Njoo, Unifuate
Januari 30–Februari 1. “Kuyafundisha Mambo Haya Kwa Uhuru kwa Watoto Wenu”: Mwanzo 5; Musa 6


“Januari 26–Februari 1. ‘Kuyafundisha Mambo Haya Kwa Uhuru kwa Watoto Wenu’: Mwanzo 5; Musa 6,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)

“Januari 26–Februari 1. ‘Kuyafundisha Mambo Haya Kwa Uhuru kwa Watoto Wenu’,” Njoo, Unifuate: 2026

Adamu na Hawa

Bora kuliko Paradiso, na Kendal Ray Johnson

Mwanzo 5; Musa 1: “Kuyafundisha Mambo Haya Kwa Uhuru kwa Watoto Wenu”

Mwanzo 5; Musa 6

Sehemu kubwa ya Mwanzo 5 ni orodha ya vizazi kati ya Adamu na Hawa na Nuhu. Tunasoma majina mengi, lakini hatujifunzi mengi kuhusu watu hao. Kisha tunasoma mstari huu wa kuvutia sana lakini usiofafanuliwa: “Na Henoko akaenda pamoja na Mungu: naye akatoweka; maana Mungu alimtwaa” (Mwanzo 5:24). Hakika pana hadithi nyuma ya mstari huu! Lakini bila ufafanuzi wa ziada, orodha ya vizazi inaendelea.

Kwa shukrani, Musa 6 inafunua maelezo ya kina ya hadithi ya Henoko—na ni hadithi nzuri. Tunajifunza juu ya unyenyekevu wa Henoko, wasi wasi wake, uwezekano ambao Mungu aliuona ndani yake, na kazi kubwa aliyoifanya kama nabii wa Mungu. Pia tunapata picha ya wazi juu ya familia ya Adamu na Hawa ikiendelea kupitia vizazi vingi. Tunasoma juu ya “utawala mkuu” wa Shetani lakini pia wa wazazi ambao waliwafundisha watoto “njia za Mungu” (Musa 6:15, 21). Cha thamani hasa ni kile tunachojifunza kuhusu mafundisho ambayo wazazi hawa na wahubiri walifundisha: imani katika Yesu Kristo, toba, ubatizo, na kumpokea Roho Mtakatifu (ona Musa 6:50–52). Mafundisho haya, kama ukuhani unaoambatana nayo, “ulikuwepo hapo mwanzo [na] utakuwepo mwisho wa ulimwengu pia” (Musa 6:7).

ikoni ya kujifunza

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Musa 6:26–36

Dhambi huzuia uwezo wangu wa kuona, kuhisi, na kusikia mambo ya Mungu.

Unaposoma Musa 6:26–36, unajifunza nini kuhusu athari za dhambi? Ni kwa jinsi gani wewe umeona athari hizi? Ni sifa gani Henoko alizokuwa nazo ambazo zilimsaidia kushinda athari hizi? Ni kwa jinsi gani Mungu alimbariki kama matokeo yake?

Musa 6:26–47

ikoni ya seminari
Mungu ananiita mimi kufanya kazi yake licha ya mapungufu yangu.

Kama utawahi kuhisi kuzidiwa na kile ambacho Bwana amekuita ufanye, hauko peke yako. Hata Henoko alijisikia hivyo hivyo wakati Bwana alipomwita yeye kuwa nabii. Unaposoma Musa 6:26-36, angalia ni kwa nini Henoko alijisikia kuzidiwa na kitu ambacho Bwana alichosema ili kumpa ujasiri.

Katika mstari wa 37–47, tafuta njia ambazo Bwana alimsaidia Henoko na zilimpa nguvu ya kutimiza kazi Yake (ona pia Musa 7:13). Unaweza kulinganisha uzoefu wa Henoko na ule wa manabii wengine ambao walijiona wana mapungufu, kama vile Musa (ona Kutoka 4:10–16), Yeremia (ona Yeremia 1:4–10), Nefi (ona 2 Nefi 33:1–4), na Moroni (ona Etheri 12:23–29). Je, unahisi Mungu anakutaka wewe ujifunze nini kutoka katika maandiko kuhusu kazi ambayo Yeye amekupa ufanye?

