Njoo, Unifuate
Desemba 7–13. “Utakatifu kwa Bwana”: Hagai 1–2; Zekaria 1–4; 7–14


“Desemba 7–13. ‘Utakatifu kwa Bwana”: Hagai 1–2; Zakaria 1–4; 7–14,’ Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)

“Desemba 7–13. ‘Utakatifu kwa Bwana,’” Njoo, Unifuate: Agano la Kale 2026

Hekalu la Laie Hawaii chini ya anga la mawingu

Hekalu la Laie Hawaii

Desemba 7–13: “Utakatifu kwa Bwana”

Hagai 1–2; Zekaria 1–4; 7–14

Baada ya utumwa wa miongo kadhaa, kundi la Waisraeli, labda wakiwemo manabii Hagai na Zekaria, waliruhusiwa kurudi Yerusalemu. Baadhi katika kundi hili walikumbuka jinsi Yerusalemu ilivyokuwa kabla ya kuharibiwa. Kwa wale ambao walishangaa kama ingefanana tena na “nyumba ya Bwana katika utukufu wake wa kwanza” (Hagai 2:3), Hagai alisema maneno ya Bwana ya kutia moyo: “Kuweni hodari, enyi watu wote wa nchi, asema Bwana. na fanya kazi: kwa maana mimi niko pamoja nanyi, … msiogope.” “Nitaijaza nyumba hii na utukufu, … na mahali hapa nitatoa amani” (Hagai 2:4–5, 7, 9).

Lakini haikuwa tu hekalu takatifu ambalo lilihitaji kujengwa upya. Kwa njia nyingi, watu wa Mungu walikuwa magofu kiroho. Na kujenga watu watakatifu huchukua zaidi ya kukata mawe na kuyapanga ili kujenga nyumba takatifu. Inamaanisha maandishi “Utakatifu kwa Bwana” lazima yachongwe si tu kwenye ukuta wa hekalu, au hata kwenye “kengele za farasi” na “kila chungu katika Yerusalemu” (Zakaria 14:20–21). Lazima pia yachongwe kwenye kila moyo.

Kwa ajili ya muhtasari wa vitabu vya Hagai na Zakaria, ona “Hagai” na “Zakaria” katika Kamusi ya Biblia.

ikoni ya kujifunza

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Hagai 1; 2:1–9

ikoni ya seminari
“Zitafakarini njia zenu.”

Kulikuwa na mambo mengi muhimu ya kufanya ili kujenga upya Yerusalemu. Lakini baada ya takribani miaka 15 kupita tangu kurudi kwa Waisraeli, Bwana hakufurahishwa kwamba ujenzi wa hekalu haukupewa kipaumbele cha juu (ona Hagai 1:2–5; ona pia Ezra 4:24). Unaposoma Hagai 1; 2:1–9, zingatia maswali kama haya:

  • Ni matokeo gani waliyokumbana nayo Waisraeli kwa sababu walikuwa hawajamaliza hekalu?

  • Ni baraka gani Bwana aliwaahidi ikiwa watamaliza ujenzi wa nyumba Yake?

  • Je, ujumbe wa Bwana kwako ni upi katika Hagai 1:5–7? Unawezaje kuwianisha vipaumbele vyako na vya Bwana? Ni lini umebarikiwa kwa kumweka Mungu kwanza katika maisha yako?

Watakatifu wa mwanzo wa Siku za Mwisho alikabiliana na hali kama hiyo ya Waisraeli katika siku za Hagai (ona Mafundisho na Maagano 95). Unajifunza nini kutoka kwenye mifano hii miwili kuhusu hisia za Bwana kuhusu mahekalu?

Ona pia Dale G. Renlund, “Yesu Kristo Ndiye Hazina,” Liahona, Nov. 2023, 96–99; Terence M. Vinson, “Wafuasi wa Kweli wa Mwokozi,” Liahona, Nov. 2019, 9–11; “We Love Thy House, O God,” Nyimbo za Dini, na. 247; “Provo City Center Temple Completed” (video), ChurchofJesusChrist.org.

7:17

Provo City Center Temple Completed

Zekaria 1–3; 7–8; 14

Bwana anaweza kunifanya mtakatifu.

