Njoo, Unifuate
Agosti 24–30. “Nami Nitayatangaza Aliyonitendea Roho Yangu”: Zaburi 49–51; 61–66; 69–72; 77–78; 85–86


“Agosti 24–30. ‘Nami Nitayatangaza Aliyonitendea Roho Yangu’: Zaburi 49–51; 61–66; 69–72; 77–78; 85–86,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)

“Agosti 24–30. ‘Nami Nitayatangaza Aliyonitendea Roho Yangu,’” Njoo, Unifuate: Agano la Kale 2026

Yesu ameshikilia taa usiku

Kuokoa Kile Kilichokuwa Kimepotea, na Michael Malm

Agosti 24–30: “Nami Nitayatangaza Aliyonitendea Roho Yangu”

Zaburi 49–51; 61–66; 69–72; 77–78; 85–86

Waandishi wa Zaburi walishiriki hisia binafsi za ndani katika ushairi wao. Waliandika kuhusu hisia za kukata tamaa, hofu, na majuto. Kwa wakati fulani, hata kuhisi wametelekezwa na Mungu, na baadhi ya zaburi zinabeba sauti ya kuvunjika moyo au kukatishwa tamaa. Kama uliwahi kuhisi kwa njia hiyo, kusoma Zaburi kunaweza kukusaidia kujua kwamba sio wewe pekee yako. Lakini pia utaona zaburi ambazo zinaweza kukutia moyo unapokuwa na hisia kama hizo, kwa sababu watunga zaburi pia walimtukuza Bwana kwa wema Wake, walishangazwa na nguvu Zake, na kufurahi kwa huruma Yake. Walijua kwamba wamelemewa na uovu na dhambi ila kwamba Bwana ni “mwema, na amekuwa tayari kusamehe” (Zaburi 86:5). Walielewa kwamba kuwa na imani katika Bwana haina maana kwamba kamwe hutapambana na mahangaiko, dhambi, au woga. Inamaanisha kwamba unajua nani wa kumwendea unapokuwa katika hali hiyo.

ikoni ya kujifunza

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Zaburi 49; 62:5–12

Ukombozi huja kwa njia ya Yesu Kristo pekee.

Zaburi 49 ina ujumbe kwa ajili ya “wote wakuu na wadogo, tajiri na maskini” (mstari wa 2). Ungeweza kusema ujumbe huu ni nini? Unahisi Zaburi 62:5–12 inaongeza nini katika ujumbe huo?

Kusoma zaburi hizi kungeweza kukupa mwongozo kutafakari njia tunazojaribiwa kuweka imani katika kitu kingine badala ya Mungu kwa ajili ya ukombozi (ona Zaburi 49:6–7). Ni kwa jinsi gani maisha yako yameshawishiwa na ushuhuda wako kwamba “Mungu atakomboa nafsi [yako], kutokana na nguvu ya kaburi”? (Zaburi 49:15).

Zaburi 51; 85–86

ikoni ya seminari
Kwa sababu ya huruma ya Mwokozi, ninaweza kusamehewa.

Mfalme Daudi aliandika Zaburi 51 baada ya kutambua haja yake ya mwisho ya kupata msamaha —kitu ambacho sote tunahitaji. Ni mistari ipi inaelezea hisia ambazo umekuwa nazo? Unapata nini katika zaburi hii ambacho kinakupa tumaini la msamaha?

Unaweza pia kupekua Zaburi 51 kwa vidokezo kuhusu kile inachomaanisha kutubu. Tengeneza orodha ya kile unachopata. Ona ikiwa unaweza kuongeza kwenye orodha yako kwa kupekua ujumbe wa Rais Russell M. Nelson “Tunaweza Kufanya Vizuri na Kuwa Wazuri” (Liahona, Mei 2019, 67–69).

Ni kwa jinsi gani ungeelezea jinsi wewe unavyojisikia kupokea msamaha kupitia Kristo? Kama unahitaji msaada kuelezea hisia zako, ungeweza kuangalia katika Zaburi 51:1–2, 7–12; 85:2–9. Baadhi ya watu hupenda kuchora au kutafuta picha zinazoonyesha hisia zao; unaweza kujaribu hilo. Mngeweza pia kuimba au kusikiliza wimbo kuhusu Mwokozi, kama vile “Nastaajabu” (Nyimbo za Dini, na. 106).

