Wito wangu kama Mshauri katika Urais wa Wasichana wa Kigingi
Majukumu
Bwana anashukuru kwa utayari wako wa kuhudumu katika Kanisa Lake. Hapa chini ni muhtasari wa majukumu ya wito wako.
Dhumuni la Wasichana
Kundi la Wasichana huwasaidia mabinti wapendwa wa Mungu kujiandaa kurudi katika uwepo Wake. Huwasaidia wasichana kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo wa maisha yote kadiri wanavyofanya na kushika maagano matakatifu na kuongeza uongofu wao. Katika madarasa na mikusanyiko yao, wasichana huwahudumia watu wengine, hutimiza majukumu ya kimaagano, wanajenga umoja na wanajifunza na kuyaishi mafundisho. (Ona Kitabu cha Maelezo ya Jumla, 11.1.1.)
Mshauri Katika Urais wa Wasichana wa Kigingi
Mshauri wa Wasichana wa kigingi anaandaa “jeshi la vijana” wa Bwana ili kukusanya Israeli kupitia kushiriki katika juhudi za kujenga imani na kuwaimarisha watu binafsi (ona Russell M. Nelson and Wendy W. Nelson, “Hope of Israel” [worldwide youth devotional, June 3, 2018], Gospel Library). Anasaidia kuelezea majukumu mapya kwa urais mpya wa wasichana katika kata, hutoa msaada endelevu, na anahudumu kwenye kamati ya uongozi wa vijana katika kigingi (ona 29.3.9).
Mikutano
Washauri katika Urais wa Wasichana wa Kigingi hutoa mafunzo kwa urais wa vikundi katika kata wakati wa mikutano ya mwaka ya uongozi wa kigingi (ona 29.3.4), Anahudhuria mikutano ya urais na mikutano ya baraza la uratibu anapoalikwa na Sabini wa Eneo kufanya hivyo (ona 29.4), na huzungumza katika mikutano ya sakramenti na mazingira mengine wakati wanapoalikwa na urais wa kigingi.
Shughuli
Chini ya maelekezo ya urais wa kigingi, urais wa Wasichana wa kigingi pia hupanga na kuratibu shughuli na kambi za Wasichana katika kigingi (ona 6.7.1.2). Kwa vigingi vingi, urais hushauriana pamoja ili kupendekeza shughuli za pamoja kwa urais wa kigingi (ona 20.3.1).
Miongozo na Sera
Miongozo ya ziada na sera inapatikana katika sehemu ya 11.6 ya Kitabu cha Maelezo ya Jumla.