“Januari 12–18. ‘Hapo Mwanzo Mungu Aliziumba Mbingu na Nchi’: Mwanzo 1–2; Musa 2–3; Ibrahimu 4–5,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)
“Januari 12–18. ‘Hapo Mwanzo Mungu Aliziumba Mbingu na Nchi’,” Njoo, Unifuate: 2026
Januari 12–18;“Hapo Mwanzo Mungu Aliziumba Mbingu na Nchi”
Mwanzo 1–2; Musa 2–3; Ibrahimu 4–5
Kwa sababu ulimwengu uliotuzunguka ni mzuri sana na wa kifahari, ni vigumu kufikiria kuwa dunia ilikuwa “wazi, na haina mtu,” na “utupu na yenye ukiwa” (Mwanzo 1:2; Ibrahimu 4:2). Kitu kimoja hadithi ya Uumbaji inatufundisha ni kuwa Mungu anaweza, baada ya muda, kufanya kitu kikubwa kutokana na kitu kisicho na umbile. Hilo ni la msaada kukumbukwa wakati maisha yanapoonekana kuwa ya vurugu. Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo ndio Waumbaji, na kazi Zao za ubunifu kwetu sisi hazijaisha. Wao wanaweza kufanya nuru ikaangaza katika nyakati za kiza katika maisha yetu. Wanaweza kujaza utupu wetu kwa maisha. Wanaweza kutubadilisha kuwa viumbe wa kiungu tuliokusudiwa kuwa. Hiyo ni kile inachomaanisha kuumbwa katika sura ya Mungu, kwa mfano Wake (ona Mwanzo 1:26). Tunao uwezekano wa kuwa kama Yeye: kuinuliwa, kutukuzwa, kimbingu.
Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Mwanzo, ona “Mwanzo” katika Kamusi ya Biblia.
Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani
Mwanzo 1:1–25; Musa 2:1–25; Ibrahimu 4:1–25
“Kwa njia ya Mwanangu wa Pekee niliviumba vitu hivi.”
Ingawa hatujui kila kitu kuhusu jinsi ulimwengu ulivyoumbwa, inavutia kutambua kile Mungu amechagua kufunua kuhusu Uumbaji. Mungu anakufundisha nini kuhusu hilo katika Mwanzo 1:1–25; Musa 2:1–25; na Ibrahimu 4:1–25? Kwa nini Yeye anataka wewe ujue mambo haya? Unapotafakari matukio haya, unaweza pia kufikiria kile yanachokufundisha kuhusu Baba wa Mbinguni, Yesu Kristo, ulimwengu, na wewe mwenyewe.
Ili kustawisha kujifunza kwako, fikiria kusoma mistari hii ukiwa nje miongoni mwa uumbaji wa Mungu au wakati ukisikiliza wimbo kama “All Creatures of Our God and King” (Nyimbo za Dini, na. 62). Ungeweza kupata picha za uumbaji Wake ambazo zinakusaidia kuhisi staha kwa Muumba. Fikiria kushiriki picha hizi, sambamba na ushuhuda wako, na wengine.
Ona pia Mafundisho na Maagano 101:32–34.
Bustani ya Edeni, na Grant Romney Clawson
Mwanzo 1:26–27; Musa 2:26–27; Ibrahimu 4:26–27
Nimeumbwa kwa mfano wa Mungu.
Unaposoma Mwanzo 1:26–27; Musa 2:26–27; na Ibrahimu 4:26–27, tafakari inamaanisha nini kuumbwa katika “mfano” wa Mungu au “sura,” mwanamume na mwanamke. Kwa nini ni muhimu kwako kujua kweli katika mistari hii? Kwa mfano, ni kwa jinsi gani kweli hizi zinaathiri jinsi unavyojiona mwenyewe, wengine, na Mungu? Ni kwa jinsi gani zinaweza kukusaidia wakati unapokuwa na hisia hasi kuhusu wewe mwenyewe?