Henoko akisali

Mwonaji Bwana Amemwinua (Musa 6:36), na Eva Timothy

Wengi wa mitume na manabii wa leo wameelezea hisia zao zinazofanana na za Henoko wakati walipoelezea jinsi walivyohisi kupokea miito yao. Kwa mfano, ona ushuhuda wa Mzee Ulisses Soares katika “Manabii Wanazungumza kwa Uwezo wa Roho Mtakatifu” (Liahona, Mei 2018, 98–99).

Unaweza kujifunza nini kutoka kwa manabii na mitume hawa kuhusu hisia zako za mapungufu? Ni lini umehisi Mwokozi akikusaidia wakati alipokuomba ufanye mambo magumu? Fikiria kuandika matukio machache katika siku zako zijazo wakati utakapohitaji kutegemea msaada wa Mwokozi. Ni kwa jinsi gani unaweza kuyakabili matukio haya kwa imani katika Yesu Kristo?

Ona pia David A. Bednar, “Kaa Ndani Yangu, na Mie Ndani Yako; Kwa hiyo Tembea Pamoja Nami,Liahona, Mei 2023, 123–25; “I’ll Go Where You Want Me to Go,” Nyimbo za Dini, na, na.270.

Musa 6:48–68

Injili ya Yesu Kristo ilifunzwa kutoka mwanzo.

Kwa sababu tunacho kitabu cha Musa, tunajua kuwa Mungu amekuwa akifundisha watoto Wake jinsi ya kupata msamaha na ukombozi tangu Adamu na Hawa. Unaposoma Musa 6:48–68, pekua kwa ajili ya kitu gani ambacho ni lazima tukijue na kukifanya ili tukombolewe. Tazama swali la Adamu katika mstari wa 53. Je, ninyi mmeshawahi kushangaa hilo? Unajifunza nini kutokana na jibu la Bwana katika mstari wa 53–65? Unaweza kufikiria juu ya mistari hii kama ujumbe wa Bwana katika ibada ya ubatizo wa Adamu. Unajifunza nini kuhusu ubatizo kutokana na ujumbe wake? Kwa nini unafikiri alifananisha ubatizo na “kuzaliwa mara ya pili”? (mstari wa 59). Je, unaweza kufanya nini ili kuendelea “kuzaliwa mara ya pili” katika maisha yako yote?

Tafuta ishara. Katika maandiko, vitu au matukio mara nyingi yanaweza kuwakilisha au kuashiria kweli za kiroho, hususani kweli kuhusu Mwokozi (ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,7). Ishara hizi zinaweza kuimarisha uelewa wako juu Yake na mafundisho Yake. Kwa mfano, unajifunza nini kutokana na ishara za mioyo na masikio katika Musa 6:27, macho na udongo wa mfinyanzi katika Musa 6:35, au maji katika Musa 6:59–60?

Musa 6:51–62

“Kuyafundisha Mambo Haya Kwa Uhuru kwa Watoto Wenu.”

Baada ya kumfundisha Adamu kweli za injili ya Yesu Kristo, katika Musa 6:51–63, Bwana alimwambia Adamu azifundishe kweli hizo kwa vizazi vijavyo. Fikiria kutengeneza orodha ya kweli hizi. (Inaweza kusaidia kugawanya kifungu katika makundi madogo ya mistari, kama vile mstari wa 51–52, 53–57, 58–60, 61–63). Kwa nini kweli hizi ni za thamani kwa vizazi vinavyoinukia vya leo? Nini kingine wewe unaweza kujifunza kutoka katika maelekezo ya Bwana kwa wazazi katika Mosia 4:14–15 na Mafundisho na Maagano 68:25–28; 93:40–50?

Kusoma kuhusu “kitabu cha kumbukumbu” ambacho familia ya Adamu na Hawa walikitunza kunaweza kukuhamasiha wewe au familia yako kutengeneza kitabu chenu cha kumbukumbu. Je, unahisi Bwana angetaka ujumuishe nini? Zingatia kuweka taarifa kutoka katika kitabu chenu cha kumbukumbu katika FamilySearch.org.

