Njoo, Unifuate
Julai 13–19. “Alimtumaini Bwana Mungu wa Israeli”: 2 Wafalme 16–25


“Julai 13–19. ‘Alimtumaini Bwana Mungu wa Israeli’: 2 Wafalme 16–25,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Nyumbani na Kanisani: Agano la Kale 2026 (2026)

“Julai 13–19. ‘Alimtumaini Bwana Mungu wa Israeli,’” Njoo, Unifuate: Agano la Kale 2026

kundi kubwa la Wayahudi wakisafiri kwenda uhamishoni Babeli

Kutoroka kwa Wafungwa, na James Jacques Joseph Tissot na wengine

“Alimtumaini Bwana, Mungu wa Israeli”

2 Wafalme 16–25

Licha ya huduma yenye nguvu ya nabii Elisha, watu wa Ufalme wa Kaskazini wa Israeli hawakutubu. Mwishowe Himaya ya Ashuru ilishinda na kuyatawanya makabila kumi ya Israeli. Wakati huo huo, Ufalme wa Kusini wa Yuda ulikuwa hauendelei vizuri sana; kuabudu sanamu kulikuwa kumekithiri huko pia.

Katikati ya uozo wote huu wa kiroho, maandiko yanataja wafalme wawili wa Yuda ambao, kwa muda, waliwageuza watu wao kwa Bwana. Mmoja alikuwa Hezekia. Wakati wa utawala wake, Waashuri walitwaa sehemu kubwa ya Yuda. Ila Hezekia na watu wake walionyesha imani katika Bwana, aliyeikomboa Yerusalemu katika njia ya kimuujiza. Baadae, baada ya kipindi kingine cha ukengeufu, Yosia akawa mfalme. Akishawishiwa kwa sehemu na ugunduzi mpya wa kitabu cha sheria ya Musa, Yosia alileta mabadiliko yaliyoamsha maisha ya kidini ya wengi wa watu wake.

Kama Israeli na Yuda, sisi wote tunafanya chaguzi nzuri na mabaya. Tunapohisi kwamba maisha yetu yanahitaji mabadiliko fulani, tunaweza kupata hamasa kutoka sehemu hizi mbili angavu katika miaka ya giza ya historia ya Yuda. Pengine mifano ya Hezekia na Yosia inaweza kutuvutia “kumwamini Bwana Mungu wetu” (2 Wafalme 18:22).

ikoni ya kujifunza

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

2 Wafalme 18–19

ikoni ya seminari
Ninaweza kubaki mkweli kwa Bwana wakati imani yangu inapopitiwa changamoto.

Wengi wetu tuna uzoefu ambao unaleta changamoto kwenye imani yetu. Kwa Hezekia na watu wake, moja wapo ya changamoto hizo zilikuja wakati jeshi la Waashuru lilipokaribia Yerusalemu. Unaposoma 2 Wafalme 18–19, fikiria kwamba uliishi Yerusalemu wakati wa nyakati hizo. Ni kwa jinsi gani ungeweza kuhisi, kwa mfano, kusikia dhihaka za Waashuru katika 2 Wafalme 18:28–37; 19:10–13? Wewe ungeweza kufanya nini ? Linganisha sababu za Waashuru kwa ajili ya Waisraeli kutomwamini Bwana na sababu ambazo Shetani hutupatia sisi kutilia shaka imani yetu leo. Unaweza pia kutofautisha sababu za Waashuru na sababu zako kwa nini wewe unamtumaini Bwana.

Unajifunza nini kutokana na kile Hezekia alichofanya katika hali hii? (ona 2 Wafalme 19:1–7, 14–19). Ni kwa jinsi gani Bwana alimjibu? (ona 2 Wafalme 19:35–37). Kwa nini unafikiri Hezekia alibaki mwaminifu? (ona 2 Wafalme 18:5–7). Tafakari jinsi Bwana amekuhimili wewe katika nyakati za changamoto. Je, unahisi kutiwa msukumo kufanya nini ili kuongeza kutumamini kwako Kwake?

