Njoo, Unifuate
Januari 5–11. “Hii Ni Kazi Yangu na Utukufu Wangu”: Musa 1; Ibrahimu 3


“Januari 5-11. ‘Hii Ni Kazi Yangu na Utukufu Wangu’: Musa 1; Ibrahimu 3,’” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)

“Januari 5–11. ‘Hii Ni Kazi Yangu na Utukufu Wangu’,” Njoo, Unifuate: 2026

nyota na nebula katika anga ya nje

Januari 5–11 “Hii ni Kazi Yangu na Utukufu Wangu”

Musa 1; Ibrahimu 3

Biblia inaanza kwa maneno “hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na nchi” (Mwanzo 1:1). Lakini kulikuwa na nini kabla ya “mwanzo” huu? Na kwa nini Mungu aliumba vyote hivi? Kupitia Nabii Joseph Smith, Bwana ametoa mwanga juu ya maswali haya.

Kwa mfano, Yeye ametupatia kumbukumbu ya ono ambamo Ibrahimu aliona maisha yetu kama roho “kabla ya ulimwengu kuwako” (ona Ibrahimu 3:22–28). Bwana pia ametupatia tafsiri yenye mwongozo wa kiungu au masahihisho ya milango sita ya kwanza ya kitabu cha Mwanzo, kinachoitwa kitabu cha Musa—ambacho hakianzi na “hapo mwanzo.” Badala yake, kinaanza na uzoefu ambao Musa aliupata wenye kutoa baadhi ya muktadha kwa ajili ya hadithi ya Uumbaji. Kwa pamoja, haya maandiko ya siku za mwisho ni mahali pazuri pa kuanzia ili kujifunza juu ya Agano la Kale kwa sababu yanajibu baadhi ya maswali ya msingi ambayo yanaweza kujenga usomaji wetu: Mungu ni Nani? Sisi ni kina nani? Je, Kazi ya Mungu ni ipi, na nafasi yetu ni ipi katika kazi hiyo? Milango ya ufunguzi ya kitabu cha Mwanzo inaweza kuonekana kama majibu ya Bwana kwa ombi la Musa: “Umrehemu mtumishi wako, Ee Mungu, na uniambie juu ya dunia hii, na wakazi wake, na pia mbingu” (Musa 1:36).

ikoni ya kujifunza

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Musa 1

ikoni ya seminari
Kama mtoto wa Mungu, ninayo hatima ya kiungu.

“Kama Bwana alikuwa anazungumza nawe moja kwa moja,” Rais Russell M. Nelson alifundisha, “jambo la kwanza ambalo Yeye angehakikisha unaelewa ni utambulisho wako wa kweli” (“Chaguzi za Milele” [ibada ya ulimwenguni kote kwa vijana wazima, Mei 2022], Maktaba ya Injili). Kinachofuata ni kwamba Shetani angejaribu kukuchanganya katika jambo hilo hilo. Tafuta mpangilio huu katika ujumbe wa Mungu kwa Musa katika Musa 1:4, 6 na katika jumbe za Shetani katika Musa 1:12. Unajifunza nini kutoka kwenye mistari hii kuhusu tofauti kati ya Mungu na Shetani?

Rais Nelson pia alifundisha, “Jinsi unavyofikiria kuhusu wewe ni nani hasa inaathiri karibu kila uamuzi ambao utaufanya” (“Chaguzi kwa milele”). Fikiria kutengeneza orodha ya chaguzi unazofanya kwa sababu ya utambulisho wako kama mtoto wa Mungu huja kabla ya majina mengine.

Ni mistari gani ya ziada au virai katika Musa 1 vinakusaidia kuelewa thamani yako ya kiungu? Ungeweza pia kusoma zaidi ujumbe wa Rais Nelson katika sehemu ya “Chaguzi kwa milele” yenye kichwa cha habari “Kwanza: Jua ukweli kuhusu wewe ni nani.” Je, unahisi kutiwa msukumo kufanya nini ili kufanya utambulisho wako kama mtoto wa Mungu kuwa kitambulisho chako muhimu zaidi?