Ona pia Dieter F. Uchtdorf, “Yesu Kristo Ni Nguvu kwa Wazazi,” Liahona, Mei 2023, 55–59; “Parenting: Touching the Hearts of Our Youth,” “But Why?” (video), Maktaba ya Injili.

familia ikisoma maandiko pamoja

Kwa ajili ya zaidi, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .

ikoni ya 01 ya sehemu ya watoto

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Musa 6:26–34

Mungu anaweza kunisaidia kufanya mambo magumu.

  • Wakati Henoko alipoitwa kuhubiri injili, alihofu kwamba atashindwa. Lakini Mungu alimsaidia. Someni pamoja hadithi hii katika Musa 6:26–34 (ona pia “Henoko Nabii” katika Hadithi za Agano la Kale, 19–21). Kwa nini Henoko alihisi kuwa hangeweza kuhubiri injili? (ona Musa 6:31). Je, ni kwa jinsi gani, Mungu alimsaidia Henoko? (ona Musa 6:32–34; 7:13).

  • Watoto wako wangeweza kufurahia kushiriki au kuigiza mifano mingine ya wakati Mungu alipowasaidia watu kufanya mambo magumu—kwa mfano, Nuhu, Daudi, Amoni, au Samweli Mlamani (ona Kitabu cha Sanaa ya Injili, na . 7, 19, 78,81). Ungeweza pia kushiriki uzoefu wako mwenyewe na waruhusu watoto wako wazungumze kuhusu jinsi Mungu anavyowasaidia kufanya mambo magumu.

Musa 6:50–62

Imani katika Kristo, toba, ubatizo na kumpokea Roho Mtakatifu kunaniandaa mimi kurudi kwa Mungu.

  • Mungu alimfundisha Adamu kile tunachohitaji kufanya ili kurudi Kwake—kuwa na imani katika Yesu Kristo, kutubu, kubatizwa, na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Wasaidie watoto wako watafute kanuni hizi katika Musa 6:52, 57. Kisha ungeweza kuwasaidia kuandika hotuba fupi kuhusu mojawapo ya kanuni hizo. Kila hotuba inaweza kujumuisha andiko, kutoka Musa 6, uzoefu, na ushuhuda. Waache washiriki hotuba zao wao kwa wao.

  • Ungeweza pia kuonyesha picha ambazo zinawakilisha kanuni za kwanza za injili (ona makala ya nne ya imani). Ziweke katika mstari unaoongoza kwenye picha ya Yesu Kristo. Unaposoma Musa 6:52, watoto wako wangeweza kusimama kando ya picha sahihi wakati wanaposikia maneno picha inawakilisha.

  • Watoto wako wangeweza kufurahia kuimba nyimbo ambazo zinafundisha kanuni katika Musa 6:52, kama vile “Faith,” “When I Am Baptized,” na “The Holy Ghost” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 96–97, 103, 105). Wasaidie watafute kanuni hizi katika Musa 6:52.

Musa 6:57–58

Baba wa Mbinguni anawataka wazazi kuwafundisha watoto wao.

  • Ili kuwahimiza watoto wako kuwasaidia wazazi wao katika wajibu wao kama walimu wa injili, fikiria kumuomba mtoto asome Musa 6:58 na kutambua amri ambayo Mungu aliwapa wazazi. Kisha ungeweza kuonyesha picha ya Adamu na Hawa wakiwafundisha watoto wao (kama ile iliyoko mwisho wa muhtasari huu) na waache watoto wako wazungumze kuhusu kile wanachokiona katika picha. Watoto wako wangeweza kuchora picha za familia zao wakisoma maandiko pamoja, wakisali pamoja, au kucheza pamoja.

Kwa ajili ya zaidi, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .

Adamu na Hawa wakiwafundisha watoto wao chini ya mti

Adamu na Hawa Wakiwafundisha Watoto Wao, na Del Parson

ukurasa wa shughuli wa Msingi: injili inanifundisha mimi jinsi ya kurudi kwa Baba wa Mbinguni