“Novemba 2–8. ‘Nami Nitatia Roho Mpya ndani Yenu’: Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)
“Novemba 2–8. ‘Nami Nitatia Roho Mpya ndani Yenu,’” Njoo, Unifuate: Agano la Kale 2026
Novemba 2–8:“Nami Nitatia Roho Mpya ndani Yenu”
Ezekieli 1–3; 33–34; 36–37; 47
Ezekieli alikuwa nabii uhamishoni. Pamoja na Waisraeli wengine, alikuwa ametekwa na kupelekwa Babeli. Huko Yerusalemu, Ezekieli angekuwa kuhani akitumikia hekaluni. Huko Babeli, alikuwa miongoni mwa “wale wafungwa,” na “alikaa pale walipoketi” (Ezekieli 3:15), mamia ya maili kutoka hekaluni na akiwa na tumaini dogo la kurudi kwenye nyumba pendwa ya Mungu. Ndipo siku moja Ezekieli akapata ono. Aliuona “utukufu wa Bwana” (Ezekieli 1:28)—sio katika hekalu la Yerusalemu lakini huko Babeli miongoni mwa waliohamishwa. Uovu huko Yerusalemu, alijifunza, ulikuwa mkubwa sana kwamba uwepo wa Mungu haukuwepo tena pale (ona Ezekieli 8–11; 33:21).
Na bado kuna kitu chenye matumaini kuhusu ujumbe wa Ezekieli. Licha ya jinsi watu wa agano walivyokuwa wameanguka, Mungu hakuwa amewaacha kabisa. Kama “wangesikia neno la Bwana” (Ezekieli 37:4), kile kilichokuwa kimekufa kingeweza kufufuliwa. “Moyo wao wa jiwe” ungeweza kubadilishwa kwa “moyo mpya” (Ezekieli 36:26). Na katika siku za baadaye, Bwana angeanzisha hekalu jipya na Yerusalemu mpya, “na jina la mji huo tangu siku hiyo litakuwa hili, Bwana yupo hapa” (Ezekieli 48:35).
Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Ezekieli, ona “Ezekieli” katika Kamusi ya Biblia.
Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani
Ezekieli 3; 34
Bwana ananialika kuwalisha kondoo Wake.
Katika Ezekieli 3 na 34, Bwana anawataja viongozi wa watu Wake kama walinzi na wachungaji wa kondoo. Unaposoma sura hizi, fikiria majina haya yanapendekeza nini kuhusu kile inachomaanisha kuwa kiongozi.
Je, ni “kondoo” gani ambao Bwana anataka wewe uwalishe? Unapata nini katika Ezekieli 34 ambacho kinaweza kumsaidia mtu anayejiandaa kutumikia misheni, kulea watoto, au kutimiza jukumu la kuhudumu? Je, ni kwa jinsi gani unaweza kufuata mfano aliouweka Mwokozi kama mchungaji wetu? (ona mstari wa 11–31).
Unaweza pia kutafakari ishara unazopata katika sura hii. Kwa mfano, ni nini kingeweza kuwakilisha “malisho mema” na “zizi jema” katika mstari wa 14? Ni nini tofauti kati ya kondoo “aliyepotea” na yule “aliyefukuzwa”? (mstari wa 16). Ni ishara gani zingine ambazo unaziona?
Ona pia Yohana 21:15–17; Gerrit W. Gong, “Kuhudumu,” Liahona, Mei 2023, 16–19.
Ezekieli 33:10–19.
Bwana anataka kusamehe.
“Ikiwa dhambi zetu … ziko juu yetu,” Waisraeli waliofungwa walijiuliza, “jinsi gani tunapaswa kuishi?” (Ezekieli 33:10). Katika kujibu, Bwana aliwafundisha kuhusu toba na msamaha. Maswali haya yangeweza kukusaidia utafakari kile ambacho Yeye alifundisha:
-
Unafikiri inamaanisha nini “kuamini haki [yako] mwenyewe”? (ona Ezekieli 33:12–13).
-
Je, unaweza kusema nini kwa mtu ambaye anahisi kwamba watu walioelezewa katika Ezekieli 33:12–19 hawatendewi haki? (ona pia Mathayo 21:28–31; Luka 18:9–11).
-
Unapata nini katika mistari hii ambacho kinakusaidia kuelewa maana ya kutubu? Je, ni utambuzi gani wa ziada unaupata katika Ezekieli 36:26–27 na Alma 7:14–16?
Ezekieli 37
Bwana anawakusanya watu Wake na kuwapa maisha mapya.
Kukusanyika kwa Israeli kumeonyeshwa katika Ezekieli 37 kupitia ishara mbili. Unaposoma juu ya ile ya kwanza—mifupa iliyokufa ikifufuliwa ((ona mstari wa 1–14)—tafakari kile kinachopendekezwa kuhusu kukusanya Israeli pande zote mbili za pazia (ona pia Ezekieli 36:24–30). Fikiria maswali kama haya:
-
Bwana anajaribu kutimiza nini kupitia kukusanyika kwa Israeli?
-
Je, Yeye anatimizaje hilo?
Ungeweza kujiuliza maswali haya haya unaposoma kuhusu ishara ya pili, katika mstari wa 15–28. Ishara ya pili inajumuisha vijiti viwili, ambavyo wasomi wengi wanatafsiri kama mbao za miti za kuandikia zilizounganishwa na bawaba. Fimbo ya Yuda inaweza kuwakilisha Biblia (kwa kuwa sehemu kubwa ya Biblia iliandikwa na uzao wa Yuda), na fimbo ya Yusufu inaweza kuwakilisha Kitabu cha Mormoni (kwa kuwa familia ya Lehi walikuwa wa uzao wa Yusufu wa Misri). Kwa kuzingatia hilo, mistari hii inakufundisha nini kuhusu jukumu la maandiko katika kukusanyika kwa Israeli?
Fikiria kuhusu jinsi ambavyo Biblia na Kitabu cha Mormoni vimefanya kazi pamoja katika maisha yako—kipekee, katika kukusaidia wewe kuja kwa Kristo. Ni vifungu gani vimekuwa vyenye maana maalumu kwako?
Ona pia 2 Nefi 3:11–13; 29:14; “Israeli, Mnaitwa,” Nyimbo za Dini, na. 7; Mada na Maswali, “Biblia,” “Kitabu cha Mormoni,” Maktaba ya Injili; “The Book of Mormon Gathers Scattered Israel” (video), Maktaba ya Injili.
The Book of Mormon Gathers Scattered Israel
Katika ono, Ezekieli aliona mto ukitiririka kutoka kwenye hekalu na kuponya Bahari ya Chumvi.
Ezekieli 47:1–12.
Ninaweza kupata uponyaji wa kiroho katika nyumba ya Bwana.
Unaposoma Ezekieli 47:1–12, ingeweza kusaidia kujua kwamba Bahari ya Chumvi ina chumvi nyingi sana kiasi kwamba samaki na mimea haiwezi kuishi ndani yake. Ni nini kinachokuvutia kuhusu maji yaliyoelezewa katika mstari wa 1–12? (ona pia Ufunuo 22:1). Je, maji haya yangeweza kuashiria nini? Je, miti iliyoelezewa katika mstari wa 12 ingeweza kuwakilisha nini?
Ujumbe wa Mzee Dale G. Renlund “Historia ya Familia na Kazi ya Hekaluni: Kuunganishwa na Uponyaji” unaongeza nini kwenye uelewa wako? (ona Liahona, Mei 2018, 47–48). Tafakari jinsi ulivyopata uzima wa kiroho na uponyaji kwa sababu ya hekalu.
Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto
Ezekieli 3:17; 33:1–5
Manabii ni kama walinzi ambao hutuonya juu ya hatari.