Ona pia “Mimi Mwana wa Mungu,” Nyimbo za Kanisa (1985), na. 181; “Our True Identity” (video), Maktaba ya Injili; Mada na Maswali, “Watoto wa Mungu,” Maktaba ya Injili.

3:39

Our True Identity

mama, baba, na mtoto wakitabasamu

Musa 1:12–26

Kwa msaada wa Bwana, ninaweza kukinza majaribu.

Kama Musa 1 inavyoonyesha wazi, uzoefu wenye nguvu wa kiroho haumaanishi kamwe hatutajaribiwa tena. Kwa kweli, mojawapo ya mbinu za Shetani ni kutujaribu kutilia mashaka uzoefu huu. Unaposoma kuhusu majibu ya Musa kwa Shetani katika mistari ya 12–26, unajifunza nini ambacho kinaweza kukusaidia wewe kubaki mkweli kwa ushuhuda ambao umeupokea? Ni nini ambacho hatimaye kilimsaidia Musa kumshinda Shetani?

Somo moja kutokana na uzoefu wa Musa ni kwamba Shetani anatujaribu kwa kugushi ukweli na uwezo wa Mungu. Fikiria juu ya baadhi ya matoleo bandia ya vitu, kama vile mmea bandia au mwanasese mdoli. Unawezaje kujua kuwa ni bandia? Kisha fikiria vitu bandia ambavyo Shetani hutumia leo kukujaribu wewe. Unajifunza nini kutoka Musa 1:13–18 kuhusu jinsi ya kutambua na kukataa vitu vyake bandia? Ni kwa jinsi gani Bwana anaweza kukusaidia? (ona Musa 1:24–26).

Ona pia Mathayo 4:1–11; Gary E. Stevenson, “Usinidanganye,” Liahona, Nov. 2019, 93–96; “I Am a Son of God” (video), Maktaba ya Injili.

6:31

I Am a Son of God

Kujifunza nyumbani kunaweza kupangwa lakini pia hujitokeza pasipo kutarajia “Fursa za kufundisha katika familia mara nyingi hutokea katika nyakati zisizo rasmi, nyakati za kila siku—wakati kula chakula, kufanya kazi za nyumbani, kucheza michezo, [au] kusafiri” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 31). Kwa mfano, pamoja na kusoma kuhusu jinsi Musa alivyokinza Shetani katika Musa 1, ungeweza kutumia muda mchache wakati wa chakula cha jioni kuzungumza kama familia kuhusu jinsi ulivyokinza ushawishi wa adui.

Musa 1:27–39; Ibrahimu 3

Kazi ya Mungu na utukufu Wake ni kunisaidia mimi nipate uzima wa milele.

Baada ya kuona ono la uumbaji wa Mungu, Musa alifanya ombi kwa Bwana: “Niambie … kwa nini mambo haya yako hivi” (Musa 1:30). Je, ni kitu gani kinakuvutia kuhusu majibu ya Bwana katika Musa 1: 31–39? Kuna tofauti gani kati ya kutokufa na uzima wa milele? (ona Mada na Maswali, “Uzima wa Milele,” Maktaba ya Injili). Ni kwa jinsi gani Yesu Kristo husaidia kuleta vyote viwili? Ibrahimu pia alipata ono, lililoandikwa katika Ibrahimu 3. Je, unapata nini katika mstari wa 24–26 ambacho kingeweza kusaidia kujibu ombi la Musa?

Ibrahimu 3:22–28

Niliishi kama roho kabla sijazaliwa duniani.

Tunajua kidogo sana kuhusu maisha kabla ya kuja duniani. Lakini mengi ya kile tunachojua kinatokana na ono la Ibrahimu katika Ibrahimu 3:22–28. Unaposoma mistari hii, tengeneza orodha ya kweli unazozipata—ikijumuisha kweli kuhusu wewe mwenyewe na kuhusu Yesu Kristo. Kwa nini kweli hizi ni muhimu kwako? “Je! ni tofauti gani hizi zinaleta katika maisha yako?

Ona pia Mada na Maswali, “Maisha Kala ya Maisha ya Duniani,” Maktaba ya Injili.