Ili kukusaidia kufikiria kuhusu maswali haya, jaribu kukamilisha sentensi kama hii: “Kwa sababu najua nimeumbwa kwa mfano wa Mungu, ninachagua …” Kurejelea “Mwili wako ni mtakatifu” katika Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana: Mwongozo wa Kufanya Chaguzi (ukurasa 22–29) unaweza kusaidia. Fikiria kuchagua kitu utakachofanya ili kumwonyesha Mungu kwamba unajua mwili wako ni mtakatifu.
Katika video “God’s Greatest Creation” (Maktaba ya Injili), Rais Russell M. Nelson anatoa ushuhuda wa mwili wa kimiujiza wa binadamu. Unapotazama video hii, jiulize, “Ni kwa jinsi gani Baba wa Mbinguni ananitaka nihisi kuhusu mwili wangu?” Ni jinsi gani hii ni tofauti kutoka jumbe unazoweza kusikia kutoka kwa wengine?
God's Greatest Creation
Baadhi ya watu wanaweza kusema kwamba kuumbwa kwa mfano wa Mungu humaanisha kwamba mawazo yetu yote, hisia, na matamanio yameidhinishwa Naye na kwamba hatuhitaji kujiboresha (au hatuwezi) kujiboresha. Ungeweza kusema nini kwa hilo? Ni umaizi gani unaupata kutoka kwa Mosia 3:19 na Etheri 12:27?
Ona pia Russell M. Nelson, “Mwili Wako: Ni Zawadi Kubwa ya Kuitunza,” Liahona, Aug. 2019, 50–55.
Mwanzo 1:27–28; 2:18–25; Musa 3:18, 21–24; Ibrahimu 5:14–18
Ndoa kati ya mwanamume na mwanamke imeamriwa na Mungu.
“Adamu na Hawa waliunganishwa pamoja katika ndoa kwa muda na kwa milele yote kwa uwezo wa ukuhani usio na mwisho” (Russell M. Nelson, “Lessons from Eve,” Ensign, Nov. 1987, 87). Tafakari hili unaposoma Mwanzo 1:27–28; 2:18–25; Musa 3:18, 21–25; na Ibrahimu 5:14–19. Unawezaje kuchukulia ndoa kwa utakatifu ambao Mungu ameipa ndoa?
Ona pia 1 Wakorintho 11:11, “Familia Tangazo kwa Ulimwengu,”,” Maktaba ya Injili.
Mwanzo 1:28; Musa 2:28; Ibrahimu 4:28.
Nina jukumu la kutunza uumbaji wa Mungu.
Ni nini Mwanzo 1:28; Musa 2:28; na Ibrahimu 4:28 inapendekeza kuhusu jukumu letu kwa uumbaji wa Mungu? Ni nini Mafundisho na Maagano 59:16–21 na 104:13–18 inaongeza kwenye uelewa wako?
Ona pia Gérald Caussé, “Utumishi Wetu wa Kidunia,” Liahona, Nov. 2022, 57–59; Mada na Maswali, “Environmental Stewardship and Conservation,” Maktaba ya Injili.
Mwanzo 2:2–3; Musa 3:2–3; Ibrahimu 5:2–3
Mungu aliibariki na kuitakasa siku ya Sabato.
Mungu aliifanya Sabato kuwa siku takatifu, na Yeye anatutaka sisi tuishike kitakatifu. Unaposoma Mwanzo 2:2–3; Musa 3:2–3; na Ibrahimu 5:2–3, fikiria kuhusu kile kinachoifanya Sabato kuwa “imebarikiwa” kwako.
Ona pia Mafundisho na Maagano 59:9–13; “The Sabbath Is a Delight” (video), Maktaba ya Injili.
Highlight: The Sabbath Is a Delight
Kwa ajili ya zaidi, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .
Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto
Mwanzo 1:1–25; Musa 2:1–25; Ibrahimu 4:1–25
Yesu aliumba dunia.
-
Ni kwa jinsi gani unaweza kufanya kujifunza kuhusu Uumbaji kuwa ya kufurahisha kwa ajili ya watoto wako? Ungeweza kuwapeleka nje kutafuta aina ya vitu ambavyo vilifanywa wakati wa kila kipindi cha Uumbaji. Watoto wako wangeweza pia kuangalia picha za vitu ambavyo Yesu aliumba (ona “Uumbaji wa Dunia” katika Hadithi za Agano la Kale, 8–12). Kisha wewe na watoto wako mngeweza kuzungumza kuhusu jinsi unavyohisi kuhusu Yesu Kristo baada ya kusoma kuhusu Uumbaji.
-
Fikiria kuimba wimbo pamoja kuhusu ulimwengu wetu mzuri kama vile“My Heavenly Father Loves Me” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 228–29). Pengine watoto wako wangeweza kuongezea kwenye wimbo vitu vingine ambavyo Mungu ameviumba ambavyo vinawasaidia kuhisi upendo Wake.
Wasaidie watoto kuelezea ubunifu wao. Wakati unapowaalika watoto kuchora, kujenga, kupaka rangi, au kuandika kitu kinachohusika na kanuni ya injili, unawasaidia kuelewa vyema kanuni hiyo, na unawapa kitu halisi cha kukumbuka juu ya kile walichojifunza” (Kufundisha katika njia ya Mwokozi,32
Mwanzo 1:26–27; Musa 2:26–27; Ibrahimu 4:26–27
Niliumbwa kwa mfano wa Mungu.
-
Watoto wako wanaweza kukuza hali ya staha na heshima kwa miili yao wenyewe na ya wengine wanapojifunza kwamba sote tuliumbwa kwa mfano wa Mungu. Ili kuwasaidia kuelewa hii ina maana gani, ungeweza kuwaacha watoto wako waangalie sura zao kwenye kioo au picha wakati ukiwasomea Musa 2:26–27. Ungeweza pia kuwaonyesha jinsi ambavyo wanyama wachanga mara nyingi wako katika “sura” ya wazazi wao (ona picha katika muhtasari huu, kwa mfano). Hii inaweza kuongoza kwenye mazungumzo kuhusu kwa nini ni muhimu kwako kujua kwamba umeumbwa katika sura ya Baba yako wa Mbinguni.
-
Wewe na watoto wako mngeweza kufurahia kuchora mwili wa binadamu na kukata michoro katika chemsha bongo. Watoto wako wanapoweka chemsha bongo yao pamoja, wangeweza kuzungumza kuhusu njia wanazoweza kumwonyesha Baba wa Mbinguni kwamba wanashukuru kwa ajili ya miili yao.
Mwanzo 2:2–3; Musa 3:2–3; Ibrahimu 5:2–3
Siku ya Sabato ni takatifu.
-
Unaposoma Musa 3:2–3, na waombe watoto wako wasikilize kile ambacho Mungu alifanya siku ya saba. Wasaidie watoto wako wapate au wachore picha za vitu wanavyoweza kufanya siku ya Jumapili ili kuifanya kuwa siku takatifu na tofauti na siku zingine. Shiriki na kila mmoja kwa nini ni muhimu kwenu kuishika kitakatifu siku ya Sabato.
-
Wasaidie watoto wako kuigiza nafasi ambapo wanamuelezea rafiki kwa nini wanachagua kufanya mambo Jumapili ambavyo huonyesha heshima kwa Baba wa Mbinguni na Yesu. Pendekeza kwamba watumie Mwanzo 2:2–3 katika maelezo yao. Ni kwa jinsi gani kuishika siku ya Sabato kwa utakatifu kunaonesha upendo wetu kwa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo?
Kwa ajili ya zaidi, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki.