“Musa na Nyoka wa Shaba,” Hadithi za Agano la Kale (2022)
“Musa na Nyoka wa Shaba,” Hadithi za Agano la Kale
Hesabu 21
Musa na Nyoka wa Shaba
Kujifunza kuwa na imani katika Bwana.
Wakati Waisraeli walipokuwa wakisafiri nyikani mara nyingi walimsahau Bwana na kulalamika. Bwana aliwatuma nyoka ili kuwasaidia kumkumbuka Yeye. Nyoka waliwauma watu, wengi wa watu hao walikufa.
Hesabu 21:1–6
Kisha watu walitubu. Walimsihi Musa aombe kwa Bwana ili afanye nyoka wale watoweke. Bwana akuwaondoa wale nyoka. Lakini alitengeneza njia kwa ajili ya watu kuokolewa kama wangeumwa.
Hesabu 21:7.
Bwana alimwambia Musa kutengeneza nyoka kutokana na shaba na kumning’iniza kwenye fimbo. Watu walipoumwa na nyoka na wakamwangalia yule nyoka wa shaba, Bwana aliwaokoa. Bwana aliwasaidia Waisraeli kuwa wanyenyekevu na kumtumaini Yeye.
Hesabu 21:8–9; 1 Nefi 17:41; Helamani 8:14–15