2025
Jela ya Liberty
Mei 2025


“Jela ya Liberty,” Rafiki, Agosti 2025, 26-28.

Ujumbe wa Kila Mwezi wa Rafiki , Agosti 2025

Jela ya Liberty

Nyumba zikiteketea kwa moto na wanaume wenye hasira wakiwa na bunduki

Watu wengi huko Missouri hawakuwapenda Watakatifu. Gavana aliwatuma askari ili kuwafanya waondoke.

Mwanaume juu ya farasi akimnyoshea upanga Joseph Smith

Askari waliwakamata Joseph Smith na viongozi wengine wa Kanisa. Usiku mmoja, walinzi walikuwa wakicheka kuhusu mambo mabaya waliyokuwa wamewafanyia Watakatifu.

Joseph Smith akiwa na minyororo kwenye vifundo vya mikono yake, akisimama na kuzungumza na wanaume

Joseph alisimama wima na kuwanyamazisha kwa sauti kubwa, “Nyamazeni!” Yeye aliongea kwa nguvu za Mungu. Walinzi walisema samahani na kuacha kuzungumza.

Joseph Smith na wanaume wengine katika Jela ya Liberty wakionekana wenye huzuni na wenye kujisikia baridi

Baadaye, Joseph na rafiki zake waliwekwa jela katika mji ulioitwa Liberty. Jela ilikuwa yenye baridi, ndogo, na yenye giza. Walikuwa tu na majani machafu ya kulalia. Chakula walichopewa kiliwafanya kuwa wagonjwa.

Joseph Smith akilia na mtu akimfariji

Joseph alikuwa na wasiwasi kuhusu Watakatifu. Lakini hangeweza kufanya cho chote cha kuwasaidia.

Joseph Smith akiwa amepiga magoti kusali katika jela

Joseph alisali sana. Aliuliza kama Mungu alikuwa amesahau kumhusu yeye na waumini wa Kanisa.

Joseph Smith akiwa amepiga magoti jela, akitazama juu kuelekea kwenye mwanga wa mwali wa jua katika dirisha dogo

Mungu alijibu sala ya Joseph. Yeye alisema, “Mwanangu, amani iwe katika nafsi yako.” Mungu alimwambia Joseph kwamba changamoto zake hazitadumu milele, na zingekuwa kwa faida yake. Yeye aliahidi kwamba Yeye angekuwa pamoja na Joseph “milele na milele” (Mafundisho na Maagano 121:7, 46).

Ukurasa wa Kupaka Rangi

Ninaweza Kuwa Kama Nuru kwa Wengine.

Shughuli ya ukurasa wa kupaka rangi ikiwa na mnara wa taa, ufukwe wa miamba, na mashua baharini

Kielelezo na Corey Egbert

Ni kwa jinsi gani wewe ni mfano mzuri kwa wengine?