-
Watoto wadogo wangeweza kufurahia kufanya vitendo vinavyoendana na Ezekieli 3:17. Kwa mfano, wanaweza kuonesha kwa kidole macho yao, masikio, na mdomo wakati unaposoma maneno “mlinzi,” “sikia,” na “mdomo.” Wangeweza pia kwenda matembezi ya masafa marefu mashambani—nje au kuzunguka chumba tu. Wanapotembea, waonye kuhusu vitu kwenye njia, kama vile mito ya kuvuka kwa kuruka juu, matawi ya kukwepwa, au wanyama wa kuwaepuka (halisi au kujifanya). Hii inaweza kutuongoza kwenye mazungumzo kuhusu jinsi nabii wa Bwana anavyotuonya juu ya hatari ambazo hatuwezi kuziona.
-
Hapa kuna njia nyingine ya kuonyesha Ezekieli 3:17; 33:1–5. Mmoja wa watoto wako angeweza kujifanya kuwa “mlinzi” kwa kuangalia nje ya dirisha na kumwambia kila mtu mwingine kile kinachotokea nje. Pia mngeweza kutazama video “Defenders of the Faith” (ChurchofJesusChrist.org). Ni kwa jinsi gani nabii wetu aliye hai ni kama mlinzi kwetu?
4:17Watchman on the Tower
Nabii Ezekieli, na Lyle Beddes
Ezekieli 37:15–23
Biblia na Kitabu cha Mormoni husaidia “kutukusanya” sisi kwa Yesu Kristo.
-
Baada ya kusoma Ezekieli 37:15–23 pamoja, wewe na watoto wako mngeweza kupata vijiti viwili na kuandika kwenye kijiti kimoja Kwa Yuda (Biblia) na kingine Kwa Yusufu (Kitabu cha Mormoni). Kisha wangeweza kushiriki hadithi au maandiko kutoka kwenye Biblia na Kitabu cha Mormoni ambayo yanawasaidia kujisikia karibu na Mwokozi na kuwa “watu [Wake]” (mstari wa 23). Kwa nini ni vizuri kuwa na vitabu hivi viwili vya maandiko?
Usijaribu kumaliza kila kitu. Unaweza usiweze kuvumbua kila ukweli katika Ezekieli na watoto wako. Kwa maombi fikiria kile wanachohitaji kuelewa, na tafuta mwongozo wa kiroho ili kuamua nini cha kufokasi. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 17.)
Ezekieli 47:1–12.
Mioyo yetu na familia zetu zinaweza kupata uponyaji katika nyumba ya Bwana.
-
Ezekieli 47 inaelezea ono la Ezekieli la maji yanayotiririka kutoka hekaluni na kuponya Bahari ya Chumvi—bahari yenye chumvi sana hata kwamba samaki na mimea hawawezi kuishi ndani yake. Pengine watoto wako wangeweza kuchora kitu kimoja au viwili kutoka kwenye ono, kama hekalu, mto, jangwa, Bahari ya Chumvi, samaki wengi, au mti uzaao matunda. Kisha, mnaposoma mstari wa 1–12 pamoja, wangeweza kushiriki mchoro wao wakati kitu hicho kinapotajwa. Ni baraka gani zilikuja kutokana na mtoni huo katika ono hili? Wasaidie watoto kuona jinsi baraka hizi zinavyofanana na baraka ambazo Mwokozi anatoa kwa wale wanaoshika maagano ya hekaluni. Video “And the River Will Grow” (Gospel Library) inaweza kusaidia.
3:43And the River Will Grow
-
Mngeweza kuimba pamoja wimbo unaoelezea baraka za hekaluni, kama vile “Families Can Be Together Forever” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,188). Wimbo huu unafundisha nini kuhusu jinsi Bwana anavyotubariki katika nyumba Yake takatifu?
Kwa ziada, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .