“Lucy Anapata Ukweli,” Rafiki, Aprili 2025, 26–28.
Ujumbe wa kila mwezi wa jarida la Rafiki , Aprili 2025
Lucy Anapata Ukweli
Siku moja, Lucy Morley mwenye umri wa miaka 15 alikuwa akimsaidia jirani yake, Abigail Daniels, kufuma nguo. Walipokuwa wakifanya kazi, wamisionari watatu walipiga hodi mlangoni. Walisema kwamba Yesu Kristo alikuwa amewatuma kushiriki ujumbe.
Wanaume wale waliwaambia Abigail na Lucy kwamba Yesu alikuwa amemwita Joseph Smith kuwa nabii. Pia waliwaambia kuhusu Kitabu cha Mormoni.
Kwa mshangao wa Lucy, Abigail alikasirika. Aliwafanya wamisionari wale waondoke.
Lucy alijua wamisionari hawa walikuwa watumishi wa Mungu. Aliwaambia waitembelee familia yake inayoishi mwisho wa mtaa.
Wamisionari walienda nyumbani kwa Morley. Wazazi wa Lucy waliwaalika wamisionari wale ili kuwafundisha wao na marafiki zao.
Jioni hiyo, watu 17 walibatizwa. Katika siku chache zilizofuata, watu 50 zaidi waliwasikia wale wamisionari na wakabatizwa. Hata jirani yake Lucy, Abigail alibadili mawazo yake. Yeye na mume wake, pamoja na Lucy na wanafamilia yake, walichagua kumfuata Yesu Kristo kwa kubatizwa.
Ukurasa wa Kupaka Rangi
Kwa Sababu ya Yesu Kristo, Mimi Nitafufuka.
Kielelezo na Corey Egbert
Ni kwa jinsi gani unamkumbuka Yesu wakati wa Pasaka?
© 2025 na Intellectual Reserve, Inc. Haki zote zimehifadhiwa. Limepigwa chapa huko Marekani. Idhini ya Kiingereza: 6/19. Idhini ya kutafsiri: 6/19. Tafsiri ya Monthly Friend Message, April 2025. Swahili. 19631 743