Ujumbe wa Rais Jeffrey R. Holland “Usiogope: Amini Tu” (Liahona, Mei 2022, 34–36) ina ushauri wenye msaada kwa nyakati za hofu au shaka. Wimbo kama “Let Us All Press On” (Nyimbo za Dini, na. 243) ungeweza pia kuwa na jumbe za kutia moyo. Unapata nini katika nyenzo hizi ambacho kinaweza kukusaidia?

Ona pia 2 Mambo ya Nyakati 31–32; 3 Nefi 3–4; Jörg Klebingat, “Ufuasi Jasiri katika Siku za Mwisho,” Liahona, Mei 2022, 107–10.

Tumia visaidizi vya kujifunza maandiko. Kanisa linatoa nyenzo nyingi ili kukusaidia kuelewa maandiko. Kwa mfano, katika Maktaba ya Injili unaweza kupata Mwongozo wa Maandiko, Mada na Maswali, na majarida ya Kanisa. Kwa kuongezea, unaposoma Agano la Kale, unaweza kupata muktadha na umaizi kwenye makala ya “Mawazo ya Kuweka Akilini” katika Njoo, Unifuate. Makala yenye kichwa cha habari “Jesus Will Say to All Israel, ‘Come Home’” ingeweza kusaidia kujifunza kwako 2 Wafalme 16–25.

familia ikisoma maandiko pamoja

2 Wafalme 19:20–37

Mambo yote yapo katika mikono ya Bwana.

Senakeribu, mfalme wa Ashuru, alikuwa na sababu nzuri ya kuamini kwamba jeshi lake lingeishinda Yerusalemu (ona 2 Wafalme 17; 18:33–34; 19:11–13). Lakini Bwana alikuwa na ujumbe kuhusu Senakeribu, uliotolewa kupitia nabii Isaya. Imeandikwa katika 2 Wafalme 19:20–34. Ni kweli zipi unazipata katika ujumbe wa Bwana ambazo zinakusaidia kuwa na imani katika Yeye na mpango Wake?

2 Wafalme 21–23

Maandiko yanaweza kugeuza moyo wangu kumwelekea Bwana.

Je, umewahi kuhisi kwamba ulikuwa umepungukiwa kitu fulani kiroho? Labda ulihisi kwamba uhusiano wako na Mungu ungeweza kuwa wenye nguvu. Ni nini kilikusaidia kugeuka na kurudi Kwake? Tafakari maswali haya unaposoma 2 Wafalme 21–23, ambayo yanaelezea jinsi Ufalme wa Yuda ulivyoangukia mbali na Bwana chini ya Mfalme Manase (ona 2 Wafalme 21) na jinsi Mfalme Josia alivyowasaidia watu kugeuka tena Kwake (ona 2 Wafalme 22–23). Ni kwa jinsi gani na kwa nini Yosia na watu wake walibadilika? (ona 2 Wafalme 22:8–11; 23:1–6, 21, 24).

Rais Spencer W. Kimball aliita hadithi ya Mfalme Yosia “mojawapo ya hadithi nzuri katika maandiko yote” (Teachings of Presidents of the Church: Spencer W. Kimball [2006], 62). Soma maneno ya Rais Kimball kuhusu Mfalme Yosia (ukurasa wa 62–64). Pengine unaweza kufikiria uzoefu wakati kifungu cha maandiko [kilipofanya] “kazi kwa nguvu” ndani yako. Unaweza kufanya nini ili kupokea uzoefu zaidi kama huo?

Ona pia Alma 31:5; “Josiah and the Book of the Law” (video), Maktaba ya Injili.

12:25

Josiah and the Book of the Law

2 Wafalme 23:1–25

Agano ni maamuzi ya roho­yote baina ya mimi na Mungu.

Ni nini kinachokuvutia kuhusu agano ambalo Yosia alifanya katika 2 Wafalme 23:3? Unapoendelea kusoma mlango wa 23, gundua kile Yosia alichokifanya ili kuonyesha msimamo wake thabiti kwa Bwana (ona pia picha mwishoni mwa muhtasari huu). Ni kwa jinsi gani unaweza kuonesha kujitolea kwako kwa dhati Kwake?

