“Februari 2–8. ‘Bwana Aliwaita Watu Wake Sayuni’ Musa 7” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Nyumbani na Kanisani.: Agano la Kale 2026 (2026)
“Februari 2–8. ‘Bwana Aliwaita Watu Wake Sayuni’,” Njoo, Unifuate: 2026
Henoko Anaona Wakati wa Meridiani, na Jennifer Paget
Februali 2–8: “Bwana Aliwaita Watu Wake Sayuni”
Musa 7
Katika historia yote, watu wamekuwa wakijaribu kufanikisha kile Henoko na watu wake walichotimiza: kujenga jumuiya iliyo bora mahali ambapo hakuna umaskini wala vurugu. Kama watu wa Mungu, tunashiriki hamu hii. Tunaita kujenga Sayuni, na inajumuisha—ikiongezea kwenye kuwajali maskini na kukuza amani—kufanya maagano, kukaa pamoja katika haki, na kuwa na umoja na kila mtu na pamoja na Yesu Kristo, “mfalme wa Sayuni” (Musa 7:53). Ikiwa ulimwengu, jumuiya yako, au familia yako sio kile unachokitaka iwe, inasaidia kuuliza, Ni kwa jinsi gani Henoko na watu wake walifanya hivyo? Je, ni kwa jinsi gani wao walikuja kuwa “wa moyo mmoja na wazo moja” (Musa 7:18) licha ya ubishi unaowazunguka? Miongoni mwa utondoti mwingi Musa 7 inatufundisha kuhusu Sayuni, hasa yenye thamani zaidi kwa Watakatifu wa Siku za Mwisho inaweza kuwa hili: Sayuni sio mji tu—ni hali ya moyo na roho. Sayuni, kama Bwana alivyofundisha, ni “walio safi moyoni” (Mafundisho na Maagano 97:21). Hivyo pengine njia iliyo bora zaidi kuanza kujenga Sayuni ni kuanza katika mioyo yetu wenyewe na majumbani mwetu.
Mawazo kwa ajili ya Kujifunza na ya Nyumbani na Kanisani
Ninaweza kusaidia kujenga Sayuni.
Wakati Nabii Joseph Smith alipojifunza kwa mara ya kwanza kuhusu Henoko na Jiji Lake la Utakatifu, alipata msukumo wa kiungu. Yeye “alijua siku ilikuwa imefika ambapo Bwana angeianzisha tena Sayuni duniani” (Saints, 1:108–9), na akaanza jitihada ya maisha yote ya kujenga Sayuni. Kusoma Musa 7 kunaweza kukutia msukumo kuendelea na juhudi hiyo leo.
Unaweza kuanza kwa kuchunguza maswali “Sayuni ni nini?” na “Ni kwa jinsi gani ni tofauti na ulimwengu wote?” Fikiria kuorodhesha majibu yanayokujia unapojifunza Musa 7, hasa mstari wa 16–21, 27, 53, 62–69.
Majibu yako kwa maswali haya yanaweza kuweka wazi kwamba bado tuna kazi kubwa ya kufanya ili kujenga Sayuni. Kwa hiyo ni kwa jinsi gani tunafanya hivyo? Ingeweza kusaidia kufikiria kuhusu nyakati ulipohisi ulikuwa “wa moyo mmoja na wazo moja” na mtu fulani (Musa 7:18). Pengine ilikuwa katika kata, familia, au kikundi kazini au shuleni. Watu walifanya nini ili kujenga umoja wa haki?
Hapa kuna baadhi ya nyenzo zingine ambazo ungeweza kuchunguza ili kupata mawazo na mwongozo wa kiungu. Chagua moja au zaidi ya kujifunza, na kisha uandike kile unachohisi umetiwa msukumo kufanya ili kujenga Sayuni:
-
Wafilipi 2:1–4; 4 Nefi 1:15–18; Mafundisho na Maagano 97:21; 105:5.
-
Ulisses Soares, “Akina Kaka na Akina Dada katika Kristo,” Liahona, Nov. 2023, 70–73.
-
D. Todd Christofferson, “Wamoja katika Kristo,” Liahona, Mei 2023, 77–80.
Mungu anataka watu Wake kuwa “wa moyo mmoja na nia moja” (Musa 7:18).
Yesu Kristo ni Mfalme wa Sayuni.”.
Je, inamaanisha nini kwako kuwa na Yesu Kristo kama Mfalme? Tazama majina mengine ya Yesu Kristo katika mstari huu. Yanakufundisha nini wewe kuhusu Yeye? Unafikiri inamaanisha nini “yeyote aingiaye langoni na [kupanda] kwa njia ya [Yeye]”?
Ona pia “Njoo, Ewe Mfalme wa Wafalme,“ Nyimbo za Dini, na.29
Mungu hulia—na hufurahi—kwa ajili ya watoto Wake.
Baadhi ya watu humwona Mungu kama kiumbe wa mbali na asiyeathiriwa na yale yanayotokea kwetu. Henoko alipata mtazamo tofauti juu ya Mungu katika ono lililoandikwa katika Musa 7. Alijifunza nini kuhusu Mungu—na wewe unajifunza nini—katika mstari wa 28–40? Kwa nini unafikiri Henoko alishangaa kumwona Mungu akilia? Kwa nini ni muhimu kwako kujua kwamba Yeye anafanya hivyo?
