2025
Yesu Kristo: Tumaini na Ahadi ya Pasaka
Aprili 2025


“Yesu Kristo: Tumaini na Ahadi ya Pasaka,” Liahona, Apr. 2025.

Ujumbe wa Kila Mwezi wa Liahona , Aprili 2025

Yesu kristo: Tumaini na Ahadi ya Pasaka

Kupitia tumaini na ahadi ya Pasaka, Yesu Kristo anajaza matamanio ya mioyo yetu na kujibu maswali ya nafsi zetu.

tawi la mti tasa

Vielelezo na Michael T. Malm

Tafadhali tengeneza wakati mtulivu na mahali pa kimbilio la kiroho unaposoma ujumbe huu.

Mara nyingi sana, ulimwengu wetu una kelele nyingi, umejaa uongo na kiburi. Lakini tunapokuwa na umaizi kuhusu sisi wenyewe na ushawishi wa Mungu, tumaini na ahadi ya Pasaka katika Yesu Kristo huwa kweli. Katika nyakati kama hizo, tunasihi:

“Ninawezaje kumwona mshiriki wa familia yangu, rafiki yangu, mpendwa wangu tena?”

“Katika ulimwengu uliojaa ‘ninachagua uhusiano wa mimi mwenyewe’, ninapata wapi na kujisikia amani, tumaini, na ushirika na Mungu (ona Mafundisho na Maagano 107:19), wale wanao nizunguka, na mimi mwenyewe?”

“Je, kuna mtu ninayeweza kumpenda—na ni nani atakayenipenda kweli? Je, uhusiano wa maagano unaweza kukua na kudumu, si kama hadithi ya kufikirika bali kwa kamba imara kuliko kamba za mauti, furaha ya kweli na ya milele?”

“Mahali palipo na maumivu mengi, mateso, na ukosefu wa haki, ninawezaje kuchangia kwenye amani, maelewano, na uelewa katika Yesu Kristo na katika injili Yake iliyorejeshwa na Kanisa Lake?”

Katika msimu huu wa Pasaka, ninatoa ushuhuda wangu juu ya Yesu Kristo na ahadi na tumaini Lake.

Ahadi ya Kuwa wa Agano na Dhumuni

Mungu, Baba yetu wa Milele aliye Mbinguni; Yesu Kristo, Mwanawe Mpendwa; na Roho Mtakatifu wao katika hali binafsi binafsi wako karibu nasi. Nuru yao isiyo na mwisho na ya milele, huruma, na upendo wa ukombozi vimefumwa katika kusudi la uumbaji na kitambaa cha uwepo wetu (ona Alma 30:44; Musa 6:62–63).

Katika Baraza la Mbinguni, “nyota za asubuhi ziliimba pamoja, na wana wote [na mabinti] wote wa Mungu walipiga kelele kwa shangwe” (Ayubu 38:7). Tulifanya uchaguzi. Sasa tunatembea kwa imani. Kupitia uzoefu wetu wenyewe, tunagundua uzuri ulioahidiwa na Mungu, uwazi, shangwe, na dhumuni katikati ya dunia ya kutokuwa na uhakika, kuvunjika moyo, na changamoto.

Hatukukusudiwa kutangatanga peke yetu katika ulimwengu wa kutokuwa na uhakika. Tunaweza kuwasiliana na mbingu, kujenga imani na kuwa sehemu ya familia na katika kaya ya jumuiya ya Watakatifu, na kuwa wakweli, huru, thabiti zaidi, wenye shangwe kupitia utiifu wa hiari na shangwe ya utiifu kwa amri za Mungu. Upatanisho—katika na kupitia Yesu Kristo unaleta agano hili la kuwa sehemu ya.

tawi la mti lenye chipukizi linalochanua

Tumaini la Maisha na Misheni ya Yesu Kristo

Kila siku, tumaini na ahadi ya Pasaka hujumuisha baraka na mafundisho ambayo Yesu Kristo alishiriki wakati wa huduma Yake kamilifu duniani. Akiwa ametawazwa mwanzoni, Yesu Kristo alizaliwa akiwa Mwana wa Pekee wa Mungu (ona Yakobo 4:5; Alma 12:33–34; Musa 5:7, 9). “Naye akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu” (ona Luka 2:52). Akitafuta tu kufanya mapenzi ya Baba Yake, Yesu Kristo alisamehe dhambi, akaponya udhaifu, akafufua wafu, na kuwafariji wagonjwa na wapweke.

Wakati mmoja, baada ya kufunga siku 40, Yeye alishuhudia “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiria masikini habari njema; Amenituma kuponya waliovunjika moyo, kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena,kuwaacha huru waliosetwa” (Luka 4:18; ona pia Isaya 61:1).

Hao ni kila mmoja wetu.