Kwa ajili ya zaidi, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .

sehemu ya watoto ikon 01

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Musa 1:1–4, 6, 12

Mimi ni mtoto wa Mungu.

  • Baada ya kusoma pamoja ujumbe wa Mungu kwa Musa katika Musa 1:4, fikiria kuwaacha watoto wako waangalie kiakisi chao katika kioo na kujipatia ujumbe sawa na huo: “Mimi ni mtoto wa Mungu.” Kisha wangeweza kutoa ujumbe sawa na huo kwa kila mmoja: “Wewe ni mtoto wa Mungu.” Unaweza hata kupata picha za watu mbalimbali na waalike watoto wako waoneshe kwa kidole kila mmoja na kusema, “Huyu ni mtoto wa Mungu.” Shiriki na kila mmoja kwa nini una furaha kujua ninyi ni watoto wa Mungu. Ni kwa jinsi gani elimu hii inabadilisha jinsi unavyojitendea wewe mwenyewe na wengine?

  • Wewe na watoto wako mngeweza kulinganisha ujumbe wa Mungu na Musa katika Musa 1:4 na ujumbe wa Shetani katika mstari wa 12. Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto wako watofautishe kati ya jumbe za Mungu kwao na za Shetani?

Yehova akimtokea Musa

Musa Anamwona Yehova, na Joseph Brickey (utondoti)

Musa 1:6, 39

Baba yetu wa Mbinguni ana kazi ya kufanya kwa ajili yangu.

  • Unaposoma Musa 1:6 pamoja na watoto wako, unaweza kuzungumza nao kuhusu “kazi” ambayo Mungu alikuwa nayo kwa ajili ya Musa. Fikiria kutumia Kitabu cha Sanaa ya Injili, na. 13–16, au Hadithi za Agano la Kale, kurasa za 64–84, ili kuwasaidia watoto wako waone kile Musa alichotimiza kwa msaada wa Baba wa Mbinguni. Je, Ni kazi gani Mungu aliyo nayo ya kufanywa na sisi (ona, kwa mfano, Mafundisho na Maagano 11:20).

Musa 1:12–26

Naweza kukinzaa vishawishi vya Shetani.

  • Unapojifunza Musa 1:12–26 pamoja na watoto wako, wasaidie kugundua kitu ambacho Musa alifanya ili kumkinza Shetani (ona mstari wa 13, 15, 18, 20–22, 26). Inaweza kuwa ya kufurahisha kwao kuigiza mambo wanayoweza kufanya ili kukinza majaribu (kama vile kusali, kuondoka, au kuomba msaada).

Ibrahimu 3:22–28

Niliishi kama roho kabla sijazaliwa duniani.

  • Kujua juu ya maisha yetu kabla ya hapa duniani kunaweza kutia moyo watoto wako kufanya chaguzi kulingana na ukweli wa milele. Ili kuwasaidia kujifunza kuhusu hilo, ungeweza kuwapa baadhi ya maneno muhimu na virai vya kutafuta katika Ibrahimu 3:22–28, kama “kabla ya ulimwengu kuwako,” “roho,” “kufanya dunia,” na “kuthibitisha.” Mistari hii inatufundisha nini kuhusu kwa nini Baba wa Mbinguni alitutuma duniani?

  • Wimbo kama “I Will Follow God’s Plan” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 164–65) ungeweza kuimarisha kile Ibrahimu 3 anachofundisha. Pengine ungeweza kuwaalika watoto wako kuchora picha zinazoendana na maneno.

  • Wasaidie watoto wako wafikirie hali ambazo wanapaswa kuchagua ikiwa watafanya au hawatafanya jambo ambalo Mungu amewaagiza wao (ona Ibrahimu 3:25; ona pia Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana: Mwongozo wa Kufanya Chaguzi). Waache wao wafanye mazoezi au wajadili majibu yamkini ya hali hizo. Je, Mwokozi anawezaje kutusaidia wakati tunapofanya chaguzi mbaya?

Kwa ajili ya zaidi, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .

Musa akimfukuza Shetani

Musa Anamshinda Shetani, na Joseph Brickey

ukurasa wa shughuli za Msingi: Mimi ni mtoto wa Mungu