Rafiki
Nuhu na Safina
Rafiki Februari 2026


“Nuhu na Safina,” Rafiki, Februari 2026, 46–48.

Ujumbe wa kila mwezi wa Rafiki , Februari 2026

Nuhu na Safina

Kielelezo cha Nuhu na familia yake wakichunga kondoo

Nuhu na familia yake walimtii Bwana. Watu wengine wote walikuwa waovu sana. Bwana alimwambia Nuhu kwamba gharika ingeifunika dunia ikiwa watu hawakutubu.

Nuhu anahubiri

Nuhu aliwaambia watu kwamba Bwana aliwapenda na aliwataka watubu na kuwa na imani katika Yesu Kristo. Watu hawakusikiliza.

Nuhu na familia yake wanajenga safina.

Bwana alimwambia Nuhu kujenga meli kubwa iliyoitwa safina. Safina ingewaweka salama familia ya Nuhu wakati wa gharika.

Wanyama wakitembea kuingia ndani ya safina

Familia ya Nuhu iliingiza vyakula ndani ya safina. Bwana aliwapeleka angalau wanyama wawili wa kila aina kwa Nuhu ili awaingize ndani ya safina. Kisha mvua ikaanza kunyesha.

Safina ikielea juu ya bahari

Mvua ilinyesha kwa siku 40 mchana na usiku 40. Gharika iliifunika dunia, kama vile Bwana alivyokuwa ameonya.

Nuhu na familia yake ndani ya safina.

Familia ya Nuhu pamoja na wanyama wote ndani ya safina walielea kwa usalama juu ya maji.

Familia ya Nuhu na wanyama wamesimama juu ya nchi na kuangalia upinde wa mvua

Wakati gharika ilipokoma, safina ilisimama juu ya ardhi kavu. Nuhu na familia yake walimshukuru Bwana kwa kuwalinda. Bwana aliahidi kamwe kutoleta gharika duniani tena. Alituma upinde wa mvua kama ukumbusho wa ahadi Yake.

Ukurasa wa Kupaka Rangi

Kumfuata Nabii wa Bwana Kutanibariki

Ukurasa wa PDF

Kielelezo na Audrey Day

Je, unaweza kufanya nini ili kumfuata Nabii?