Ono lilipoendelea, Henoko alilia pia. Lakini Mungu pia alishiriki naye sababu za kufurahi. Yatafute katika Musa 7:41–69. Unajifunza nini kutokana na ono la Henoko ambacho kinaweza kukusaidia “kuinua moyo wako, na kufurahi,” licha ya “uchungu” katika maisha yako (mstari wa 44)?
Ona pia Jeffrey R. Holland, “Fahari ya Mungu,” Liahona, Nov. 2003. 70–73.
Yesu Kristo atakuja tena katika siku za mwisho.
Ono la Henoko, hasa kile kilichoandikwa katika Musa 7:59–67, ni moja ya unabii wa kwanza wa historia ya Ujio wa Pili wa Mwokozi. Ni nini kinachokuvutia kuhusu jinsi mistari hii inavyoelezea siku za mwisho? Kwa mfano, fikiria jinsi unavyohisi unabii kutoka mstari wa 62 unavyotimizwa. Je, virai hivi vinakufundisha nini wewe kuhusu kazi ya Mungu katika siku hizi za mwisho?
Ona pia Henry B. Eyring, “Akina Dada katika Sayuni,” Liahona, Nov. 2020, 67–69.
Kwa ajili ya zaidi, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .
Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto
Mungu anatutaka tuwe “wa moyo mmoja na wazo moja”?
-
Ili kuwasaidia watoto wako wajifunze kuhusu Henoko na Sayuni, ungeweza kutumia “Henoko Nabii” katika Hadithi za Agano la Kale (19–21) au mstari wa pili wa “Follow the Prophet” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 110–11). Kisha ungeweza kuwaomba watoto wako wakusaidie kusimulia tena hadithi hiyo kwa maneno yao wenyewe. Picha za Henoko katika muhtasari huu zinaweza kusaidia.
-
Hii ni njia mojawapo ya kuwasaidia watoto wako waelewe inamaanisha nini kuwa wa “moyo mmoja na wazo moja” (Musa 7:18): Tengeneza moyo wa karatasi na ukate vipande vipande, vya kutosha kwa kila mtoto kupata kimoja. Waache waandike majina yao kwenye kipande chao na wafanye kazi pamoja kuweka moyo pamoja. Wanapofanya hivyo, ungeweza kuzungumza kuhusu vitu unavyovipenda kuhusu kila mtoto.
-
Waombe watoto wengine kuhesabu mara ngapi neno “Sayuni” limeonekana katika Musa 7:18–21, 62–63, 68–69. Kila mara wanapopata neno hilo, wasaidie kugundua kile mstari unachosema kuhusu Sayuni (ona pia Mwongozo wa Maandiko, “Sayuni,” Maktaba ya Injili). Ni kwa jinsi gani tunaweza kuwa zaidi kama watu walioelezewa katika mistari hii?
Himiza kujifunza maandiko binafsi kila siku Iwe unaifundisha familia yako nyumbani au darasani Jumapili, mojawapo ya njia bora unazoweza kuwasaidia wengine kujenga imani ya kudumu katika Yesu Kristo ni kuwasaidia kujenga tabia ya kutafuta uzoefu binafsi na maandiko. Shiriki uzoefu ulionao kwenye maandiko, na watie moyo wanafamilia au washiriki wa darasa kushiriki uzoefu wao. Tunaposikia kuhusu jinsi kusoma maandiko kunavyowabariki wengine, mara nyingi tunapata msukumo wa kutafuta baraka hizo hizo kutoka kwa Bwana. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25.)
Baba wa Mbinguni ananitaka nichague kumfuata Yeye
-
Ili kutambulisha Musa 7:32–33 kwa watoto wako, unaweza kuzungumza nao kuhusu chaguo walilopaswa kufanya hivi karibuni. Kisha mngeweza kusoma mistari pamoja ili kupata Baba wa Mbinguni anataka tuchague nini . Ni chaguzi gani tunaweza kufanya ili kuonyesha kwamba tunamchagua Yeye? Pengine watoto wako wangeweza kufanya zamu kuigiza mojawapo ya chaguzi hizi wakati wengine wakibahatisha kitendo kinawakilisha nini.
Yesu atakuja tena duniani.
-
Katika Musa 7:59, Henoko anamwuliza Bwana swali. Waalike watoto wako walitafute, na kisha waombe watafute jibu katika mstari wa 60. Ungeweza pia kuzungumza nao kuhusu wakati ambapo walikuwa wanatarajia mtu fulani arudi nyumbani. Waulize jinsi walivyohisi na kile walichofanya ili kujiandaa. Ni kwa jinsi gani tunaweza kujiandaa kwa ajili ya kurudi kwa Yesu?
-
Fikiria kuonyesha picha za nyakati wakati Mwokozi alipowatokea watu (ona Kitabu cha Sanaa ya Injili,, na. 60, 82, 83, na 84). Je, Watu wanafanya nini kwenye picha? Je, Watu wangeweza kuhisi vipi walipokutana na Yesu? Mngeweza pia kuimba wimbo kuhusu Ujio wa Pili wa Mwokozi, kama vile “When He Comes Again” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,, 82–83), na waulize watoto vile wanafikiri itakavyokuwa wakati Yesu atakaporudi tena. Acha watoto washiriki jinsi wanavyohisi juu ya kumwona Yesu wakati atakapokuja.tena.
Kwa ajili ya zaidi, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .