“Januari 19–25. Anguko la Adamu na Hawa: Mwanzo 3–4; Musa 4–5,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)
“Januari 19–25. Anguko la Adamu na Hawa,” Njoo, Unifuate: 2026
Adamu na Hawa, na Douglas M. Fryer
Januari 19–25: Anguko la Adamu na Hawa
Mwanzo 3–4; Musa 4–5
Mwanzoni, hadithi ya Anguko la Adamu na Hawa inaweza kuonekana kama janga. Adamu na hawa wakafukuzwa nje ya Bustani nzuri ya Edeni Walipelekwa kwenye ulimwengu wa maumivu, huzuni, na kifo (ona Mwanzo 3:16–19). Na walitengwa na Baba yao wa Mbinguni. Lakini kweli zilizorejeshwa kupitia Nabii Joseph Smith katika kitabu cha Musa zinatupatia mtazamo wa kipekee juu ya Anguko.
Ndio Bustani ya Edeni ilikuwa nzuri. Lakini Adamu na Hawa walihitaji zaidi ya mazingira mazuri. Wao walihitaji—na sisi sote tunahitaji—fursa ya kukua. Kuondoka Bustani ya Edeni ilikuwa hatua muhimu ya kwanza kuelekea kurudi kwa Mungu na hatimaye kuwa kama Yeye. Hii ilimaanisha kukabiliana na upinzani, kufanya chaguzi, kufanya makosa, kujifunza kutubu, na kumtumainiai Mwokozi, ambaye Upatanisho Wake unafanya uwezekano wa uendeleaji na “shangwe ya ukombozi wetu” (Musa 5:11). Kwa hiyo unaposoma kuhusu Anguko la Adamu na Hawa, usifokasi juu ya kinachoonekana kama janga bali juu ya uwezekano—siyo juu ya paradiso Adamu na Hawa waliyoipoteza bali juu ya utukufu ambao uchaguzi wao umeruhusu sisi kuupokea.
Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani
Mwanzo 3; Musa 4
Anguko lilikuwa sehemu muhimu ya mpango wa Mungu.
Ni kweli kwamba uchaguzi wa Adamu na Hawa ulisababisha matatizo mengi tunayopitia katika maisha ya duniani. Lakini hiyo haimaanishi tujutie uchaguzi wao. Unaposoma Mwanzo 3 na Musa 4, unaweza kujiuliza mwenyewe, kwa nini Anguko lilikuwa muhimu kwa mpango wa Mungu?
Kulingana na Musa 5:9–12, Adamu na Hawa walihisi vipi kuhusu Anguko? Ni kwa jinsi gani unaweza kutumia maneno yao kwenye uzoefu wako katika ulimwengu ulioanguka? Nini kingine unachojifunza kutoka 2 Nefi 2:19–25?
Ona pia Mosia 3:19; Alma 12:21–37;;na Mafundisho na Maagano 29:39–43.
Kuondoka Edeni, na Annie Henrie Nader
Mwanzo 3:1–7; Musa 4:22–31; 5:4–15
Yesu Kristo anatoa matumaini, na ukombozi.
Hadithi ya Adamu na Hawa ni moja ya matumaini na ukombozi kupitia Yesu Kristo. Kuona kwa nini, unaweza kuanza kwa kutafuta matokeo ya Anguko katika Mwanzo 3:1–7; Musa 4:22–31 na kuwekea alama au kuorodhesha kile unachopata. Ni kwa jinsi gani matokeo haya yanakuathiri? Kisha ungeweza kupekua Musa 5:4–15, ukitafuta mpango wa Mungu wa kutukomboa kutokana na athari hizo. Kwa nini Adamu na Hawa “walifurahi” baada ya malaika kuwatembelea? Je, unajifunza nini kutoka kwao kuhusu mpango wa Baba wa Mbinguni?
Ona pia “Because of Him” (video), Maktaba ya Injili.
Because of Him
Mwanzo 3:16; Musa 4:22
Inamaanisha nini kwamba Adamu alitakiwa kuwa “mtawala” wa Hawa?
Kifungu hiki cha maandiko wakati mwingine kimeeleweka vibaya kwa kumaanisha kwamba mwanamume anahalalishwa katika kumtendea mkewe vibaya. Katika siku zetu, manabii wa Bwana wamefundisha kwamba mume na mke wanapaswa kuonana kama wenza walio sawa katika kutimiza majukumu yao matakatifu katika familia (ona “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu” [Maktaba ya Injili]). Mzee Dale G. Renlund na Dada Ruth Lybbert Renlund walielezea kwamba mume mwenye haki “atatafuta kutumikia; atatambua kosa na atatafuta msamaha; atakuwa mwepesi kutoa sifa; atajali mapendeleo ya washiriki wa familia; atauona uzito mkuu wa wajibu wa kutoa ‘mahitaji muhimu ya maisha na ulinzi’ kwa ajili ya familia yake; atamtendea mke wake kwa heshima ya hali ya juu na kwa staha. … Ataibariki familia yake” (Ukuhani wa Melkizedeki: Kuelewa Mafundisho, Kuishi Kanuni [2018], 23).
Ninahitaji haki ya kujiamulia na upinzani ili kukua.
Mzee Dale G. Renlund alifundisha, “Lengo la Baba yetu wa Mbinguni katika uzazi siyo kufanya watoto Wake watende kile kilicho sahihi; ni kufanya watoto Wake wachague kutenda kile kilicho sahihi na hatimaye kuwa kama Yeye.” (“Chagueni Hivi Leo,” Liahona, Nov. 2018, 104). Kwa nini ni muhimu sana katika mpango wa Baba wa Mbinguni kwamba sisi tuchague kufanya kile kilicho sahihi?
Unaposoma Musa 4:1–4, tafuta kile Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo walichofanya ili kulinda haki yako ya kuchagua—haki yako ya kujiamulia. Ni kwa jinsi gani unaweza kupata nguvu zao za kulinda? Kwa ajili ya mawazo, fikiria kujifunza sehemu ya “Fanya chaguzi zenye mwongozo wa kiungu” katika Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana: Mwongozo wa Kufanya Chaguzi (4–5).
Fikiria pia kusoma kile ambacho Lehi alifundisha kuhusu haki ya kujiamulia katika 2 Nefi 2:11–20, 25–30. Kwa nini upinzani ni muhimu kwa haki ya kujiamulia? Ni kwa jinsi gani unaweza kuonyesha shukrani kwa Yesu Kristo kwa kukufanya uwe “huru kuchagua”? (2 Nefi 2:27)
Ona pia Dallin H. Oaks, “Upinzani katika Vitu Vyote,” Liahona, Mei 2016, 114–17; Mada na Maswali, “Haki ya Kujiamulia,” Maktaba ya Injili; “Chagua Jema,” Nyimbo za Dini, na. 135.
Ongeza ushiriki. Shughuli nyingi za kujifunza zinaweza kufanywa kama mtu binafsi, familia, au darasa, katika makundi madogo madogo; au katika jozi Tumia mbinu mbalimbali ili kuruhusu watu kushiriki ambao wasingeweza kwa njia yoyote kupata nafasi. Kwa shughuli hii, ungeweza kumwalika mtu mmoja au kikundi kusoma Musa 4 na ule mwongozo wa Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana wakati kikundi kingine kinajifunza mistari katika 2 Nefi 2. Kisha wangeweza kufundishana kile walichojifunza katika sehemu yao husika.
Shetani anatafuta “kunidanganya na kunipofusha”.
Unaposoma Musa 4:4–12; 5:13–33, fikiria kuorodhesha njia ambazo Shetani alijaribu kuwajaribu Adamu na Hawa na watoto wao. Ni kwa jinsi gani anajaribu kwa kutumia vitu sawa na hivi leo? Ni kwa jinsi gani Baba wa Mbinguni anakusaidia wewe kupinga uongo wa Shetani?
“Mimi, Bwana Mungu … niliwavika nguo.”
Baada ya kula tunda lililokatazwa, Adamu na Hawa walijaribu kufunika uchi wao wenyewe. Baadaye, Bwana alijitolea kuwavisha. Unaposoma Musa 4:13–16, 27, fikiria yafuatayo:
-
Tafakari uchi na mavazi vinaweza kuwakilisha nini katika maandiko (ona, kwa mfano, Ufunuo 7:9, 13–15; 2 Nefi 9:14; Mafundisho na Maagano 109:22–26, 76). Unajifunza nini kutokana na uzoefu wa Adamu na Hawa na uchi na mavazi?
