Njoo, Unifuate
Agosti 17–23. “Bwana Ndiye Mchungaji Wangu”: Zaburi 1–2; 8; 19–33; 40; 46


“Agosti 17–23. ‘Bwana Ndiye Mchungaji Wangu’: Zaburi 1–2; 8; 19–33; 40; 46,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)

“Agosti 17–23. ‘Bwana Ndiye Mchungaji Wangu,’” Njoo, Unifuate: Agano la Kale 2026

Yesu akiwaongoza kondoo

Bwana Ndiye Mchungaji Wangu, na Yongsung Kim. Picha kwa hisani ya havenlight.com

Agosti 17–23: “Bwana Ndiye Mchungaji Wangu”

Zaburi 1–2; 8; 19–33; 4046

Hatujui kwa uhakika nani aliandika Zaburi. Baadhi zimehusishwa na Mfalme Daudi, lakini nyingi zake, waandishi wake hawajulikani. Bado hata baada ya kusoma Zaburi, tunahisi kama vile tunajua mioyo ya watunga zaburi, hata kama hatujui majina yao. Tunafahamu kwamba Zaburi ilikuwa ni sehemu muhimu ya kuabudu kwa Waisraeli, na tunajua kwamba Mwokozi alizinukuu mara kwa mara. Katika Zaburi, tunapata dirisha kuingia kwenye moyo wa watu wa kale wa Mungu. Tunaona jinsi walivyojisikia kuhusu Mungu, kitu gani wao walichohofia, na namna walivyopata amani. Kama waaminio leo, duniani kote, bado tunatumia maneno haya katika kumwabudu kwetu Mungu. Ni kama waandishi wa Zaburi walikuwa na dirisha ndani ya nafsi zetu , kwa sababu walielezea jinsi tunavyojisikia kuhusu Mungu, kile tunachohofia, na jinsi tunavyopata amani.

Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Zaburi, ona “Zaburi” katika Kamusi ya Biblia.

ikoni ya kujifunza

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Zaburi 1; 23; 26–2846

“Nami nimemtumaini … Bwana.”

Unaposoma Zaburi, unaweza kugundua ni mara ngapi waandishi wanaelezea hofu, huzuni, au wasiwasi. Hisia kama hizi ni za kawaida, hata kwa watu wa imani. Lakini kile kinachosababisha Zaburi kuleta msukumo ni kwamba pia inatoa suluhisho zenye msukumo, ikijumuisha kumtumainia Bwana kabisa. Unaposoma Zaburi 1; 23; 26–2846, andika:

  • Mwaliko wa kumtumainia Bwana:

  • Maneno ambayo yanamwelezea Yeye.

  • Maneno yanayoelezea amani, nguvu, na baraka zingine Yeye anazotoa.

  • Maneno ambayo huwaelezea watu ambao wanamtumaini Yeye.

Pia angalia picha za wazi na ishara ambazo Zaburi hutumia kufundisha kuhusu Mwokozi. Kwa mfano, katika Zaburi 23, ni nini virai kama “katika malisho ya majani mabichi hunilaza” au “maji ya utulivu” (mstari wa 2) huleta akilini? Je, “gongo” na “fimbo” vyanifariji (mstari wa 4) vinaashiria nini? Inaweza kumaanisha nini kwa “kikombe” chetu (mstari wa 5) kinafurika?

Zaburi 222

Yesu Kristo ndiye Masiya aliyeahidiwa.

Zaburi nyingi huelekeza kwenye maisha ya duniani ya Yesu Kristo. Wakristo katika nyakati za Agano Jipya waliona miunganiko hii pia. Fikiria kusoma marejeo ya maandiko yafuatayo. Tafuta uhusiano kati ya maneno katika zaburi hizi na maisha ya Mwokozi:

  • Zaburi 2:1–3 na Matendo ya Mitume 4:24–28

  • Zaburi 2:7 na Matendo ya Mitume 13:30–33

  • Zaburi 22:1 na Mathayo 27:45–46

  • Zaburi 22:7-8 (ona Mathayo 27:39–43)

  • Zaburi 22:16 na Luka 23:32–33

  • Zaburi 22:18 na Mathayo 27:35

  • Zaburi 31:5 na Luka 23:46

Je, unajifunza nini kutokana na kujifunza miunganiko hii? Ni unabii na ahadi gani za kimaandiko bado hazijatimizwa? Unapata nini katika ahadi hizi ambazo hukupa tumaini kwa ajili ya siku za usoni?

mto na mawe

Zaburi 8; 1933

“Nchi imejaa fadhili za Bwana.”

Kusoma Zaburi 8; 19; na 33 kunaweza kukupa msukumo kufikiria uumbaji wa ajabu wa Bwana. Zingatia hisia zako unapofanya hivyo. Ungeweza pia kutaka kuimba au kutafakari maneno ya wimbo unaohusiana na zaburi hizi kama vile “How Great Thou Art” (Hymns, 86). Ni kwa jinsi gani uumbaji wa Bwana “huhubiri utukufu wa Mungu” kwako (Zaburi 19:1).

Hapa kuna baadhi ya nyimbo zingine zilizoongozwa na Zaburi:

Tumia muziki. Rais Dallin H. Oaks said: “Kuimba nyimbo za dini ni njia bora za kujiweka katika uwiano na Roho wa Bwana. … Muziki mtakatifu una uwezo wa kipekee wa kuwasilisha hisia zetu za upendo kwa Bwana. Aina hii ya mawasiliano ni msaada wa ajabu kwa kuabudu kwetu. … Nyimbo zetu za dini zina mahubiri ya kimafundisho yasiyo na kifani, yaliyozidiwa tu na maandiko katika ukweli wake na athari ya kishairi” (“Worship through Music,” Ensign, Nov. 1994, 10, 11). Ni nyimbo zipi zinazohusiana na Zaburi ungeweza kusikiliza au kuimba ili kuboresha kuabudu kwako wiki hii?

Zaburi 19:7–1129

Neno la Bwana lina nguvu, “huiburudisha nafsi.”

Katika Zaburi, maneno kama ushuhuda, sheria, amri, na hukumu yanaweza kurejelea neno la Bwana. Kumbuka hilo unaposoma Zaburi 19:7–11. Mistari hii inapendekeza nini kwako kuhusu neno la Bwana? Zaburi 29 inakufundisha nini kuhusu sauti Yake? Katika uzoefu wako, ni kwa jinsi gani neno, au sauti ya Bwana iliendana na maelezo haya?

Zaburi 24; 26–27

ikoni ya seminari
Mwokozi anaweza kunisaidia kuwa msafi ili niweze kuingia katika uwepo wa Mungu.

Kwa sababu hekalu huko Yerusalemu lilijengwa kilimani, kirai “mlima wa Bwana” (Zaburi 24:3) kingeweza kumaanisha hekalu au kwenye uwepo wa Mungu. Hii inaongeza nini katika uelewa wako wa Zaburi 24? Inamaanisha nini kwako kuwa na “mikono safi na moyo mweupe”? (mstari wa 4). Unaposoma Zaburi 26–27, ni kipi kingine unajifunza kuhusu nyumba ya Bwana?

Wakati mwingine, tunaweza kukata tamaa kusikia kwamba tunahitaji kuwa wasafi ili kuingia katika uwepo wa Mungu. Hata hivyo, sote tunahangaika, na hakuna kati yetu aliye mkamilifu. Ni tumaini gani unapata katika ujumbe wa Mzee David A. Bednar “Mikono Safi na Moyo Safi”? (Liahona, Nov. 2007, 80–83). Unawezaje kutumia ujumbe wake kumsaidia mtu anayehisi kuzidiwa na kutaka kuwa mkamilifu? Fikiria jinsi unavyoweza kupokea msaada wa Mwokozi katika juhudi zako za kuwa na “mikono safi na moyo safi.”