Kwa maoni yako, ni nini thamani ya kuwa na “utakatifu kwa Bwana’ uliochongwa kwenye vitu vya kila siku kama vile vilivyotajwa katika Zekaria 14:20? (ona pia Kutoka 28:36–38). Nini thamani ya kuwa yamechongwa kwenye mahekalu leo? Kirai hiki kina maanisha nini kwako? Ni kwa jinsi gani unaweza kufanya utakatifu kuwa sehemu ya maisha yako ya kila siku? Tafakari maswali haya unaposoma mialiko ya Bwana kwa watu Wake kuwa watakatifu zaidi katika Zekaria 1:1–6; 3:1–7; 7:8–10; 8:16–17.

Ungeweza pia kusoma Zekaria 2:10–11; 8:1–8; 14:9–11, 20–21 ili kujifunza jinsi maisha yatakavyokuwa katika siku zijazo wakati sisi sote tutaishi na Bwana katika hali ya utakatifu. Ni nini kinakuvutia kuhusu ono la Zekaria kuhusu siku zijazo za Yerusalemu? Je! unapata nini hapo ambacho ungependa kukiona katika jumuiya yako? Je, kwa jinsi gani Bwana anaweza kutuandaa tuishi katika hali ambazo Zekaria alielezea?

Yesu akiingia Yerusalemu kwa punda

“Tazama, mfalme wako anakuja kwako; Ni mwenye haki, naye ana wokovu; Ni mnyenyekevu, amepanda punda,” (Zekaria 9:9). Kuingia kwa Shangwe, na Harry Anderson

Zekaria 9:9–11; 11:12–13; 12:10; 13:6–7; 14:1–9

Yesu Kristo ndiye Masiya aliyeahidiwa.

Maandishi kadhaa ya Zekaria yanaelekeza kwa huduma ya duniani ya Yesu Kristo na pia Ujio Wake wa Pili Hapa chini kuna baadhi ya unabii wa Zekaria, pamoja na maandiko kuhusu kutimizwa kwake. Unaposoma vifungu hivi, jiulize mwenyewe, “Hili linanifundisha nini kuhusu Mwokozi?

  • Zekaria 9:9–11 (ona Mathayo 21:1–11; 1 Petro 3:18–19)

  • Zekaria 11:12–13 (ona Mathayo 26:14–16; 27:1–7)

  • Zekaria 12:10 (ona Yohana 19:37; Ufunuo 1:7)

  • Zekaria 13:6–7; 14:1–9 (ona Mathayo 26:31; Mafundisho na Maagano 45:47–53)

Unafikiri ingekuwaje kuwa miongoni mwa watu wanao mkaribisha Yesu Yerusalemu kama ilivyoelezwa katika Zekaria 9:9–11? Ni kwa jinsi gani unaweza kumkaribisha Yeye katika maisha yako, majumbani mwenu, na jumuiya yako?

Ona pia Mwongozo wa Maandiko, “Masiya,” Gospel Library; “The Lord’s Triumphal Entry into Jerusalem” (video), Gospel Library; Ronald A. Rasband, “Hosana kwa Mungu Aliye Juu Sana,” Liahona, Mei 2023, 108–12.

1:22

The Lord's Triumphal Entry into Jerusalem

Kwa ziada, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .

ikoni ya sehemu ya watoto

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Hagai 1:2–8

“Zitafakarini njia zenu.”

  • Unaposoma sehemu za Hagai 1:2–5 pamoja na watoto wako, wasaidie kujua ni kwa nini Bwana hakupendezwa na watu. Pengine watoto wako wangeweza kuchagua kirai kutoka mstari wa 6 na kuchora picha yake. Wangeweza kuonyeshana wao kwa wao na kukisia ni kirai gani kila mchoro unawakilisha. Tunapotumia muda kwa vitu vingine zaidi ya vile Bwana anavyotaka, hiyo ni vipi kama kula lakini kutoshiba? Mngeweza kuzungumza kuhusu jinsi mnavyoweza kutenga muda kwa ajili ya vitu ambavyo ni muhimu kwa Bwana.

