa ambazo mara nyingi huja wakati wa changamoto. Pengine wewe au wengine unao wajua mmepata uzoefu wa hisia kama hizo. Unaposoma Zaburi 102:12–28; 103; 116, tafuta virai ambavyo vinakupa kujiamini kwamba unaweza “kuliita jina la Bwana” katika majaribu yako (Zaburi 116:13). Ungeweza kutaka kuwekea alama, kukariri, au kushiriki na wengine virai vinavyokupa tumaini katika Yeye.
Ona pia Isaya 25:8; Waebrania 2:17–18; Alma 7:11–13; Camille N. Johnson, “Kristo ni Faraja,” Liahona, Mei 2023, 81–83; “Iwapi Amani?” Nyimbo za Dini, na. 62).
Carl Heinrich Bloch (1834-1890), Kristo Akiwaponya Wagonjwa huko Bethsaida, 1883, mafuta kwenye katani, inchi 100 ¾ x 125 ½. Makumbusho ya Sanaa ya Chuo Kikuu cha Brigham Young, ilinunuliwa kwa fedha kutoka kwa Jack R. na Mary Lois Wheatley, 2001.
Zaburi 110; 118
Yesu Kristo alitimiza unabii kutoka katika Zaburi hizi.
Zaburi imejumuisha vifungu vinavyoelekeza kwenye maisha na huduma ya Yesu Kristo. Hapa kuna mifano michache:
-
Zaburi 110:1–4 (ona Mathayo 22:41–45; Waebrania 5:4–10; 6:20)
-
Zaburi 118:22 (ona Mathayo 21:42; Matendo ya Mitume 4:10–11; 1 Petro 2:7)
-
Zaburi 118:25–26 (ona Mathayo 21:9)
Mistari hii inakufundisha nini kuhusu Yesu Kristo? Kwa nini ni muhimu kujua hili kumhusu Yeye?
Zaburi 119
Neno la Mungu daima litaniweka katika njia Yake.
Zaburi 119 imejumuisha virai vingi ambavyo hulinganisha maisha yetu na safari ya kurudi kwa Baba yetu wa Mbinguni. Unaposoma, angalia maneno kama “tembea”, “njia,” “namna,” “nyayo,” na “tangatanga.” Tafakari safari ya maisha yako—pale umekuwa, pale ulipo sasa, na pale unapoelekea. Je, unajifunza nini kutoka kwenye zaburi hii kuhusu safari yako ya kurudi nyumbani? Umejifunza nini kwa kutazama njia za wengine? Kulingana na zaburi hii, Mungu ametoa nini kukusaidia wewe kubaki katika njia Yake?
Fikiria kuhusu wakati ambapo kufuata njia au ramani kulikusaidia kusafiri mahali fulani kwa mafanikio. Uzoefu huo unakufundisha nini kuhusu kufuata njia ya Mungu?
Katika maandiko mengine mengi, Bwana na manabii Wake wanasema juu ya njia. Hapa chini kuna baadhi ya mifano. Fikiria kupekua mistari hii na kuandika au kushiriki na wengine kile unachojifunza.
|
Andiko |
Kile ninachojifunza kuhusu njia ya Mungu |
|---|---|
Andiko Mithali 4:11–19 | |
Andiko Mathayo 7:13–14 | |
Andiko | |
Andiko | |
Andiko | |
Andiko |
Ni kwa jinsi gani kweli hizi zinakusaidia kubaki kwenye njia ya Mungu?
Ni umaizi gani wa ziada unaweza kujifunza kutokana na ushauri ufuatao kutoka kwa Rais Russell M. Nelson?
“Ikiwa safari yetu maishani inatakiwa kuwa yenye mafanikio, tunahitaji kufuata maelekezo ya kiungu. Bwana alisema, ‘Nitegemeeni katika kila wazo; msitie shaka, msiogope’ [Mafundisho na Maagano 6:36] Na mtunga Zaburi aliandika, ‘Neno lako ni taa ya miguu yangu na mwanga wa njia yangu’ [Zaburi 119:105]. …
“Katika safari yako ya maisha, unakutana na vikwazo vingi na kufanya baadhi ya makosa. Mwongozo wa kimaandiko hukusaidia kutambua makosa na kufanya masahihisho muhimu. Unaacha kwenda katika mwelekeo mbaya. Unajifunza kwa uangalifu ramani ya barabara ya kimaandiko. Halafu unaendelea na toba na kurejesha vinavyohitajika kurejeshwa ili kuingia kwenye ‘njia nyembamba iliyosonga inayoongoza kwenye uzima wa milele’ [2 Nefi 31:18]” (“Living by Scriptural Guidance,” Ensign, Nov. 2000, 17).
Ona pia Dieter F. Uchtdorf, “Mwana Mpotevu na Barabara Inayoongoza Nyumbani,” Liahona, Nov. 2023, 86–88.
Zaburi 134–36
Bwana ni mwenye nguvu sana kuliko sanamu yoyote.
Angalia kwa nini kulingana na Zaburi 135:15–18, ni ujinga kuamini katika miungu ya uongo. Unaweza kujaribiwa kuamini nini ambacho ni sawa na sanamu? Unaweza kutengeneza orodha ya mambo ambayo Bwana anaweza kufanya, kama watunga zaburi walivyofanya katika Zaburi 134–36. Je, ni mambo gani yenye nguvu Yeye aliyokutendea?
Zaburi 139
Bwana anaujua moyo wangu.
Unapata nini katika Zaburi 139 ambacho kinakusaidia uelewe kwamba Bwana anakujua wewe—mawazo na matendo yako, nguvu na udhaifu? Ni kwa jinsi gani ukweli huu hushawishi maisha yako na chaguzi zako?
Zaburi 146–50
“Msifuni Bwana.”
Unaposoma zaburi hizi za mwisho za sifa, fikiria kuhusu sababu ulizo nazo za kumsifu Bwana. Kwa nini ni muhimu kumsifu Yeye? Ni zipi baadhi ya njia unazoweza kumsifu Yeye?
Kwa ziada, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .
Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto
Zaburi 102:1–2
Bwana hunifariji na kunipa tumaini.
-
Wewe au mmoja wa watoto wako mngeweza kusoma Zaburi 102:1–2, mkitafuta jinsi Bwana anavyotusaidia wakati wa magumu yetu. Je, ni kwa jinsi gani sisi tunaweza kupata msaada Wake? Mngeweza pia kushiriki mmoja na mwingine nyakati mlipohitaji msaada na kuhisi kwamba Mungu alisikia sala zenu.
Zaburi 119:105
Neno la Mungu ni kama nuru.
-
Watoto wako wanaweza kuwa na burudani kuzungumza kuhusu jinsi inavyoonekana kuwa gizani. Au wangeweza kujadili mambo ambayo ni magumu kufanya gizani? Ungeweza kuwaalika kufanya kitu fulani kama macho yao wakiwa wamefumba, kama vile kuchora picha. Tunajifunza nini kutoka katika Zaburi 119:105 kuhusu nuru na neno la Mungu?
-
Tafuta kitu ambacho Baba wa Mbinguni ametupatia ili kutusaidia kukaa katika njia Yake katika mistari ifuatayo: Zaburi 119:47–48; 119:105; 1 Nefi 11:25; 2 Nefi 31:20. Tunaweza kufanya nini ili kukaa katika njia ya Mungu?
-
Watoto wako wangeweza kufurahia kuangalia picha za vitu vilivyotajwa katika Zaburi 119:105. Wanaweza kuweka picha kwa mpangilio wakati wanaposoma mstari huo. Mngeweza pia kuimba wimbo unaohusiana nao kwa pamoja, kama vile “Teach Me to Walk in the Light” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 177) au “I Will Walk with Jesus” (Gospel Library).
Zaburi 139:1–3, 23–24
Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wananijua na wananipenda.
-
Fikiria kutengeneza orodha fupi za vitu unavyovijua kuhusu kila mmoja wa watoto wako. Unapoisoma orodha ya kila mmoja kwa wakati, waombe watoto wabashiri ni nani unamuongelea. Kisha, baada ya kusoma Zaburi 139:1–3 pamoja, ungeweza kuorodhesha vitu ambavyo Baba wa Mbinguni na Yesu wanajua kutuhusu sisi.
-
Andika maneno ya Zaburi 139:23–24 kwenye kipande cha karatasi au ubaoni. Waalike watoto wako wapigie mstari maneno ambayo yanaelezea mambo ambayo Mungu anaweza kutufanyia. Je, ni kwa nini tungependa Mungu afanye mambo haya?
Zaburi 146:1, 5–9
Ninaweza kumsifu Bwana.
-
Pengine watoto wako wangeweza kushiriki uzoefu wa wakati mtu fulani alipowasifu au kuwaambia walifanya kazi nzuri. Shiriki baadhi ya mambo mazuri kutoka Zaburi 146:6–9 ambayo Bwana ameyafanya (wasaidie watoto wako waelewe maneno yasiyo ya kawaida). Waalike watoto wako wazungumze kuhusu mambo mengine anayofanya kwa ajili yetu. Ni kwa jinsi gani tunaweza kumsifu Yeye kwa vitu hivyo?
Jifunze nyumbani; shiriki na wengine. Rais Russell M. Nelson amefundisha kwamba nyumbani panapaswa kuwa “kitovu cha kujifunza injili” (“Kuwa Mtakatifu wa Siku za Mwisho wa Mfano,” Liahona, Nov. 2018, 113). Unaweza kufanya nini wiki hii ili kuongeza kina cha kujifunza kwako Zaburi kwako binafsi au kama familia? Baada ya kujifunza kwako, fikiria kushiriki na wengine kile ulichojifunza na kuhisi. Unaweza kufanya hivi katika mazungumzo, kupitia maandishi au mitandao ya kijamii, au kanisani.
Kwa ziada, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .