10. Kanaani Nyakati za Agano la Kale
Kask.
Sidoni
Dameski
Milima ya Lebanoni
Mlima Hermoni
Litani
Farpa
Tiro
Foenike
Dani (Laishi)
Hazori
Ziwa Hule (Maji ya Meromu)
Ako
Bashani
Bahari ya Kinerethi (Galilaya)
Kishoni
Bonde la Yezereeli
Gathi-heferi
Mlima Karmeli
Endori
Mlima Tabori
Yarmuki
Megido
Kilima cha More
Yezereeli
Beth-sheani
Dothani
Mlima Gilboa
Samaria
Samaria
Gileadi
Uwanda wa Sharoni
Shekemu
Mlima Ebali
Penueli
Mahanaimu
Mlima Gerizimu
Yaboki
Yafa
Shilo
Bahari Kuu (Bahari ya Mediterania)
Aiyaloni
Betheli (Luzu)
Ai
Mto Yordani
Raba (Amani)
Gibeoni
Yeriko
Amoni
Soreki
Yerusalemu
Ashdodi
Ekroni
Mlima wa Mizeituni
Mlima Nebo
Gathi
Bethlehemu
Ashkeloni
Ela
Tekoa
Bahari ya Chumvi (Bahari ya Mauti)
Gaza
Shefela
Uwanda wa Filistia
Lakishi
Hebroni
Engedi
Arnoni
Gerari
Gerari
Yuda
Moabu
Besori
Beer-sheba
Kir-haresethi
Idumaya
Eneo la Sodoma na Gomora
Negevu
Araba
Zeredi
Edomu
Kilomita
0 20 40 60
A B C D
1 2 3 4 5 6 7 8
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
15
15
15
15
16
17
18
19
20
21
-
Dani (Laishi) Yeroboamu alimsimamisha ndama wa dhahabu kwa ajili ya kuabudiwa na Ufalme wa Kaskazini (1 Fal. 12:26–33). Dani ulikuwa ni mpaka wa Kaskazini wa Israeli ya Kale.
-
Mlima Karmeli Eliya alipambana na manabii wa Baali na akafungua mbingu ili mvua inyeshe (1 Fal. 18:17–46).
-
Megido Mahali pa mapambano mengi (Amu. 4:13–16; 5:19; 2 Fal. 23:29; 2 Nya. 35:20–23). Sulemani alianzisha ushuru ili kuijenga Megido (1 Fal. 9:15). Mfalme Yosia wa Yuda alijeruhiwa vibaya sana katika pambano dhidi ya Farao Neko wa Misri (2 Fal. 23:29–30). Wakati wa Ujio wa Pili wa Bwana pigano kuu la mwisho litafanyika katika Bonde la Yezereeli kama sehemu ya pambano la Armagedoni (Yoe. 3:14; Ufu. 16:16; 19:11–21). Jina la Armagedoni ni nukuu ya Kiyunani kutoka Har-megidoni, Kiebrania, au Mlima wa Megido.
-
Yezereeli Jina la mji katika bonde lililo kubwa zaidi na lenye rutuba sana la Israeli lenye jina hilo hilo. Wafalme wa Ufalme wa Kaskazini walijenga Kasri mahali hapa (2 Sam. 2:8–9; 1 Fal. 21:1–2). Malkia mwovu Yezebeli aliishi na kufa hapa (1 Fal. 21; 2 Fal. 9:30).
-
Beth-sheani Waisraeli walipambana na Wakanaani hapa (Yos. 17:12–16). Mwili wa Sauli ulikomewa kwenye kuta za ngome hii (1 Sam. 31:10–13).
-
Dothani Yusufu aliuzwa utumwani na kaka zake (Mwa. 37:17, 28; 45:4). Elisha alipata ono la mlima uliojaa farasi na magari yanayokokotwa na farasi wa moto (2 Fal. 6:12–17).
-
Samaria Mji mkuu wa Ufalme wa Kaskazini (1 Fal. 16:24–29). Mfalme Ahabu alimjengea hekalu Baali (1 Fal. 16:32–33). Eliya na Elisha walihudumu hapa (1 Fal. 18:2; 2 Fal. 6:19–20). Katika mwaka 721 K.K. Waashuru waliuteka, wakimalizia kukamata yale makabila kumi (2 Fal. 18:9–10).
-
Shekemu Ibrahimu alijenga madhabahu hapa (Mwa. 12:6–7). Yakobo aliishi karibu na hapa. Simeoni na Lawi waliwaua kinyama wanaume wote wa mji huu (Mwa. 34:25). Ushawishi wa Yoshua wa “chagueni—leo” kumtumikia Mungu ulikuja katika Shekemu (Yos. 24:15). Hapa Yeroboamu alijenga mji mkuu wa kwanza wa ufalme wa Kaskazini (1 Fal. 12).
-
Mlima Ebali na Mlima Gerizimu Yoshua aliwagawa Israeli juu ya milima hii miwili—baraka za torati zilitangazwa kutoka Mlima Gerizimu, wakati laana ilikuwa kutoka Mlima Ebali (Yos. 8:33). Wasamaria baadaye walijenga hekalu juu ya Gerizimu (2 Fal. 17:32–33).
-
Penueli (Penieli) Hapa Yakobo alishindana mweleka usiku wote na mjumbe wa Bwana (Mwa. 32:24–32). Gideoni aliiangamiza ngome ya Wamidiani (Amu. 8:5, 8–9).
-
Yafa Yona alisafiri kwa meli kutoka hapa kuelekea Tarshishi ili kuepuka huduma yake kwa Ninawi (Yon. 1:1–3).
-
Shilo Katika wakati wa Waamuzi, mji mkuu wa Israeli na hema vilikuwa hapa (1 Sam. 4:3–4).
-
Betheli (Luzu) Hapa Ibrahimu alijitenga na Lutu (Mwa. 13:1–11) na akapata ono (Mwa. 13; Ibr. 2:19–20). Yakobo alipata ono la ngazi iliyofika mbinguni (Mwa. 28:10–22). Hema liliwekwa hapa kwa muda (Amu. 20:26–28). Yeroboamu alimsimamisha ndama wa dhahabu kwa ajili ya kuabudu ufalme wa Kaskazini (1 Fal. 12:26–33).
-
Gibeoni Watu wa Hiti kutoka hapa walimlaghai Yoshua kuingia mkataba (Yos. 9). Jua lilisimama tuli wakati Yoshua aliposhinda vita (Yos. 10:2–13). Hili pia lilikuwa eneo la muda la hema (1 Nya. 16:39).
-
Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Ekroni, Gathi (miji mitano ya Wafilisti) Kutoka katika miji hii Wafilisti mara kwa mara walifanya vita dhidi ya Israeli.
-
Bethlehemu Raheli alizikwa karibu ya hapa (Mwa. 35:19). Ruthu na Boazi waliishi hapa (Rut. 1:1–2; 2:1, 4). Uliitwa mji wa Daudi (Lk. 2:4).
-
Hebroni Ibrahimu (Mwa. 13:18), Isaka, Yakobo (Mwa. 35:27), Daudi (2 Sam. 2:1–4), na Absalomu (2 Sam. 15:10) waliishi hapa. Huu ulikuwa mji mkuu wa kwanza wa Yuda chini ya Mfalme Daudi (2 Sam. 2:11). Inaaminika kwamba Ibrahimu, Sara, Isaka, Rebeka, Yakobo, na Lea walizikwa hapa katika pango la Makpela (Mwa. 23:17–20; 49:31, 33).
-
Engedi Daudi alijificha kumkimbia Sauli na hivyo kuokoa maisha ya Sauli (1 Sam. 23:29–24:22).
-
Gerari Ibrahimu na Isaka waliishi hapa kwa muda (Mwa. 20–22; 26).
-
Beer-sheba Ibrahimu alichimba kisima hapa na alifanya agano na Abimaleki (Mwa. 21:31). Isaka alimwona Bwana (Mwa. 26:17, 23–24), na Yakobo aliishi hapa (Mwa. 35:10; 46:1).
-
Sodoma na Gomora Lutu alichagua kuishi Sodoma (Mwa. 13:11–12; 14:12). Mungu aliiangamiza Sodoma na Gomora kwa sababu ya uovu (Mwa. 19:24–26). Yesu baadaye aliitumia miji hii kama mifano ya uovu (Mt. 10:15).