“Agosti 3–9. Esta: ‘Wewe Umekuja … kwa Ajili ya Wakati kama Huu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)
“Agosti 3–9. ‘Wewe Umekuja … kwa ajili ya Wakati Kama Huu,’” Njoo, Unifuate:Agano la Kale 2026
Malkia Esta Anaokoa Watu wa Yehova, na Sam Lawlor
Agosti 3– 9: “Wewe Umekuja … kwa ajili ya Wakati Kama Huu”
Esta
Matukio mengi katika kitabu cha Esta yanaweza kuonekana kama bahati nzuri au kudra. Ni kwa jinsi gani unaweza kueleza jinsi msichana wa Kiyahudi yatima aliweza kuwa malkia wa Uajemi kwa wakati stahiki kuokoa watu wake kutokana na kuchinjwa? Ni nafasi zipi ambazo Modekai binamu wa Esata itatokea asikie mpango wa kumuua mfalme? Je, haya yalikuwa bahati tu, au yalikuwa sehemu ya mpango mtakatifu? Mzee Ronald A. Rasband alisema: “Kile kinachoweza kuonekana kama bahati isiyo maalum, hakika, kinaonekana na Baba wa Mbinguni mwenye upendo. … Bwana yupo ndani ya vipengele vidogo vidogo vya maisha yetu” (“Kwa Usanifu Mtakatifu,” Liahona, Nov. 2017, 56). Tungeweza mara nyingi tusitambue ushawishi wa Bwana katika “vipengele hivi vidogo vidogo.” Lakini tunajifunza kutokana na uzoefu wa Esta kwamba Yeye anaweza kuongoza njia zetu na kutuandaa sisi “kwa ajili ya wakati kama huo” (Esta 4:14) ambapo tunapoweza kuwa vyombo katika mikono Yake kutimiza malengo Yake.
Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Esta, ona “Esta, kitabu cha” katika Kamusi ya Biblia.
Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani
Esta
Bwana hutuweka katika hali ambapo tunaweza kuwabariki watu wengine.
Rais Dieter F. Uchtdorf alifundisha kwamba kila mmoja wetu “anasimama mahali pa kipekee na ana kazi muhimu ambayo [sisi] pekee tunaweza kuifanya. … Bwana alikupa wewe majukumu yako kwa sababu fulani. Kunaweza kuwa na watu na mioyo ambayo wewe pekee unaweza kuifikia na kuigusa. Pengine hakuna mtu mwingine yeyote ambaye angeweza kufanya hivyo kwa njia sawa” (“Inua Pale Unaposimama,” Liahona, Nov. 2008, 56).
Unaposoma hadithi ya Esta, tafakari jinsi kauli hii inavyotumika kwake. Angalia njia ambazo Bwana alizitumia kufanya iwezekane kwake kuwaokoa Wayahudi (ona, kwa mfano, Esta 2:21–23; 3:10–14; 4:14–16). Kisha tafakari jinsi Yeye alivyokupa fursa za kuwabariki wengine. Ni katika baadhi ya hali zipi au mahusiano yapi ambayo Yeye amekuongoza wewe “kwa ajili ya wakati kama huo” (Esta 4:14). Ikiwa una baraka ya kipatriaki, fikiria kuisoma ili ujifunze zaidi kuhusu kazi ambayo Bwana anakutaka ufanye. Je, unaweza kufanya nini ili kutimiza kazi hii?
Ona pia “For Such a Time as This” (video), ChurchofJesusChrist.org.
For Such a Time as This
Tunajifunza zaidi kwa kufanya kuliko kwa kusikiliza. Mzee David A. Bednar alishauri walimu: “Kusudio letu halipaswi kuwa ‘Je, niwaambie nini?’ Badala yake, swali la kujiuliza wenyewe ni ‘Ni kipi ninaweza kuwaalika wafanye? Ni maswali gani yenye mwongozo wa kiungu ninayoweza kuuliza ambayo, kama wako tayari kujibu, yataanza kumwalika Roho Mtakatifu katika maisha yao?’” (katika Kufundisha Katika Njia ya Mwokozi, 25). Kama unaifundisha familia yako au darasa kuhusu Esta, ni nini ungeweza kuwaomba wafanye ambacho kitawasaidia kujifunza?
“Wakati Hamani alipoona kwamba Mordekai hakusujudia … kisha Hamani alijawa na ghadhabu” (Esta 3:5).
Esta 3; 5:9–14; 7
Kiburi na hasira vinaweza kuongoza kwenye anguko.
Katika kitabu cha Esta, tunajifunza kutoka katika uaminifu wa Esta na Mordekai lakini pia tunajifunza kutoka kwenye kiburi na hasira ya Hamani. Unaposoma Esta 3; 5:9–14, gundua hisia za Hamani, maneno, na matendo yake. Je, yanafunua nini kumhusu yeye na hamasa zake? Ni madhara yapi aliyapata? (ona Esta 7). Kusoma kuhusu Hamani kunaweza kukuchochea kutathimini kitu gani kinahamasisha hisia na matendo yako. Je, Unashawishika kufanya mabadiliko yoyote? Unawezaje kumgeukia Baba wa Mbinguni kwa ajili ya msaada?
Ona pia Mithali 16:32; Alma 5:28.
Esta 3–4; 5:2–3; 8:11–12
Kufunga kunaonyesha kwamba ninamwamini na kumtegemea Bwana.
Gundua kwa nini Esta na Wayahudi wengine waliamua kufunga (ona Esta 3:13; 4:1–3, 10–17). Je, ni kwa jinsi gani kufunga kuliwabariki wao? (ona Esta 5:2–3; 8:11–12). Kwa nini Bwana anatutaka tufunge? (ona Mada na Maswali, “Kufunga na Matoleo ya Mfungo,” Maktaba ya Injili). Fikiria jinsi unavyoweza kufanya kufunga kuwe baraka kubwa zaidi katika maisha yako.
Ona pia Isaiah 58:6–12; “Fasting: Young Single Adult Ward, Amanda” (video), ChurchofJesusChrist.org.
Fasting: Young Single Adult Ward, Amanda
Esta 3:1–11; 4:10–17; 5:1–4; 9:17–19
Kufanya jambo sahihi mara nyingi kuna hitaji ujasiri mkubwa.
Wakati Mordekai na Esta waliposimamia imani yao na watu wao, waliweka maisha yao hatarini. Chaguzi zetu zinaweza kuwa na matokeo makali sana, lakini kufanya jambo sahihi bado kunaweza kuhitaji ujasiri. Unajifunza nini kutoka katika Esta 3:1–4; 4:10–17 kuhusu kuwa na ujasiri kufanya jambo sahihi? Gundua matokeo tofauti ambayo Mordekai na Esta waliyapata baada ya kuonyesha ujasiri (ona Esta 3:5–11; 5:1–4). Esta na Mordekai walihitaji kujua nini kuhusu Mungu ili kufanya chaguzi walizofanya?
Fikiria juu ya hali ambapo unahitaji ujasiri wa kusimama kwa ajili ya kile kilicho sahihi. Unajifunza nini kutoka kwa Esta na Mordekai ambacho kinaweza kukusaidia kupata ujasiri katika Bwana?
Ujasiri wa Esta ulisababisha “siku ya furaha” (ona Esta 9:17–19). Ni kwa jinsi gani ujasiri kama wa Kristo umekupa “siku ya furaha”?
Ona pia “Courage,” “Dare to Stand Alone” (videos), Gospel Library; “Tupo Waaminifu wa Imani,” Nyimbo za Kanisa, na. 147.
Courage
Dare to Stand Alone
Kwa ziada, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .
Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto
Esta 2:5–7
Naweza kuitumikia familia yangu.
-
Unaweza kuhisi kutiwa msukumo kutumia Esta 2:7 kuwafundisha watoto wako kuhusu kuwasaidia wanafamilia wenye shida, kama Mordekai alivyomfanyia Esta. Mngeweza kusoma mstari pamoja au kuufanyia muhtasari kwa maneno yako mwenyewe. Kisha wewe na watoto wako mngeweza kuwafikiria wanafamilia ambao wangeweza kuhitaji msaada wenu. Tengenezeni mpango wa kuwasaidia.
Esta 3:1–11; 4:10–17
Bwana anaweza kunisaidia kuwa jasiri.
-
Mifano ya Esta na Mordekai inaweza kuwasaidia watoto wako waelewe kwamba ujasiri humaanisha kufanya kile kilicho sahihi hata wakati unapoogopa. Fikiria kuandika virai Mordekai alikuwa jasiri wakati yeye … na Esta alikuwa jasiri wakati … . Mnapojifunza hadithi ya Esta pamoja, watoto wako wangeweza kupendekeza njia za kumalizia sentensi. Ungeweza kusoma Esta 3:1–11; 4:10–17 au “Malkia Esta” (katika Hadithi za Agano la Kale, 166–70) au angalia picha katika muhtasari huu. Kisha andika Nitakuwa jasiri kwa …, na waalike watoto wako waorodheshe vitu ambavyo Baba wa Mbinguni anawataka wafanye ambavyo vinahitaji ujasiri. Wimbo kuhusu ujasiri, kama vile “Dare to Do Right” (Kitabu chaNyimbo za Watoto, 158), ungeweza kusaidia.
2:45Queen Esther
-
Waambie pia wajifunze kuhusu nyakati ambapo Yesu Kristo alikuwa jasiri; kwa mfano, wakati Yeye alipoteseka kwa ajili ya dhambi zetu, huko Gethsemane na msalabani (ona Mathayo 26:36–39; 27:33–35). Waombe watoto wako washiriki wakati ambapo walikuwa jasiri, na shiriki uzoefu wako mwenyewe pia.
Esta 4:1–3, 10–17
Kufunga huleta baraka za Bwana.
-
Kusoma Esta 4:1–3, 10–17 kunaweza kukusaidia kuwafundisha watoto wako kuhusu kufunga. Kwa nini Esta na Wayahudi walifunga? Waambie watoto wako kwa nini unafunga. Ungeweza pia kuwauliza jinsi ambavyo wangeelezea kufunga kwa rafiki ambaye hajawahi kufanya hivyo hapo awali. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuwasaidia rafiki zetu kuelewa baraka ambazo huja kutokana na kufunga?
-
Wahimize watoto wako wafikirie kitu fulani ambacho wangeweza kuhitaji msaada wa Bwana. Pendekeza wafanye hilo kuwa sehemu yao ya mfungo kwa Jumapili ijayo ya mfungo.
Kwa sababu Esta alikuwa jasiri, aliweza kuwaokoa watu wa Bwana.
Esta 4:14
Ninaweza kuwa chombo katika mikono ya Mungu.
-
Wasaidie watoto wako waelewe kwamba wakati Esta alipokuwa na hofu, Mordekai alimtia moyo kwa kuelezea kwamba Bwana alimsaidia kuwa malkia “kwa wakati kama huo” (Esta 4:14). Mordekai alimaanisha nini kwa hili? Zungumza na kila mmoja kuhusu jinsi Esta alivyokuwa chombo cha Bwana. Tunawezaje kuwa vyombo vya Bwana?
-
Unawezaje kuwasaidia watoto wako waelewe chombo ni kitu gani? Pengine ungeweza kumwalika mtu fulani kupiga wimbo kwenye chombo cha muziki au kuonyesha picha ya mtu akitumia chombo. Ungeweza pia kuzungumza kuhusu kile inamaanisha kuwa chombo katika mikono ya Mungu.
Kwa ziada, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .