2025
Ninawezaje kujua kwamba kweli nimetubu na nimesamehewa?
Juni 2025


Ujumbe wa kila mwezi wa Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Juni 2025

Ninawezaje kujua kwamba kweli nimetubu na nimesamehewa?

msichana akisali

Kuja Duara Kamili, na Jenedy Page

Bwana amesema, “Tazama, yule ambaye ametubu dhambi zake, huyu anasamehewa, na Mimi, Bwana, sizikumbuki tena.”

“Kwa hili mnaweza kujua kama mtu ametubu dhambi zake—tazama, ataungama na kuziacha” (Mafundisho na Maagano 58:42–43).

Kupitia toba ya dhati, tunaweza kupokea msamaha. Wakati unapohisi faraja kutoka kwa Roho, unaweza kujua kwamba nguvu ya Mwokozi ya kulipia dhambi inafanya kazi katika maisha yako. Na kama tutateleza tena, tunaweza tena kutubu, kusamehewa, na kuendelea kujaribu.

Kwa nyongeza, Mzee Dieter F. Uchtdorf wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili amefundisha: “Shetani atajaribu kutufanya tuamini kwamba dhambi zetu hazisamehewi kwa sababu tunaweza kuzikumbuka. Shetani ni mwongo. … Mungu hakuahidi kwamba sisi hatutakumbuka dhambi zetu. Kukumbuka kutatusaidia kuepuka kutenda makosa hayo hayo tena. Lakini kama tutakuwa wakweli na waaminifu, kumbukumbu ya dhambi zetu italainishwa muda baada ya muda.”