2025
Joseph Smith Anapokea Mabamba ya Dhahabu
Februari 2025


“Joseph Smith Anapokea Mabamba ya Dhahabu,” Rafiki, Februari 2025, 26–28.

“Ninaweza Kuwa Shahidi Kwamba Kitabu cha Mormoni ni cha Kweli,” Rafiki, Februari 2025, 48.

Ujumbe wa kila mwezi wa jarida la Rafiki, Februari 2025

Joseph Smith Anapokea Mabamba ya Dhahabu

Unaweza kusoma hadithi hii katika Joseph Smith—Historia ya 1:28–60.

Joseph Smith akiangalia nje ya dirisha

Miaka mitatu baada ya Ono la Kwanza, Joseph Smith alijihisi vibaya kuhusu baadhi ya makosa aliyokuwa amefanya. Aliomba kwa Baba wa Mbinguni kuhusu hilo.

Joseph akiwa amepiga magoti katika sala

Wakati Joseph alipokuwa akisali, mwanga ulijaa chumbani. Alimwona malaika amesimama hewani. Jina la malaika yule lilikuwa Moroni.

Malaika Moroni akimtembelea Joseph Smith chumbani kwake

Moroni alisema kulikuwa na kitabu kilichotengenezwa kwa kurasa za dhahabu, au mabamba. Kilizikwa katika kilima karibu na nyumbani kwao Joseph. Kitabu hicho kilihusu watu ambao waliishi katika mabara ya Amerika miaka mingi iliyopita. Moroni alisema Mungu angemsaidia Joseph kutafsiri kitabu hicho.

Joseph Smith akichungulia ndani ya shimo ili kuona hayo mabamba ya dhahabu

Joseph alikwenda kwenye kilima na kukuta mabamba hayo chini ya jiwe zito. Moroni alikuja na kusema kwamba Joseph bado hakuwa tayari kuyachukua.

Malaika Moroni akizungumza na Joseph Smith

Joseph alipokuwa mkubwa, Moroni alikutana naye juu ya kilima na kumpatia yale mabamba. Moroni alimwambia Joseph ayatunze salama.

Joseph Smith akizungumza na familia

Joseph alianza kutafsiri mabamba yale katika lugha ya Kiingereza. Alitumia vifaa maalumu kutoka kwa Mungu ili kumsaidia. Kitabu hicho kilichapishwa mwaka 1830 kama Kitabu cha Mormoni. Kinafundisha kuhusu Yesu Kristo na injili Yake.

Ukurasa wa Kupaka Rangi

Ninaweza Kuwa Shahidi Kwamba Kitabu cha Mormoni Ni cha Kweli.

Ukurasa wa kupaka rangi wa msichana akikumbatia Kitabu cha Mormoni

Kielelezo na Corey Egbert

Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia wengine kujifunza kuhusu Yesu Kristo katika Kitabu cha Mormoni?