-
Kama umepokea endaumenti hekaluni, fikiria Adamu na Hawa wangeweza kusema nini kwako kuhusu umuhimu wa vazi lako la hekaluni na kile linachowakilisha.
Ona pia “Sacred Temple Clothing” (video), Maktaba ya Injili.
Sacred Temple Clothing
Mungu atakubali dhabihu zangu kama ninazitoa kwa moyo ulio radhi na wa utiifu.
Unapojifunza Musa 5:4–9, 16–26, Fikiria mitizamo tofauti ya Adamu na Hawa, na watoto wao Kaini na Habili, kuhusu dhabihu. Je, ni kwa nini Bwana aliikubali dhabihu ya Habili lakini sio ya Kaini?
Je, Bwana anakutaka utoe dhabihu ya nini? Je, kuna chochote katika mistari hii ambacho huumba jinsi unavyofikiria kuhusu dhabihu hizo?
Kwa zaidi, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .
Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto
Yesu Kristo anatuokoa kutoka kwenye Anguko.
-
Ili kuwasaidia watoto wako waelewe vyema Anguko la Adamu na Hawa, ungeweza kunakili picha kutoka “Adamu na Hawa” (katika Hadithi za Agano la Kale, 13–16) na kuzikata. Kisha mnaweza kufanya kazi pamoja kuziweka picha katika mpangilio wakati mkijadili uzoefu wa Adamu na Hawa. Unapofanya hivyo, zungumza kuhusu kwa nini ilikuwa muhimu, katika mpango wa Baba wa Mbinguni, kwa Adamu na Hawa kuondoka kwenye Bustani ya Edeni.
-
Watoto wako wanaweza kuhisi shukrani kwa Upatanisho wa Yesu Kristo wanapoelewa jinsi Yeye anavyoshinda athari za Anguko. Mnaposoma pamoja Musa 4:25; 6:48; Warumi 5:12; 2 Nefi 2:22–23, wasaidie watoto wako watafute njia za kukamilisha sentensi hii: “Kwa sababu ya Anguko, mimi …” Kisha, mnaposoma pamoja Musa 5:8–11, 14–15; 6:59; Alma 11:42, wangeweza kukamilisha sentensi hii: “Kwa sababu ya Yesu Kristo, mimi …” Shiriki na kila mmoja na mwenzake shukrani zenu kwa ajili ya Yesu Kristo.
Ninaweza kuchagua mema.
-
Fikiria somo rahisi la vitendo ili kutambulisha kanuni ya haki ya kujiamulia: Waalike watoto kupaka rangi ukurasa wa shughuli za wiki hii, lakini wape rangi moja tu ya kutumia. Kwa nini ingekuwa bora kuwa na chaguzi? Kisha mngeweza kusoma pamoja Musa 4:1–4 na kuzungumza kuhusu kwa nini Mungu anatutaka tuweze kuchagua kati ya mema na mabaya. Ni kwa jinsi gani, Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo hutusaidia kufanya chaguzi nzuri?
-
Wasaidie watoto wako wafikirie juu ya na wachore picha za chaguzi mzuri wanazoweza kufanya ili kumfuata Yesu Kristo. Au mngeweza kuimba pamoja wimbo kuhusu kufanya chaguzi sahihi, kama vile ““Choose the Right Way”” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,160–61). Mnaweza kuambiana nyinyi kwa nyinyi kuhusu wakati ambapo mlifanya uchaguzi mzuri, na muelezee kuhusu jinsi mlivyojihisi baadaye.
Anguko, na Robert T. Barrett
Ninaweza kusali kwa Baba wa Mbinguni.
-
Wakati Adamu na Hawa walipolazimika kuondoka kwenye Bustani ya Edeni, hawangeweza kuwa na Baba wa Mbinguni tena. Soma Musa 5:4, 8 na watoto wako, na wasaidie watafute Adamu na Hawa walichofanya nini ili kuhisi kuwa karibu Naye na kumsikia Yeye. Je, ni mambo gani tunaweza kusema kwa Baba wa Mbinguni katika sala zetu?
Kwa ajili ya zaidi, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .
Katika Mfano wa Dhabihu ya Mzaliwa Pekee wa Baba, na Mike Malm (ona Musa 5:5–9)