Katika Chakula cha Jioni, Yesu Kristo aliosha miguu ya wanafunzi Wake (ona Yohana 13:4–8). Katika ulimwengu wa Kale na Mpya, “maji ya uzima” na “mkate wa uzima” Mwenyewe alianzisha sakramenti. Katika ibada takatifu ya sakramenti, tunamwomba Baba na tunafanya agano la kujichukulia juu yetu jina la Yesu Kristo, daima kumkumbuka Yeye, na kutii amri Zake, ili daima Roho Wake apate kuwa pamoja nasi (ona Luka 22:19–20; 3 Nefi 18:7, 10–11).

Katika Bustani ya Gethsemane, Yesu aliteseka zaidi ya binadamu anavyoweza kuteseka ili kukomboa na kulipa adhabu ya makosa yetu. Damu ilitoka kwenye kila kinyweleo. Aliteseka maumivu haya kwa ajili ya wote, ili kwamba tusiweze kuteseka kama tungetubu (ona Mafundisho na Maagano 18:11; 19:16).

Akisalitiwa na kutuhumiwa kwa uwongo, Yesu Kristo alidhihakiwa na kupigwa mijeledi, na taji la miiba lilitupwa juu ya kichwa Chake cha unyenyekevu (ona Mathayo 27:26, 29; Marko 15:15, 17, 20, 31; Luka 22:63; Yohana 19:1–2). “Kuchubuliwa kwa ajili ya uovu wetu … kwa kupigwa kwake sisi tumeponywa” (Isaya 53:5). “Aliinuliwa juu kwenye msalaba” ili kutuleta Kwake (ona 3 Nefi 27:14–15). Bado, hata msalabani, Yesu Kristo alisamehe (ona Luka 23:34). Alimwomba Yohana amtunze mama Yake (ona Yohana 19:26–27). Alihisi kuachwa (ona Mathayo 27:46; Marko 15:34). Ili andiko lipate kutimizwa, Alisema Aliona kiu (ona Yohana 19:28). Wakati yote yalipokuwa yametimizwa, Yeye mwenyewe “alikata roho” (Luka 23:46; ona pia Yohana 10:17–18).

Yesu Kristo anajua jinsi ya kutusaidia katika magonjwa yetu, udhaifu, upweke, kutengwa, na taabu (ona Alma 7:12). Mateso kama hayo mara nyingi huja kama matokeo ya chaguzi za wengine. Yeye pia anajua jinsi ya kufurahi pamoja nasi katika furaha na shukrani zetu, jinsi ya kulia pamoja nasi wakati furaha yetu inapokuwa imejaa. Kwa upole, Anatuita katika jina Lake, kwa sauti Yake, katika zizi Lake. Anamwita kila mtu kila mahali. Anatualika sisi kuona na kuelewa maisha ya duniani kupitia mtazamo wa milele. Tunapotembea wima na kushika maagano yetu, Yeye anaahidi kwamba vitu vyote vinaweza kufanya kazi pamoja kwa faida yetu (ona Mafundisho na Maagano 90:24; Warumi 8:28).

Katika wakati na njia Yake, urejesho unakuja—sio tu kwa jinsi mambo yalivyokuwa bali pia kwa kile yanachoweza kuwa. Kwa kweli, Yesu Kristo anaweza kutuweka huru kutokana na utumwa na dhambi, kutokana na kifo na jehanamu, na anaweza kutusaidia kutimiza utambulisho wetu wa kiungu tunapokuwa zaidi ya tunavyofikiria, kupitia imani na toba.

Ahadi ya Ukombozi

Kwa sababu ya Yesu Kristo, kifo sio mwisho. Wakati wa Pasaka tunatangaza:

Kifo kimeshindwa; mwanadamu yuko huru.

Kristo ameleta ushindi.

Kwa amri na nguvu kutoka kwa Baba Yake, Yesu angeweza kuyaweka chini maisha Yake na kuyachukua tena (ona Yohana 10:17). Wakati mwili Wake ukiwa kaburini, Yesu Kristo alihudumu na kufanya mpangilio katika ulimwengu wa roho, akitangaza “ukombozi wao kutokana na kamba za kifo” (Mafundisho na Maagano 138:16).

Asubuhi ya siku ya tatu, Alifufuka kutoka kaburini. Alizungumza na Mariamu. Aliwatokea wanafunzi wawili wakiwa njiani kwenda Emau, Mitume Wake, na wengineo. (Ona Mathayo 28; Marko 16; Luka 24; Yohana 20).

Katika ushuhuda wa kujirudia, aliwaalika wanafunzi Wake kutupa nyavu zao upande mwingine wa merikebu; wakati huu, ingawa tena zilijaa samaki, nyavu hazikuchanika (ona Yohana 21:6–11; Luka 5:3–7). Aliwalisha chakula wanafunzi na kumsihi Petro mara tatu kuwalisha kondoo na wanakondoo Wake (ona Yohana 21:12–17). Alipaa kwenda mbinguni, akitangaza kwamba wanafunzi Wake wakati huo na sisi sote sasa tunapaswa kushiriki habari tukufu za Pasaka na injili Yake kwa kila taifa, kabila, na watu (ona Mathayo 28:19–20; Marko 16:15).

Yesu Kristo ni Mchungaji wetu Mwema na Mwanakondoo wa Mungu. Alitoa uhai Wake kwa ajili ya, na kutoa uhai Wake kwa kondoo Wake. Katika bustani na msalabani, Yeye alibeba yasiyovumilika na alilipia dhambi zetu. Sasa na milele, Yeye hutuonyesha kwa mfano jinsi “kifo kinavyofungua njia ya kuingia katika umilele.”

Kupitia nguvu ya Yesu Kristo ya Upatanisho na Ufufuko, miili yetu na roho zetu vitaunganishwa tena katika ufufuko wa kimwili. Tutakuwa watukufu, tukirejeshwa katika nyuso na umbo la kimwili, mguu hadi mkono. Hata nywele za vichwa vyetu zitarejeshwa. Tutakuwa huru kutokana na maradhi ya muda, magonjwa, ajali ya kimwili, na kutojiweza kiakili. Upatanisho wa Kristo unaweza kutubariki kushinda kila aina ya utengano wa kiroho na kifo cha kiroho. Kwa sharti la toba, tunakuwa huru kutokana na kila dhambi na huzuni na kufunguliwa kwa utimilifu wa milele wa upendo na shangwe. Tukiwa wasafi, huru, tunaweza kurudi katika uhusiano wetu pendwa wa kifamilia hadi kwenye uwepo mtukufu wa selestia wa Mungu Baba yetu na Yesu Kristo.

Tutawaona wapendwa wetu kwa mara nyingine tena. Tunapoungana tena na wale tunaowapenda, tutaonana kwa mtazamo wa milele—kwa upendo mkuu, uelewa, na ukarimu. Upatanisho wa Yesu Kristo unaweza kutusaidia kukumbuka kile kilicho muhimu na kusahau kile kisicho muhimu. Kumwona Mwokozi wetu na uhusiano wetu kwa imani kuu na shukrani huleta amani, hufanya mizigo iwe myepesi, hupatanisha mioyo, na huziunganisha familia hapa duniani na milele yote.

tawi la mti lenye maua

Tumaini la Wingi na Shangwe

Pasaka katika Yesu Kristo inajumuisha kufunguliwa kwa madirisha ya mbinguni, tunda la mzabibu likiongezeka, na ardhi kuwa ya kupendeza. Pasaka katika Yesu Kristo inajumuisha kuwafariji na kuwatunza wajane na mayatima, wenye njaa na wasiojiweza, wale ambao wanaogopa, kunyanyaswa, au kupatwa na madhara pasipo kuwa na hatia. Akimjali kila mmoja, Yesu Kristo anatualika kuona na kutumikia kwa upendo na huruma, kama Yeye anavyofanya.

Katika mambo yote mazuri, Yesu Kristo anarejesha kwa wingi (ona Yohana 10:10; Alma 40:20–24). Anaahidi kwamba “dunia imejaa, na kuna vya kutosha na kubakia” (Mafundisho na Maagano 104:17). Urejesho wake wa vitu vyote unajumuisha utimilifu wa injili Yake, mamlaka na nguvu Yake ya ukuhani, na ibada na maagano matakatifu yanayopatikana katika Kanisa Lake, linaloitwa kwa jina Lake, hata Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho.

Pasaka katika Yesu Kristo inajumuisha nyumba zaidi takatifu za Bwana kuja karibu na watoto wa Mungu katika maeneo mengi, kuleta katika mioyo yetu mafundisho ya “waokozi juu ya Mlima Sayuni” (ona Obadia 1:21). Bwana hutoa njia ya kutakasa, isiyo na ubinafsi kwa ajili yetu kutoa duniani kile ambacho wapendwa walioondoka wanakihitaji na kukitamani katika umilele ambacho hawawezi kujipatia wao wenyewe.

Hilo ndilo tumaini, ahadi, na ushuhuda wangu. Ninamshuhudia Mungu Baba yetu; Mwokozi na Mkombozi wetu, Yesu Kristo; na Roho Mtakatifu. Katika Pasaka na kila siku, na tuweze kupata tumaini la milele na ahadi katika mpango mtakatifu wa furaha wa Mungu, pamoja na njia yake ya agano ya mabadiliko matakatifu kutoka maisha ya duniani hadi kutokufa na uzima wa milele. Kila siku uhakika wa Upatanisho wa Yesu Kristo uweze kufanya mizigo yetu iwe myepesi, kutusaidia kuwafariji wengine katika huzuni zao, na kuziweka huru nafsi zetu ili kupokea shangwe Yake timilifu.

Kupitia tumaini na ahadi ya Pasaka, Yesu Kristo anajaza matamanio ya mioyo yetu na kujibu maswali ya nafsi zetu.

Muhtasari

  1. Yohana 4:10, 14; 6:35; 7:37; ona pia Isaya 49:10.

  2. (Ona Mathayo 26:26–29; Marko 2:22–25; Luka 10:17–20; Yohana 1–11.)

  3. Kafufuka!,” Nyimbo za Dini, na. 199.

  4. Msalabani Golgota,” Nyimbo za Dini, na. 101.

  5. Ona Teachings of Presidents of the Church: Joseph Smith (2011), 473, Maktaba ya Injili.