Kwa ajili ya zaidi, ona matoleo ya mwezi huu ya majarida ya Liahona na Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana. .

ikoni ya sehemu ya watoto

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

2 Wafalme 18:3–6; 19:14–19

Ninaweza kumtumainia Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

  • Katika 2 Wafalme 18:3, 5–6, wasaidie watoto wako wagundue kile kilichomfanya Hezekia kuwa mfalme mzuri. Kisha mnaposoma pamoja 2 Wafalme 19:14–19, wangeweza kugundua jinsi alivyoonyesha kwamba alimtumaini Bwana. Ungeweza kutazama picha ya Yesu na kuzungumza kuhusu kwa nini tunaweza kumtumainii Yeye. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuonesha kwamba tunamtumaini Bwana?

2 Wafalme 22:1–7

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanaweza kunitumaini.

  • Katika 2 Wafalme 22:1, wasaidie watoto wako wagundue jinsi mzee Yosia alikuwa na umri gani wakati alipokuwa mfalme. Tunajifunza nini kuhusu Yosia katika mstari wa 2? Fikiria shughuli ambayo ingeweza kuonesha kumfuata Bwana na kutokugeuka “upande wa kulia au kushoto.”

  • Wafanyakazi wanaoelezewa katika 2 Wafalme 22:3–7 waliatumaini hela za kujenga upya hekalu “kwa sababu walitenda kazi kwa uaminifu” (msitari wa 7). Baada ya kusoma mistari hii, wewe na watoto wako mngeweza kuzungumza kuhusu mambo ambayo umetumainiwa nayo. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuwa waaminifu kama wafanyakazi katika mistari hii?

mwandishi na Mfalme Yosia

Mwandishi akileta karatasi lililokunjwa la maandiko kwa Mfalme Yosia, na Robert T. BarrettY

2 Wafalme 22:8–11; 23:2–3

Maandiko yananifundisha kumfuata Yesu Kristo.

  • Ili kutambulisha hadithi ya Mfalme Yosia katika 2 Wafalme 22–23, ungeweza kuficha nakala ya maandiko mahali fulani katika chumba. Waalike watoto wako kuitafuta. Kisha ungeweza kushiriki kile kilichotokea wakati mmoja wa makuhani wa Yosia alipopata maandiko ndani ya hekalu (ona 2 Wafalme 22:8–11; ona pia “Mfalme Yosia” katika Hadithi za Agano la Kale, 148–49). Ni nini kingeweza kutokea kwetu kama hatungekuwa na maandiko? Shiriki na kila mmoja kwa nini una furaha kwamba tuna maandiko leo.

    1:36

    King Josiah

  • Baada ya kusoma 2 Wafalme 23:2–3, wewe na watoto wako mngeweza kuzungumza kuhusu maandiko ambayo yamekutia msukumo wa “kumfuata Bwana” (mstari wa 3). Mngeweza pia kuimba pamoja wimbo kuhusu maandiko, kama vile “Search, Ponder, and Pray” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,109).

2 Wafalme 23:1–3

Nitayashika maagano yangu na Mungu.

  • Wakati Yosia na watu wake walijifunza amri za Mungu, walifanya agano la kuziishi. Soma kuhusu hili pamoja na watoto wako katika 2 Wafalme 23:1–3, na wasaidie watafute maneno au virai ambavyo vinaonyesha jinsi watu walivyohisi kuhusu amri za Bwana. Inawezekana watoto wako wangeweza kusimama na kuzungumza kuhusu nini ingemaanisha “[kusimama] kwenye maagano.” Kisha wangeweza kutembea papo hapo walipo na kuzungumzia kuhusu “kumfuata Bwana” kunamaanisha nini. Kifuatacho, wangeweza kuweka mikono yao kwenye mioyo yao na kupendekeza njia tunazoweza kutii maagano yetu “kwa mioyo [yetu] yote.”

Kwa ajili ya zaidi, ona toleo la mwezi huu la jarida la Rafiki .

watu wakibomoai sanamu kwa kamba

Watu wa Yosia wakiondoa sanamu katika kwenye jiji; kielelezo na William Hole

ukurasa wa shughuli za Msingi: Maandiko yananifundisha kumfuata Yesu Kristo.