“Je, Ni Kitu Gani Kinafanya Maandiko kuwa ‘ya Thamani Kuu’?,” Liahona, Jan. 2024.
Njoo, Unifuate
Je, ni Kitu Gani Kinafanya Maandiko Kuwa “ya Thamani Kuu”?
Maandiko yalikuwa “ya thamani kuu” (1 Nefi 5:21) kwa familia ya Lehi. Yalikuwa muhimu sana kiasi kwamba Bwana aliamuru watoto wa Lehi wasafiri kurudi hadi Yerusalemu ili kuchukua mabamba ya shaba (ona 1 Nefi 3:2–5), kazi ambayo ilihatarisha maisha yao. Maandiko (hususani Kitabu cha Mormoni) vile vile ni muhimu kwetu sisi leo. Je, umewahi kufikiria hivi karibuni kuhusu kwa nini ni muhimu?
|
Je, ni kitu gani mabamba ya shaba yaliipa familia ya Lehi? |
Je, Kitabu cha Mormoni kinatupa nini sisi leo? |
|
Maneno ya manabii (1 Nefi 3:20) |
Msingi wa ushuhuda wa Joseph Smith, Urejesho, na manabii walio hai (Utangulizi wa Kitabu cha Mormoni) |
|
Hadithi ya Uumbaji na Adamu na Hawa (1 Nefi 5:11) |
Mafundisho ya ufafanuzi kuhusu mpango wa wokovu (2 Nefi 2; Alma 12; 34) |
|
Sheria ya Musa (1 Nehi 4:15–16) na amri nyinginezo (1 Nefi 5:21) |
Mafundisho ya Kristo na amri nyinginezo (2 Nefi 31; 3 Nefi 11; 27) |
|
Kumbukumbu ya Wayahudi na ushahidi wao juu ya Kristo (1 Nefi 5:12) |
Mashahidi wa ziada wa Kristo kutoka “kondoo Wake wengine” (3 Nefi 15:21–24) |
|
Kumbukumbu ambayo ilihifadhi lugha ya baba zao (1 Nefi 3:19) na koo zao (1 Nefi 5:14) |
Kumbukumbu ambayo inaweza kutusaidia sisi kuwakusanya Israeli waliotawanyika (3 Nefi 21:6–7) |