Ili kutubu, tunahitaji imani sio tu kwamba Yesu Kristo anaweza kutusafisha lakini pia kwamba Yeye atafanya hivyo. Unapata nini katika Zaburi 86:5, 13, 15 ambacho kinakusaidia kujua Mwokozi anaweza na yuko tayari kusamehe?

Ona pia Alma 36; Peter F. Meurs, “Angeweza Kuniponya!,” Liahona, Mei 2023, 39–41.

Zaburi 51:13–15; 66:5–20; 71:15–24

Ushuhuda wangu juu ya Yesu Kristo unaweza kuwasaidia wengine kuja Kwake.

Tafakari jinsi ulivyopata ushuhuda wako juu ya Yesu Kristo na nguvu Zake za kulipia dhambi. Kisha, unapojifunza, Zaburi 51:13–15; 66:5–20; 71:15–24, fikiria namna unavyoweza kuwaalika wengine “kuja na kuyatazama matendo ya Mungu” (Zaburi 66:5). Kama ungetaka “kutangaza kile [Bwana] alichoitendea roho [yako]” (Zaburi 66:16), ungetangaza nini?

Inamaanisha nini kwako “kusimulia haki [Yake] mchana kutwa.” (Zaburi 71:24).

Ona pia Alma 26.

mvulana akishiriki maandiko na wengine

“Njoni, sikie, … Nami nitayatangaza kile [Mungu] alichokifanya kwa ajili ya roho yangu” (Zaburi 66:16).

Zaburi 63; 69; 77–78

Bwana atanisaidia katika nyakati zangu za uhitaji.

Zaburi kadhaa zinaelezea jinsi ilivyo kujisikia uko mbali na Mungu na kuhitaji sana msaada Wake (ona Zaburi 63:1, 8; 69:1–8, 18–21; 77:1–9). Katika Zaburi 6369; 77–78, unapata nini ambacho kiliwapa watunga zaburi uhakika tena?

Unapokuwa na dhiki, ni kwa jinsi gani “kukumbuka matendo ya Bwana” na “maajabu Yake ya kale” kunakusaidia? (Zaburi 77:11). Baadhi ya maajabu haya yanaelezwa katika Zaburi 78. Wakati unapoyasoma, tafakari kile kinachokusaidia “umwekee Mungu tumaini [lako]” (mstari wa 7).

Kwa ziada, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana..

ikoni ya sehemu ya watoto

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Kwa sababu Jumapili hii ni Jumapili ya tano ya mwezi, walimu wa madarasa ya Msingi wanahimizwa kutumia shughuli za kujifunza katika “Kiambatisho B: Kuwaandaa Watoto kwa Ajili ya Maisha Yote kwenye Njia ya Mungu ya Agano.”

Zaburi 51; 86:5, 13, 15

Wakati ninapofanya uchaguzi usio sahihi, Yesu anaweza kunisaidia kubadilika.

  • Ili kuwasaidia watoto wako wagundue kweli kuhusu toba katika Zaburi 51, ungeweza kuchora moyo mkubwa. Kisha ungeweza kuwasaidia watoto wako kuandika ndani ya moyo mambo mabaya ambayo Shetani hutujaribu ili tufanye. Ni kwa jinsi gani tunayatoa mambo haya kutoka mioyoni mwetu? Waombe watoto wako watafute neno moyo katika Zaburi 51:10, 17. Zungumza kuhusu kile mistari hii inachofundisha kuhusu toba. Waache watoto wako wafute maneno ndani ya moyo na waandike maneno mapya ambayo yanaelezea njia ambazo Yesu anaweza kutubadilisha tunapotubu.

  • Unaweza kutaka kuwasaidia watoto wako wajifunze inamaanisha nini kuwa na “moyo uliovunjika na uliopondeka” (Zaburi 51:17). Wangeweza kufanya zamu kuvunja kitu ambacho kina ganda gumu, kama vile yai au nazi. Ungeweza kuwasaidia kulinganisha ganda na vitu ambavyo vinatuzuia kuhisi upendo wa Baba wa Mbinguni. Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kufungua moyo wetu Kwake?

  • Mngeweza pia kutazama picha ya Mwokozi pamoja na uwaulize watoto wako ni maneno gani wangeyatumia kumwelezea Yeye. Waalike wao watafute maneno ambayo yanamwelezea Mwokozi katika Zaburi 86:5, 13, 15. Kwa nini ni muhimu kujua kuhusu vitu hivi kumhusu Yeye?

Zaburi 61:2–3

Yesu Kristo ni mwamba wangu.

  • Watoto wako wangeweza kufurahia kuchora picha za ishara katika Zaburi 61:2–3. Ni kwa jinsi gani Yesu Kristo ni kama “mwamba” mkubwa (mstari wa 2), “kimbilio,” na “ngome yenye nguvu”? (mstari wa 3).

mnara wa mlinzi uliojengwa kwa mawe

“Kwa maana ulikuwa kimbilio langu, ngome yenye nguvu” (Zaburi 61:3).

Zaburi 66:16; 77:11; 78:6–7

“Nitayakumbuka matendo ya Bwana.”

  • Waombe watoto wako washiriki baadhi ya hadithi zao wanazopenda za maandiko (picha kutoka kwenye Kitabu cha Sanaa ya Injili zinaweza kusaidia). Hadithi hizi zinatufundisha nini kuhusu Bwana? Mngeweza kusoma pamoja Zaburi 66:16 na kuchukua zamu kujibu swali “Bwana amefanya nini kwa ajili ya nafsi yangu”?

  • Unaposoma Zaburi 77:11; 78:6–7 kwa pamoja, mngeweza kushiriki na kila mmoja jinsi mnavyojaribu “kuyakumbuka matendo ya Bwana” (Zaburi 77:11), ikijumuisha matendo Yake katika maisha yako. Sakramenti inatusaidiaje sisi “kumkumbuka daima? (Moroni 4:3; 5:2).

Zaburi 71:8

Ninaweza kuwaelezea wengine kuhusu Yesu Kristo.

  • Baada ya kusoma Zaburi 71:8 pamoja na watoto wako, waalike wachore mdomo mkubwa. Waombe wakusaidie “kujaza” mdomo huo na picha au maneno yanayowakilisha vitu tunavyoweza kuwaambia wengine kumhusu Yesu Kristo.

  • Ungeweza kupitisha picha ya Yesu Kristo. Mtu aliyeshikilia picha anaweza kusema kitu kimoja wanachokijua kumhusu Yeye. Ni jinsi gani tunaweza kuwasaidia watu wengine kujua kuhusu vitu hivi?

Watoto wana mengi ya kushiriki “Wakati ambapo watoto wanajifunza jambo geni, kawaida wanapenda kushiriki na wengine. Himiza hamu hii kwa kuwapatia watoto nafasi za kufundishana kanuni za injili, kwa wanafamilia wao, na marafiki zao. Pia waombe washiriki pamoja nawe fikira zao, hisia, na uzoefu unaohusiana na kanuni unazofundisha. Utagundua kwamba wanao umaizi ambao ni rahisi, safi, na wenye nguvu” (Kufundisha katika njia ya Mwokozi32).

Zaburi 86:7

Baba wa Mbinguni husikia na kujibu maombi yangu.

  • Zaburi nyingi ni kama sala kwa Mungu. Unaposoma Zaburi pamoja na watoto wako, unaweza kuwaonyesha mambo tunayoweza kutumia kuwasiliana na watu ambao wako mbali, kama vile simu au barua. Kisha someni Zaburi 86:7. Ni kwa jinsi gani tunaweza “kumuita” Baba wa Mbinguni? Je, Yeye hujibu kwa namna gani?

  • Mngeweza kuimba pamoja wimbo kuhusu sala, kama vile “A Child’s Prayer” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 12–13; ona pia Susan H. Porter, “Ombeni, Yeye Yupo,” Liahona, Mei 2024, 77–79). Simulianeni kuhusu wakati ambapo Mungu alijibu maombi yako.

Kwa ziada, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki.

picha ya Yesu

Njoo kwa Kristo, na Casey Childs

Ukurasa wa shughuli ya Watoto: Wakati ninapofanya uchaguzi usio sahihi, Yesu Kristo anaweza kunisaidia kubadilika