2025
Lucy Anapata Ukweli
Aprili 2025


“Lucy Anapata Ukweli,” Rafiki, Aprili 2025, 26–28.

Ujumbe wa kila mwezi wa jarida la Rafiki , Aprili 2025

Lucy Anapata Ukweli

Msichana akifungua mlango ili kuruhusu kikundi cha wanaume kuingia ndani huku mwanamke akiwa amekaa kitandani

Siku moja, Lucy Morley mwenye umri wa miaka 15 alikuwa akimsaidia jirani yake, Abigail Daniels, kufuma nguo. Walipokuwa wakifanya kazi, wamisionari watatu walipiga hodi mlangoni. Walisema kwamba Yesu Kristo alikuwa amewatuma kushiriki ujumbe.

Mwanamke kwenye kifaa cha kufumia akiwa amekunja uso huku wanaume wakizungumza na msichana mdogo

Wanaume wale waliwaambia Abigail na Lucy kwamba Yesu alikuwa amemwita Joseph Smith kuwa nabii. Pia waliwaambia kuhusu Kitabu cha Mormoni.

Mwanamke mwenye hasira akiwafukuza wanaume nje ya nyumba yake

Kwa mshangao wa Lucy, Abigail alikasirika. Aliwafanya wamisionari wale waondoke.

Wanaume wakiangalia nyuma wakati msichana akiwakimbilia

Lucy alijua wamisionari hawa walikuwa watumishi wa Mungu. Aliwaambia waitembelee familia yake inayoishi mwisho wa mtaa.

Wanaume kwenye meza ya chakula cha jioni pamoja na msichana na familia yake

Wamisionari walienda nyumbani kwa Morley. Wazazi wa Lucy waliwaalika wamisionari wale ili kuwafundisha wao na marafiki zao.

Msichana na kuweka taulo kuzunguka mabega ya mwanamke wakati mtu mwingine anabatizwa katika mto ulio upande wa nyuma

Jioni hiyo, watu 17 walibatizwa. Katika siku chache zilizofuata, watu 50 zaidi waliwasikia wale wamisionari na wakabatizwa. Hata jirani yake Lucy, Abigail alibadili mawazo yake. Yeye na mume wake, pamoja na Lucy na wanafamilia yake, walichagua kumfuata Yesu Kristo kwa kubatizwa.

Ukurasa wa Kupaka Rangi

Kwa Sababu ya Yesu Kristo, Mimi Nitafufuka.

Kielelezo cha kaburi tupu

Kielelezo na Corey Egbert

Ni kwa jinsi gani unamkumbuka Yesu wakati wa Pasaka?