“Watakatifu Wanaenda Magharibi,” Rafiki, Desemba 2025, 26–28.
Ujumbe wa kila mwezi katika Rafiki, Desemba 2025
Watakatifu Wanaenda Magharibi
Baada ya kifo cha Joseph Smith, Brigham Young na Mitume wengine waliliongoza Kanisa. Brigham alijua Watakatifu walipaswa kuondoka Nauvoo kwa sababu hapakuwa salama. Lakini Bwana aliwataka wamalizie kujenga hekalu kwanza.
Wakati hekalu lilipokuwa tayari, maelfu ya Watakatifu walifanya maagano na Bwana na waliunganishwa kama familia.
Sasa ilikuwa ni wakati wa kuanza safari yao kuelekea magharibi. Hali ya hewa ilikuwa baridi, na watu walikuwa wagonjwa na wenye njaa.
Brigham alisali kwa ajili ya msaada. Bwana alisema wanapaswa kusaidiana, na Yeye angewabariki na kuwasaidia.
Safari bado ilikuwa ngumu sana. Baadhi ya watu walifariki. Lakini kwa sababu ya maagano yao ya hekaluni, Watakatifu walijua wangewaona wanafamilia wao tena.
Watakatifu wa kwanza waliwasili katika Bonde la Salt Lake mwaka 1847. Hapa wangeweza kumwabudu Bwana na kuifanya kazi Yake kwa amani.
Kwa miaka mingi, Watakatifu zaidi walifika na kujenga mahekalu zaidi. Wamisionari walisafiri ulimwenguni kote kuifundisha injili ya Yesu Kristo. Kanisa la Mwokozi liliendelea kukua, likiwabariki watoto wa Baba wa Mbinguni kila mahali.
Ukurasa wa Kupaka Rangi
Yeye Ni Nuru, Uzima, na Tumaini la Ulimwengu
Kielelezo na Corey Egbert
Je, wewe unafanya nini wakati wa Krismasi ili kumkumbuka Yesu Kristo?
© 2025 na Intellectual Reserve, Inc. Haki zote zimehifadhiwa. Limepigwa chapa Marekani. Idhini ya Kiingereza: 6/19. Idhini ya kutafsiri: 6/19. Tafsiri ya Monthly Friend Message, December 2025. Swahili. 19637 743