  • Ungeweza pia kusoma mstari wa 8 kwa watoto, na waalike wajifanye “kupanda mlimani,” “kuleta miti,” na “kuijenga nyumba [ya Bwana].” Watoto wako wangetengeneza orodha ya mambo wanayofanya katika siku ya kawaida, ikiwa ni pamoja na mambo ambayo Bwana aliwaomba wafanye. Waombe watoto wako “wazitafakari njia [zao]” kwa kuzungushia kile ambacho Bwana angeweza kusema ni mambo muhimu kwenye orodha yao.

Ufundishaji unaolenga nyumbani. Rais Russell M. Nelson amefundisha kwamba nyumbani panapaswa kuwa “kitovu cha kujifunza injili” (“Kuwa Mtakatifu wa Siku za Mwisho wa Mfano,” Liahona, Nov. 2018, 113). Familia yako inapojifunza ushauri wa Hagai wa “zitafakarini njia zenu,” mnaweza kuzungumza kuhusu jinsi ya kumweka Mungu kwanza katika maisha ya familia yako.

Zekaria 3:1–7

Kufanya na kushika maagano kunaweza kunisaidia kuwa zaidi kama Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

  • Katika ono, Zekaria alimwona kuhani mkuu, ambaye alikuwa “amevaa nguo chafu sana” (Zekaria 3:3). Malaika alimpa nguo safi. Ungeweza kuwasaidia watoto wako wagundue kweli muhimu kwa kusoma pamoja Zekaria 3:1–7 na kuzungumza kuhusu kile nguo chafu na nguo safi zinaweza kuwakilisha. Ni kwa jinsi gani tunakuwa wasafi kutokana na dhambi zetu, hata baada ya kubatizwa? Ni kwa jinsi gani agano letu la ubatizo hutusaidia “kwenda katika njia za [Bwana]”?

  • Wewe na watoto wako mngeweza kuangalia picha ya ubatizo, kama ile iliyoko katika muhtasari huu. Kwa nini tunavaa nguo nyeupe kwenye ubatizo wetu? Mngeweza pia kuimba wimbo kuhusu ubatizo kama vile “When I Am Baptized” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 103); wimbo huu unafundisha nini kuhusu kwa nini Bwana anataka sisi tubatizwe?

baba akimbatiza binti yake ndani ya mto

Zekaria 9:9–11; 11:12; 13:6–7

Yesu Kristo ndiye Masiya aliyeahidiwa.

  • Watoto wako wangeweza kupenda kupiga taswira ya tukio lililotabiriwa katika Zekaria 9:9, wakati Yesu alipokuja Yerusalemu katika wiki ya mwisho ya maisha Yake duniani. Ili kusaidia katika hili, waoneshe wao picha ya tukio hilo, kama ile iliyoko katika muhtasari huu. Ungeweza pia kushiriki nao “Mwokozi Anakwenda Yerusalemu” (katika Hadithi za Agano Jipya, 110–12). Watoto wako wangeweza kuwaonesha watu katika picha ambao “wanafurahia sana.” Mfalme ni nani katika Zekaria 9:9? Kwa nini tunamshukuru Yeye?

    1:35

    Chapter 44: The Savior Goes to Jerusalem

  • Fikiria kuwasaidia watoto wako walinganishe unabii kutoka kwa Zekaria na mistari ya Agano Jipya linaloelezea kutimizwa kwake. Hapa kuna baadhi ya mifano: Zekaria 9:9 na Mathayo 21:5–9; Zekaria 9:11 na 1 Petro 3:18–19; Zekaria 11:12 na Mathayo 26:14–16; Zekaria 13:7 na Mathayo 26:31. Je, tunajifunza nini kuhusu Mwokozi kutoka kwenye mistari hii?

Kwa ajili ya zaidi, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .

Ishara kwenye mahekalu mengi ukisomeka “Utakatifu kwa Bwana” na “Nyumba ya Bwana” katika lugha tofauti

“Utakatifu kwa Bwana” uonekana kwenye kila hekalu.

Ukurasa wa shughuli wa Msingi: Yesu Kristo anaweza kufanya roho yangu kuwa safi