Njoo, Unifuate
Septemba 7–13. “Naye Atayanyoosha Mapito Yako”: Mithali 1–4; 15–16; 22; 31; Mhubiri 1–3; 11–12


“Septemba 7–13. ‘Naye Atayanyoosha Mapito Yako’: Mithali 1–4; 15–16; 22; 31; Mhubiri 1–3; 11–12,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)

“Septemba 7–13. ‘Naye Atayanyoosha Mapito Yako,’” Njoo, Unifuate: Agano la Kale 2026

Yesu pamoja na watoto

Yesu pamoja na Watoto, na Dilleen Marsh

Septemba 7–13: “Naye Atayanyoosha Mapito Yako”

Mithali 1–4; 15–16; 22; 31; Mhubiri 1–3; 11–12

Ungeweza kufikiria kitabu cha Mithali kama mkusanyiko wa ushauri wa hekima kutoka kwa wazazi wenye upendo (ona Mithali 1:8). Ujumbe wake mkuu ni kwamba ikiwa unatafuta hekima—hususani hekima ya Mungu—maisha yatakwenda vizuri. Lakini Mithali inafuatwa na kitabu cha Mhubiri, ambacho kinaonekana kusema, “Sio rahisi hivyo.” Mhubiri aliyenukuliwa katika Kitabu cha Mhubiri aliona kwamba “Akatia moyo [wake] ili kuijua hekima” lakini bado alipata “kujilisha upepo” na “wingi wa huzuni” (Mhubiri 1:17–18). Kwa njia nyingi tofauti, kitabu kinauliza, “Je, kunaweza kuwa na maana halisi katika ulimwengu ambao kila kitu kinaonekana kuwa bure, cha muda mfupi, na hakina uhakika?”

Na bado, wakati vitabu hivi viwili vinaangalia maisha kwa mitazamo tofauti, vinafundisha kweli zinazofanana. Mhubiri anatangaza: “Yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu” (Mhubiri 12:13). Hii ni kanuni ile ile inayopatikana kote katika Mithali: “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote” (Mithali 3:5; ona pia mstari wa 7). Maisha daima ni mazuri—kama siyo daima kamilifu—wakati tunapomwamini na kumfuata Bwana Yesu Kristo.

Kwa ajili ya muhtasari wa vitabu hivi, ona “Mithali, kitabu cha” na “Mhubiri” katika Kamusi ya Biblia.

ikoni ya kujifunza

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Mithali 1–4; 15– 31; Mhubiri 1–3; 11–12

“Tega sikio lako kusikia hekima.”

Vitabu vya Mithali na Mhubiri vimejaa umaizi kuhusu hekima. Zingatia kuwekea alama neno “hekima” na maneno yanayohusiana, kama “maarifa” na “uelewa” unapoyapata katika Methal 1–4; 15–16; Mhubiri 1–3; 11–12. Ni kwa jinsi gani sura hizi zinaleta matokeo ya jinsi unavyofikiri kuhusu hekima? Kutokana na unachokipata, ni kwa jinsi gani ungeelezea hekima ambayo “Bwana hutoa”? (Mithali 2:6). Ni baraka zipi huja kutokana na hekima ya Mungu?

Ona pia Mathayo 7:24–27; 25:1–13.

Wasaidie wengine kushiriki kile wanachojifunza. “Wape wanafunzi fursa za kushiriki wao kwa wao kile wanachojifunza kuhusu Mwokozi na injili Yake. Kufanya hivikutawasaidia wao wafanye kweli wanazofundishwa ziwe zinawahusu na kuweza kuzielezea. Kunaweza pia kuwasaidia wapate kujiamini katika uwezo wao wa kushiriki kweli katika mazingira mengine” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi26). Kwa mfano, unaweza kuwaalika wanafunzi kuandika baadhi ya marejeleo kutoka kwa Mithali au Mhubiri ambapo walipata umaizi kuhusu hekima ya Mungu. Kisha waalike wazungumze kuhusu kile walichojifunza.

Mithali 1:7; 2:5; 3:7; 15:33; 16:6; 31:30; Mhubiri 12:13

“Usiwe mwenye hekima machoni pako; mche Bwana.”

Mada nyingine inayopatikana kote katika Mithali na Mhubiri ni “kumcha Bwana.” Angalia kirai hiki unaposoma. Unafikiri inamaanisha nini kumcha Bwana? Tafuta umaizi katika ujumbe wa Mzee David A. Bednar “Therefore They Hushed Their Fears” (Liahona, Mei 2015, 46–49). Je, Ni kwa jinsi gani kumcha Bwana ni tofauti na aina nyingine za hofu?

Ona pia Mithali 8:13.

Methali 3:5–74

ikoni ya seminari
“Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote.”

Ni kwa jinsi gani ungeweza kujaribu kumshawishi mtu kwamba ni bora “kumtumaini Bwana” kuliko “kutegemea … ufahamu [wetu] wenyewe”? (Mithali 3:5). Ni ulinganishi gani au masomo gani ya vitendo ungeweza kutumia? Unapotafakari Mithali 3:5–7, fikiria njia ambazo unaweza kukamilisha sentensi kama hizi: Kumtumaini Bwana ni kama … Kutegemea uelewa wetu wenyewe ni kama …

Kwa nini si busara kutegemea uelewa wetu wenyewe? Ni kwa jinsi gani umegundua kwamba Bwana ni mwaminifu?

Hata hivyo, tunaweza kuona vigumu kumtumaini Bwana nyakati zingine. Kwa nini iwe hivyo? Mzee Gerrit W. Gong anapendekeza baadhi ya sababu, pamoja na ushauri wenye msaada, katika “Tumaini Tena” (Liahona, Nov. 2021, 97–99). Ni hadithi au mafundisho gani unayopata katika ujumbe huu ambayo yanaweza kumsaidia mtu kurejesha imani yao katika Bwana?

Vyote Mithali 3:6 na Mithali 4 hulinganisha maisha na “mapito” au “njia.” Unafikiri inamaanisha nini kumruhusu Bwana “anayanyooshe mapito [yako]”? (Mithali 3:6). Unapata nini katika sura ya 4 ambacho kinakusaidia “kutafakari pito la miguu [yako]”? (mstari wa 26). Kwa mfano, nini mstari wa 11–12 na 18–19 inakufundisha kuhusu baraka za kufuata njia sahihi? Je, mstari wa 26–27 inamaanisha nini kwako wewe?

Ona pia 2 Nefi 31:18–21; “Lord, I Would Follow Thee,” Nyimbo za Dini, na. 220.

Mithali 15; 16:24–32

“Jibu la upole huondoa hasira.”

Baadhi ya mawazo katika Mithali15–16 yanaweza kukuhimiza kuboresha jinsi unayowasiliana na wengine, haswa wapendwa. Kwa mfano, fikiria kuhusu nyakati mahususi ambapo “jibu la upole” lilisaidia “[kugeuza] ghadhabu” (Mithali 15:1).

Unaweza pia kufikiria nyakati ambazo Mwokozi alionyesha mfano wa mafundisho katika Mithali 15:1–4, 18 (ona Marko 12:13–17; Yohana 8:1–11). Je, ni kwa jinsi gani unaweza kufuata mfano Wake unapotangamana na wengine?

Ni kwa jinsi gani ushauri katika Mithali 15; 16:24–32 unatumika katika mawasiliano ya kidijitali ya leo? Ona kama unaweza kupata mstari katika sura hizi ambao unaweza kufafanua upya kama ushauri kuhusu kujumuika kwenye mitandao ya kijamii au kupitia maandishi.

Ona pia Neil L. Andersen, “Kumfuata Yesu: Kuwa Mpatanishi,” Liahona, Mei 2022, 17–20; Ronald A. Rasband, “Maneno Ni Muhimu,” Liahona, Mei 2024, 70–77; Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana: Mwongozo wa Kufanya Chaguzi (2022), 11–12.

mwanamke na shakwe wa baharini

Nani Anaweza Kumpata Mwanamke Mwema? II, na Louise Parker

Mithali 31:10–31.

“Mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa.”

Mithali 31:10–31 inaelezea “mwanamke mwema,” au mwanamke mwenye nguvu kubwa ya kiroho, uwezo, na ushawishi. Unaweza kujaribu kufupisha kwa maneno yako mwenyewe nini kila moja ya aya hizi zinasema kuhusu mwanamke mwema. Ni sifa ipi kati ya hizi wewe unaweza kuiga?

Mhubiri 1–3;12

Maisha ya Duniani ni ya muda.

Kwa nini ni muhimu kwako kukumbuka kwamba mengi katika ulimwengu huu, kama vile Mhubiri 1–2 inasisitiza, ni “ubatili” (au ni ya muda na mara nyingi siyo muhimu)? Unagundua nini katika Mhubiri 12 ambacho huupatia uzima thamani ya milele?

Kwa ajili ya zaidi, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .

ikoni ya sehemu ya watoto

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Mithali 1:7; 2:5; 15:33; 16:6; Mhubiri 12:13

“Kumcha Mungu” humaanisha kumpenda na kumtii Yeye.

  • Ili kuwasaidia watoto wako waelewe vifungu kuhusu kumcha Mungu, ungeweza kubadilisha neno “woga” kwa maneno kama staha, upendo, au utii (ona pia Waebrania 12:28). Ni kwa jinsi gani hii inaleta matokeo ya jinsi tunavyofikiria kuhusu mistari hii? Ni kwa jinsi gani tunaonyesha kwamba tunamcha Bwana?

Mithali 3:5–7

Ninaweza kutumaini katika Bwana kwa moyo wangu wote.

  • Wewe na watoto wako mngeweza kubuni vitendo vinavyoendana na Mithali 3:5–7, kama vile kutengeneza moyo kwa mikono yako, ukiegemea upande mmoja, ukitembea mahali pamoja na kuelekeza macho yako. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuonyesha kwamba tunamwamini Yesu Kristo kwa mioyo yetu yote?

  • Ili kuonyesha kile inachomaanisha “usizitegemee akili zako mwenyewe” (Mithali 3:5), fikiria kuwaalika watoto wako waegemee kitu thabiti na imara, kama ukuta. Kisha wangeweza kujaribu kuegemea kitu ambacho sio thabiti, kama ufagio. Au wanaweza kujaribu kuegemeza fimbo au penseli dhidi ya vitu vyenye uthabiti tofauti, kama vile kitabu au kipande cha karatasi. Kwa nini ni muhimu “kumtumaini Bwana” (mstari wa 5) na kutozitegemea “akili zetu wenyewe”?

mwanamke aliyezama katika mawazo akiwa na ua

Kujifunza Kumtumainia Bwana, na Kathleen Peterson

Mithali 15:1, 18

Ninaweza kutumia maneno ya ukarimu.

  • Pengine wewe na watoto wako mnaweza kufikiria hali ambapo wewe au wao mnaweza kuhisi hasira. Someni Mithali 15:1 pamoja, na wasaidie watoto wako watumie mstari huu katika hali walizofikiria. Labda wangeweza kufanya mazoezi ya “majibu laini.” Wimbo kuhusu ukarimu, kama vile “Love Is Spoken Here” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 190–91), ungeweza kuimarisha kanuni hii.

  • Ili kujifunza kile inamaanisha “kutokuwa mwepesi wa hasira” (Mithali 15:18), wewe na watoto mngeweza kushiriki nyakati ninyi (au mtu mnayemjua) alipohisi hasira lakini akachagua kuwa mkarimu. Wasaidie watoto wako wafikirie juu ya mambo tunayoweza kuwa wepesi kama tutakuwa wapole kwa hasira.” Kwa mfano, tunaweza kuwa wepesi kufikiria kuhusu Yesu, kumwomba Baba wa Mbinguni msaada, kufikiria wimbo wa Watoto, au, kama inawezekana, kuondoka.

Kwa ziada, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki.

Yesu akiwaongoza kondoo wawili

“Katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako” (Mithali 3:6). Yeye Ananiongoza, na Yongsung Kim Picha kwa hisani ya havenlight.com

Ukurasa wa shughuli ya Watoto: Ninaweza kutumia maneno ya ukarimu