Ona pia Bradley R. Wilcox, “Ustahili Si Kukosa Dosari,” Liahona, Nov. 2021, 61–67.

Kwa ajili ya zaidi, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana.

ikoni ya sehemu ya watoto

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Zaburi 23; 27–28; 3246

Bwana ananipa amani, nguvu na mwongozo.

  • Fikiria kuandika Bwana ni … Waalike watoto wako watafute njia za kukamilisha sentensi hiyo wakitumia maandiko kama haya: Zaburi 23:1; 27:1; 28:1; 28:7; 32:7; 46:1. Je, maandiko haya yanatufundisha nini kuhusu jinsi Bwana anavyoweza kutusaidia sisi?

  • Unaweza kujadiliana na watoto wako ni nini mwanakondoo anahitaji ili kuwa salama na mwenye afya. Kisha, mnaposoma pamoja Zaburi 23, wasaidie watoto wako walinganishe kile mchungaji anachofanya kwa ajili ya mwanakondoo na kile Yesu anachotufanya kwa ajili yetu. Tunahitaji nini ili tuwe salama na wenye afya kiroho? Imbeni pamoja wimbo ambao ungeweza kuwapa mawazo, kama vile “I Feel My Savior’s Love” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 74–75).

Hekalu la Concepción Chile

Hekalu la Concepción Chile

Zaburi 24:3–4

Ili kuingia hekaluni, tunahitaji “mikono safi na moyo mweupe.”

  • Mnaposoma Zaburi 24:3 pamoja, watoto wako wangeweza kutafuta maneno ambayo yanawakumbusha juu ya hekalu. Wangeweza pia kutazama picha ya hekalu. Kisha mngeweza kusoma pamoja mstari wa 4 ili kujifunza nani anaweza kuingia hekaluni. Ungeweza kuzungumza kuhusu jinsi mikono inapokuwa michafu na jinsi tunavyoisafisha. Ni kwa jinsi gani tunakuwa wachafu kiroho? Ni kwa jinsi gani Mwokozi anasaidia kutusafisha kiroho?

Zaburi 30:5

Yesu Kristo anaweza kugeuza huzuni kuwa shangwe.

  • Ikiwa una watoto wadogo, ungeweza kuwaalika wao wajifanye wanalia wakati unasoma kutoka katika Zaburi 30:5, “Kkulia kunaweza kudumu kwa usiku.” Kisha waombe waonyeshe shangwe unaposoma, “Lakini asubuhi huwa furaha.” Rudia kirai hiki mara chache.

  • Onyesha picha ya Mwokozi, na waambie watoto wako kile Yeye amefanya kwa ajili yako ambacho hukuletea shangwe. Ungeweza kumpa kila mtoto zamu ya kunyanyua picha na kushiriki kile Yesu amefanya ambacho huwaletea shangwe.

Zaburi 46:10

“Tulieni,na mjue kuwa Mimi ni Mungu.”

  • Wasaidie watoto wako kukariri mstari wa kwanza kutoka katika Zaburi 46:10: “Acheni, mjue kuwa Mimi ni Mungu.” Je, inamaanisha nini “kutulia”? Pengine ungeweza kutumia muda kiasi kujifanyia mazoezi ya kutulia. Ungeweza pia kushiriki na kila mmoja uzoefu wakati ulipokuwa “umetulia” kuliimarisha uhusiano wako na Mungu. Wasaidie watoto wako wafikirie nyakati katika siku ambapo wanaweza “kutulia” kuhisi kuwa karibu na Baba wa Mbinguni.

Kwa ziada, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .

Mwokozi akiwa amemshikilia mwanakondoo

Mchungaji Mwema, na Eva Timothy

Ukurasa wa shughuli ya Watoto: “Bwana ndiye Mchungaji wangu”